*WAZIRI WA FEDHA ASHIRIKI MAZUNGUMZO YA WAZIRI MKUU NA MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA DUNIA*

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ameshiriki kikao cha Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba Madelu, alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayesimamia Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika, Dkt. Zarau Wendeline Kibwe, leo Agosti 28, 2026, katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Bungeni jijini Dodoma.

Mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha na kuendeleza ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii, pamoja na kujadili maeneo muhimu ya ushirikiano yenye lengo la kuongeza fursa za maendeleo kwa wananchi.

Ushiriki wa Waziri wa Fedha katika kikao hicho unaendelea kusisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Tanzania na Benki ya Dunia, hususan katika kuimarisha utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya Taifa, kuongeza uwekezaji katika miradi ya kimkakati na kuendeleza juhudi za Serikali za kujenga uchumi jumuishi na endelevu.

Benki ya Dunia imekuwa mshirika muhimu wa maendeleo kwa Tanzania, ikishirikiana na Serikali katika maeneo mbalimbali ya kiuchumi na kijamii, ikiwa ni pamoja na miundombinu, elimu, afya, kilimo, uendelezaji wa sekta binafsi na kuimarisha mifumo ya usimamizi wa uchumi na fedha za umma.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elija Mwandumbya, Kamisha Msaidizi wa Idara ya Fedha za Nje Wizara ya fedha, Bw. Patrick Pima, Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uchambuzi wa Sera Wizara ya Fedha, Bw. Mbayani Saruni, na Maafisa wengine waandamizi wa Wizara ya Fedha.

 

WAZIRI MKUU, DKT. MWIGULU NCHEMBA, ATETA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA DUNIA KWA KUNDI LA KWANZA LA NCHI ZA AFRIKA, DKT. ZARAU WENDELINE KIBWE.*


















WAZIRI MKUU, DKT. MWIGULU NCHEMBA, ATETA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA DUNIA KWA KUNDI LA KWANZA LA NCHI ZA AFRIKA, DKT. ZARAU WENDELINE KIBWE.* – Matukio Daima Habari










*BUNGE LAMTHIBITISHA NDEJEMBI KWA ASILIMIA 100 UMAKAMU WA RAIS.*

_*Waziri Mkuu asema anatosha, kiti kimempata mtu sahihi wa kumsaidia Mheshimiwa Rais.*_

BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo (Ijumaa, Agosti 28, 2026) limemthibitisha Mheshimiwa Deogratius Ndejembi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Ndejembi amepitishwa kwa asilimia 100 ya kura zote 324 zilizopigwa na waheshimiwa wabunge, ambapo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa imani aliyoionesha kwake kwa kumteua kuwa Makamu wa Rais na katika nafasi nyingine mbalimbali za uongozi.

Pia Mheshimiwa Ndejembi amelishukuru Bunge kwa imani kubwa waliyompa kiasi cha kumpigia kura kwa asilimia mia moja.

Mapema akiwasilisha hoja ya kuthibitisha uteuzi wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Mheshimiwa Deogratius Ndejembi anatosha na ni mtu sahihi wa kumsaidia Mheshimiwa Rais katika nafasi ya Makamu wa Rais, 

akiitaja kuwa ni nafasi yenye dhamana na majukumu makubwa katika uongozi wa nchi.

“Majukumu hayo yanahitaji mtu mwenye uzoefu wa uongozi, uelewa mpana wa shughuli za Serikali, uwezo wa kufanya kazi kwa karibu na Rais, busara katika kushughulikia masuala ya kitaifa, pamoja na uwezo wa kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya Serikali,” amesema Dkt. Mwigulu.

“Mheshimiwa Rais amemteua Mheshimiwa Deogratius John Pancras Ndejembi kwa kuzingatia, pamoja na mambo mengine, uzoefu alioujenga katika uongozi wa kisiasa na katika nafasi mbalimbali za Serikali,” ameongeza Waziri Mkuu.

Dkt. Mwigulu amesisitiza kuwa uzoefu wa uongozi alionao Mheshimiwa Deogratius Ndejembi unadhihirisha kuwa ni mtu sahihi kutumikia wadhifa wa Makamu wa Rais.

“Mheshimiwa Deogratius John Pancras Ndejembi si mgeni katika uongozi wa Umma na katika siasa za nchi yetu. Kabla ya kuwa Mbunge, Mheshimiwa Ndejembi alihudumu kama Mkuu wa Wilaya katika Wilaya ya Kongwa. Mheshimiwa Spika, baada ya kuchaguliwa kuwa Mbunge, Mheshimiwa Ndejembi ameendelea kuaminiwa na Mheshimiwa Rais na kupewa majukumu mbalimbali ndani ya Serikali.”

“Amehudumu katika nafasi ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora; Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa; Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu; Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kabla ya kuhudumu kama Waziri wa Nishati,” ameongeza Waziri Mkuu.

Dkt. Mwigulu amesema katika kipindi ambacho amehudumu ndani ya Serikali, Mheshimiwa Ndejembi ameonesha uwezo wa kubeba majukumu mbalimbali na kufanya kazi katika sekta zenye mahitaji na changamoto zinazotofautiana, akisisitiza kuwa uzoefu huo ni muhimu kwa Makamu wa Rais ambaye, kwa nafasi yake, anatakiwa kuwa tayari kumsaidia Rais katika masuala mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano na kutekeleza majukumu yoyote atakayokabidhiwa kwa mujibu wa Katiba.

“Kwa kuzingatia majukumu ya Kikatiba ya Makamu wa Rais niliyoyaeleza, pamoja na uzoefu wa kisiasa, kiutawala na kiutendaji wa Mheshimiwa Deogratius John Pancras Ndejembi, Serikali inaamini kuwa ana uwezo wa kutekeleza kwa uaminifu na ufanisi majukumu ya nafasi ya Makamu wa Rais na kumsaidia Mheshimiwa Rais katika kuendeleza shughuli za Serikali na maendeleo ya Taifa letu,” amefafanua Dkt. Mwigulu.

MALI ZA HALMASHAURI MJI MAFINGA ZAFIKIA SH BILIONI 73

 

Fedelica Myovela mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga 

NA MATUKIO DAIMA MEDIA , MAFINGA

HALMASHAURI ya Mji Mafinga imeeleza kuwa ina mali zenye thamani ya takribani Sh bilioni 73, huku mali mpya zenye thamani ya Sh bilioni 3.8 zikinunuliwa katika mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2026.

Huku ofisi ya mkuu wa mkoa wa Iringa chini ya uwakilishi wa George Sangai ambae ni afisa usimamizi fedha ofisi ya mkuu wa mkoa ikiipongeza Halmashauri hiyo kuwa mkoa unajivunia sana kuwa Halmashauri ya mfano .

“Mkoa unajivunia sana mafanikio makubwa ya Halmashauri ya Mji Mafinga kweli madiwani ,watumishi na mkurugenzi mpo vizuri sana “

Aidha, taarifa za fedha za Halmashauri hiyo zinaonesha mtaji wake umefikia Sh bilioni 80.57.

Mhasibu Mkuu wa Halmashauri ya Mji Mafinga, Billiard Mlindoko

Hayo yameelezwa na Mhasibu Mkuu wa Halmashauri ya Mji Mafinga, Billiard Mlindoko, wakati akiwasilisha rasimu ya taarifa za hesabu za Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2025/2026 katika Mkutano Maalum wa Baraza la Madiwani.

Mlindoko amesema taarifa hizo zimeandaliwa kwa kuzingatia miongozo ya Serikali za Mitaa pamoja na Viwango vya Kimataifa vya Uhasibu katika Sekta ya Umma (IPSAS).

Amesema Halmashauri pia inatumia mfumo wa MUSE katika shughuli za uhasibu na ufungaji wa hesabu, ikiwa ni sehemu ya matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa fedha za umma.

“Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo miongozo ambayo tunaitumia ya Serikali za Mitaa, lakini pia kuna miongozo ya kimataifa inayojulikana kama IPSAS. Pia tunatumia mfumo wa MUSE katika ufungaji wa hesabu,” amesema Mlindoko.

Akizungumzia hatua za uandaaji na uwasilishaji wa hesabu hizo, amesema Halmashauri inatakiwa kuwasilisha rasimu ya taarifa ifikapo Agosti 31 ya kila mwaka.

Baada ya hatua hiyo, Halmashauri hupewa muda wa mwezi mmoja kufanya marekebisho yanayohitajika kabla ya taarifa kamili kuwasilishwa kwa ajili ya ukaguzi.

“Taarifa hii huwa inawasilishwa tarehe 31 Agosti ya kila mwaka na ndiyo maana leo tunawasilisha. Baada ya kumaliza tutaunganisha katika kitabu tunachotakiwa kuwasilisha ili kiwe rasimu,” amesema.

Ameongeza kuwa marekebisho yote yanapaswa kukamilishwa ifikapo Septemba 30, kwa mujibu wa mwongozo, kabla ya taarifa hizo kuwa tayari kwa ajili ya ukaguzi.

Mlindoko amesema taarifa ya hesabu inajumuisha taarifa kuhusu muundo wa Halmashauri, madiwani, kamati mbalimbali za Baraza la Madiwani, vikao, shughuli za kiuchumi pamoja na utekelezaji wa bajeti.

Pia inaonesha huduma zinazotolewa kwa wananchi, miradi ya maendeleo inayotekelezwa, mafanikio yaliyopatikana na changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali.

BAKAA YA FEDHA SH BILIONI 2.7

Akizungumzia taarifa ya hali ya kifedha (financial position), Mlindoko amesema hadi kufikia mwisho wa mwaka wa fedha, Halmashauri ilikuwa na bakaa ya fedha ya takribani Sh bilioni 2.7.

Pia ilikuwa ikidai watu na taasisi mbalimbali takribani Sh milioni 115.

“Katika mali za muda mfupi tuna bakaa ya Sh bilioni 2.7, lakini pia kuna watu tunaowadai katika Halmashauri ambapo tuna Sh milioni 115 na mchanganuo wake umeoneshwa katika taarifa hii,” amesema.

Mbali na mali za muda mfupi, amesema Halmashauri ina mali za muda mrefu (non-current assets), zikiwemo majengo, vifaa na mali nyingine zinazotarajiwa kutumika kwa kipindi kinachozidi mwaka mmoja.

Kwa mujibu wa Mlindoko, katika mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2026, Halmashauri ilinunua mali mbalimbali zenye thamani ya Sh bilioni 3.8.

“Kwa mwaka huu wa fedha ulioishia Juni 30, 2026, tumeweza kununua mali zenye thamani ya Sh bilioni 3.8. Kwa hiyo, mali zetu kwa jumla zimefikia takribani Sh bilioni 73,” amesema.

Ameeleza kuwa taarifa hiyo imeambatanishwa na mchanganuo wa mali zilizonunuliwa katika mwaka husika ili kurahisisha uhakiki na ukaguzi wa hesabu.

MADENI YA HALMASHAURI

Kwa upande wa madeni, Mlindoko amesema Halmashauri ina madeni mbalimbali ya muda mfupi, yakiwemo ya zabuni, watumishi na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Pia yapo madeni yanayohusiana na michango ya mfuko wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu pamoja na fedha za amana zinazoshikiliwa na Halmashauri kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli na miradi ya Serikali.

“Katika madeni ya muda mfupi tuna madeni ya zabuni, madeni ya watumishi, deni la NHIF na michango ya mfuko wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Pia tuna fedha za amana ambazo nazo ni deni kwa sababu fedha hizo zipo kwenye miradi ya Serikali,” amesema.

Mlindoko amesema taarifa za fedha pamoja na viambatanisho vyake zina umuhimu mkubwa katika kuhakikisha hesabu za Halmashauri zinakaguliwa kwa ufanisi, kwa kuwa wakaguzi huhitaji nyaraka na vielelezo mbalimbali kuthibitisha taarifa zilizowasilishwa.

Rasimu hiyo ya hesabu za mwisho za Halmashauri ya Mji Mafinga kwa mwaka wa fedha 2025/2026 inapaswa kujadiliwa na Baraza la Madiwani kabla ya kukamilishwa na kuwasilishwa kwa ajili ya ukaguzi.

Hesabu hizo zinaonesha hali ya kifedha ya Halmashauri, ikiwemo mali, madeni, mtaji na utekelezaji wa bajeti pamoja na majukumu mbalimbali yaliyotekelezwa katika mwaka husika.

Uandaaji na uwasilishaji wa taarifa hizo ni sehemu ya taratibu za uwajibikaji katika usimamizi wa fedha za umma, zinazolenga kuweka wazi namna rasilimali za Halmashauri zilivyokusanywa, kutumika na kusimamiwa katika mwaka wa fedha 2025/2026.

Hata hivyo chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Mufindi kupitia mwenyekiti wake wilaya George Kavenuke akimpongeza mhasibu huyo na kushauri semina ya fedha kwa madiwani kutolewa zaidi.

Reginant Kivinge Mwenyekiti wa

Halmashauri ya Mji Mafinga alisema mafanikio hayo yanatokana na ushirikino mzuri wa madiwani ,watumishi chini ya mkurugenzi Fedelica Myovela .

Hata hivyo alisema mafanikio makubwa zaidi yataendelea kuonekana iwapo madiwami na watumishi kila mmoja kutimiza wajibu wake .

Katika baraza hilo la madiwani mkurugenzi wa Halmashauri hiyo aliwakilishwa na kaimu mkurugenzi Peter Ngussa ambae alisema Halmashauri hiyo imejipanga kuendelea kutekeleza malengo yake na mipango ya serikali kupitia Dira 2050.

TAZAMA VIDEO YA BARAZA BOFYA LINK HII

Thunder Riches: Fortune Eagle, Mchezo Mpya Watingisha Meridianbet

Global Publishers
August 28, 2026
6 views
0 Comments

Ulimwengu wa michezo ya kasino umevuka kiwango kingine baada ya kuwasili kwa Thunder Riches: Fortune Eagle, mchezo mpya kabisa unaopatikana kwa kipekee kupitia Meridianbet. Huu ni ujio unaokuja na msisimko mpya kwa wapenzi wa burudani za kasino wanaopenda kujaribu michezo yenye mvuto wa kipekee. Fortune Eagle anatandaza mabawa yake na kukualika kwenye safari ambayo kila hatua inaweza kukuletea burudani na nafasi ya ushindi unaoweza kukufanya utabasamu.

Safari hii inahusu bahati, msisimko na uzoefu mpya. Ukiingia kwenye Thunder Riches: Fortune Eagle, unapata nafasi ya kujionea kile ambacho mchezo huu mpya umeandaliwa nacho. Games Global imeleta uzoefu huu mpya, huku Meridianbet ikikupa nafasi ya kuwa miongoni mwa wachezaji wa kwanza kuufurahia. Kwa wale wanaopenda kuvumbua michezo mipya, Fortune Eagle ni jina ambalo hutaki kulikosa.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Mchezo huu hauji kama burudani ya kawaida. Fortune Eagle anapochanua mabawa yake, anakupeleka kwenye safari yenye mvuto inayoweza kukufanya utake kuendelea kugundua kinachofuata. Kila wakati unaingia kwenye mchezo huu wa kasino mtandaoni, unapata nafasi ya kuishi uzoefu tofauti na kuipa bahati yako nafasi ya kuamua safari itakufikisha wapi.

Sasa ni wakati wa kuchukua hatua. Jisajili Meridianbet, ingia kwenye Thunder Riches: Fortune Eagle na ucheze. Usibaki kusikia kutoka kwa wengine kuhusu mchezo huu mpya wakati unaweza kuucheza mwenyewe. Fortune Eagle tayari amefika na anasubiri kukuonyesha ulimwengu wake wa burudani.

Bahati haipigi hodi mara mbili kila wakati, hivyo usikose ujio huu mpya. Tandaza mabawa ya burudani, fuata safari ya bahati na ugundue kinachokusubiri Meridianbet.

BONANZA LA BUNGE KULENGA AFYA NA MSHIKAMANO WA WATUMISHI

 

Na Hamida Ramadhan, Matukio Daima Media Dodoma

WIZARA 14 na Taasisi 10 zinatarajiwa kushiriki katika Bonanza la Michezo la Bunge la 13 litakalofanyika kesho jijini Dodoma, likilenga kuimarisha afya, mshikamano na mahusiano ya kikazi miongoni mwa wabunge, watumishi wa Bunge na taasisi mbalimbali za Serikali.

Bonanza hilo litafanyika kuanzia saa 12:00 asubuhi katika Viwanja vya Mipango, eneo la John Merlin Secondary School, ambapo washiriki watashindana katika michezo mbalimbali ikiwamo mpira wa wavu, mpira wa pete, kikapu, kuvuta kamba na mbio, sambamba na burudani.

Akizungumza na waandishi wa habari Bungeni Dodoma kuhusu maandalizi ya bonanza hilo, Mbunge wa Jimbo la Makete na Mwenyekiti wa Bonanza la Michezo la Bunge, Festo Richard Sanga, amesema maandalizi yamekamilika na washiriki kutoka taasisi mbalimbali wamejiandaa kwa ajili ya mashindano hayo.

Sanga amesema bonanza hilo limeandaliwa ikiwa ni sehemu ya juhudi za Bunge kuendeleza michezo miongoni mwa watumishi wake na wakati huo huo kutoa fursa ya kujenga mahusiano na taasisi zinazoshirikiana nalo.

Amesema mgeni rasmi katika bonanza hilo anatarajiwa kuwa Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu, ambaye atakuwa sehemu ya tukio hilo linalolenga kuunganisha watumishi na wadau mbalimbali kupitia michezo.

Amesema michezo ni nyenzo muhimu katika kuimarisha afya ya mwili na akili, huku ikitoa nafasi kwa watumishi kukutana katika mazingira yasiyo rasmi na kujenga urafiki na mshikamano.

Kwa upande wa udhamini, Benki ya NMB imewekeza Sh210 milioni katika kufanikisha bonanza hilo, ikiwa ni sehemu ya ushirikiano wake na Bunge pamoja na dhamira yake ya kushiriki katika shughuli zinazolenga kuleta thamani kwa jamii.

Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Benki na Serikali wa NMB, Vicky Bishubo, amesema ushirikiano kati ya benki hiyo na Bunge una historia ndefu na umejengwa katika misingi ya mahusiano ya kimkakati.

Bishubo amesema NMB inatambua nafasi ya Bunge katika maendeleo ya Taifa na itaendelea kushirikiana nalo katika shughuli mbalimbali zenye manufaa kwa jamii.

“Mahusiano yetu na Bunge ni ya kihistoria na kama mashirika ya kimkakati tunayathamini. Tunaahidi kuendelea kuboresha huduma zetu kwa jamii na wakati wowote tunahitaji muendelee kutushirikisha,” amesema Bishubo.

Amesema Sh210 milioni zilizowekezwa katika bonanza hilo ni sehemu ya dhamira ya NMB ya kurudisha thamani kwa jamii, huku michezo ikiwa miongoni mwa maeneo yanayoweza kuunganisha watu, kuhamasisha maisha yenye afya na kujenga mahusiano.

Bishubo amesema NMB imewezesha mahitaji mbalimbali ya bonanza hilo, ikiwamo vifaa vya michezo, mipira na vikombe vya washindi, ili kuhakikisha mashindano yanafanyika katika mazingira bora.

Amesema jukumu la NMB katika jamii haliishii katika kutoa huduma za kifedha pekee, bali benki hiyo pia inashiriki katika shughuli za kijamii zinazolenga kuboresha ustawi wa wananchi.

Kwa upande wake, Sanga amesema ushiriki wa wizara na taasisi hizo unalifanya bonanza hilo kuwa jukwaa la kuimarisha mahusiano ya kitaasisi, huku washiriki wakipata nafasi ya kubadilishana uzoefu na kujenga mshikamano.

Amesema pamoja na ushindani, bonanza hilo litakuwa na burudani mbalimbali zitakazowapa washiriki na wageni nafasi ya kufurahia tukio hilo.

Bonanza hilo linatarajiwa kuwa zaidi ya mashindano ya michezo, kwani litatoa fursa ya kuhamasisha maisha yenye afya na kuimarisha mahusiano kati ya Bunge, Serikali na sekta binafsi.

JAMII YAHIMIZWA KUTUMIA VYAKULA VYA MIMEA ASILI KUIMARISHA KINGA ZA MWILI

 

Na Lilian Kasenene, Morogoro

Matukio Daima Media

JAMII imehimizwa kutumia vyakula vitokanavyo na mimea, mbegu na matunda ya asili ili kuimarisha kinga za mwili na kujikinga na magonjwa sugu.

Mkurugenzi wa HOPECA Products na Amra Gogondi, Dk Manimba Daniel, alisema vyakula vinavyotokana na mimea na mbegu za asili vina vitamini na virutubisho muhimu vinavyosaidia kutunza na kurekebisha mwili.

Alisema jamii inapaswa kubadilisha mtindo wa maisha kwa kutumia vyakula vya asili, kufanya mazoezi mepesi na endelevu kwa ajili ya kuchangamsha mwili, pamoja na kuhakikisha inapata muda wa kutosha wa kupumzika.

Dk Daniel alisema unga wa HOPECA ni tiba lishe unaotokana na mchanganyiko wa aina 20 za mbegu za mimea pamoja na matunda mbalimbali ya asili, hivyo kuwa na virutubisho mbalimbali muhimu mwilini.

“HOPECA ni mchanganyiko wa vitamini C, nyuzinyuzi na madini ambayo yanasaidia kuimarisha kinga ya mwili, kuboresha homoni na kusaidia kuondoa uchafu mwilini,” alisema Mkurugenzi huyo.

Akizungumza kwenye Tamasha la Utamaduni wa Tanzania lilnalo3nd3lea mkoani Morogoro, Dk Daniel alisema pia unga wa tunda la Amra Gogondi, ambalo ni tundapori, unasaidia kusafisha damu na kuondoa mafuta yasiyofaa mwilini.

“Chai ya Amra inachangamsha mwili, inayeyusha mafuta kwenye damu, inapunguza cholesterol na kusaidia kuondoa uchafu kwenye utumbo unaotokana na mabaki ya vyakula,” alisema Dk Daniel.

Alisema unga wa Amra pia unasaidia kukarabati mwili kwa kuchochea uzalishaji wa chembe hai mpya zinazosaidia mwili kupambana na maradhi.

Doumbia Bado Anajitafuta! Ashindwa Kutamba Dhidi ya Coastal

Shechambo Chris
August 28, 2026
18 views
0 Comments

Mshambuliaji wa Simba SC, Ibrahim Doumbia bado anajitafuta kutokana na kushindwa kufungua ukurasa wa mabao katika mechi 4 za ligi zilizochezwa na vinara 2026/27.

Raia huyo wa Mali alianza kikosi cha kwanza Agosti 27,2026 ubao wa Uwanja wa Meja Jen. Isahmuyo uliposoma Simba SC 1-0 Coastal Union, Bao la ushindi kwenye mchezo huo lilifungwa na Ismail Toure dakika ya 74.

Rekodi zinaonyeshwa kuwa Doumbia alitumia dakika 63 uwanjani baada ya Kocha Mkuu, Steve Barker kumpa nafasi kuanza kupambania nembo ya timu hiyo.

Katika dakika hizo Doumbia alifanya jaribio moja la hatari dakika ya 9 kwa mguu wa kulia. Jaribio hilo liligonga mwamba na kurejea uwanjani.

Majaribio mengine aliyofanya ilikuwa dakika ya 20 kwa pigo la kichwa akitumia pasi ya kona iliyopigwa na Libase Gueye. Dakika ya 24, 27, 36, 57.

Alionyeshwa kadi ya njano dakika ya 59 kwa kumchezea faulo nyota wa Coastal Union, Alichezewa faulo dakika ya 21.

Licha ya balaa ambalo alionyesha uwanjani, Doumbia hajapata bahati kufunga ndani ya ligi na timu yake inaongoza ligi ikiwa na pointi 12.

Safu ya ushambuliaji ya Simba SC imefunga jumla ya mabao 7, Toure na Clatous Chama kila mmoja amefunga mabao mawilimawili.
Lunyamadzo Mlyuka, DarTU

WANANCHI URU KUSINI WACHANGIA ZAIDI YA MILIONI 200 KUKARABATI SHULE

 

Na Matukio Daima Media, Moshi

WANANCHI wa Kata ya Uru Kusini, Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, wameonyesha nguvu ya ushirikiano kwa kuchangisha zaidi ya shilingi milioni 200 na kuzitumia kukarabati Shule ya Msingi Kimanganuni iliyokuwa na baadhi ya majengo chakavu.

Ukarabati huo umehusisha kubomoa baadhi ya majengo yaliyokuwa katika hali mbaya na kujenga miundombinu mipya ikiwemo vyumba vya madarasa, vyoo, maji, umeme pamoja na kuweka majiko yanayotumia nishati safi kupikia.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ukarabati wa shule hiyo, Leonard Kisarika, amesema fedha hizo zimetokana na michango ya wananchi pamoja na wanafunzi wa zamani waliosoma shuleni hapo tangu mwaka 1965.

Kisarika amesema hatua hiyo imeonyesha kuwa wananchi wanaweza kushirikiana katika kutatua changamoto za maendeleo ya jamii badala ya kusubiri kila jambo lifanywe na Serikali.

Kwa upande wake, Wakili Octavian Kiwale, ambaye ni miongoni mwa wanafunzi waliowahi kusoma katika shule hiyo, amesema wahitimu wameona umuhimu wa kurudisha kwa jamii walichopata kupitia shule hiyo kwa kushiriki katika ukarabati wake.

Kiwale amesema shule hiyo ina historia kubwa kwa jamii ya Uru Kusini na kwamba kuboresha mazingira yake ni uwekezaji katika elimu ya watoto wa kizazi cha sasa.

Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Ukarabati,Gaudens Anizeth Mushi, amesema ushiriki wa wananchi na wahitimu katika kuboresha shule hiyo ni mfano wa namna jamii inavyoweza kuunganisha nguvu zake katika kuharakisha maendeleo.

Akizungumzia hali ya shule hiyo, Mkuu wa Shule ya Msingi Kimanganuni, Hadija Mfinanga, amesema ukarabati huo umebadilisha mazingira ya shule na kuwapa wanafunzi mazingira bora zaidi ya kujifunzia.

Mfinanga amesema pamoja na maboresho hayo, bado shule hiyo inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa madawati zaidi ya 50.

Amesema maboresho hayo yana umuhimu mkubwa kwa wanafunzi na walimu, kwa kuwa mazingira bora ya shule yana mchango katika kuboresha ufundishaji na ujifunzaji.

Hata hivyo, viongozi wa shule na wadau hao wameendelea kuomba ushirikiano wa jamii katika kukamilisha mahitaji yaliyobaki, hususan upatikanaji wa madawati.

Mwisho

UN YAITAKA TANZANIA KUSITISHA UHAMISHAJI WA WAMASAI NGORONGORO NA LOLIONDO

 

Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Kutokomeza Ubaguzi wa Rangi (CERD) imeitaka Tanzania kusitisha mara moja kile ilichokitaja kuwa uhamishaji wa nguvu wa jamii ya Wamasai kutoka makazi ya mababu zao katika Ngorongoro na Loliondo.

Katika taarifa iliyotolewa Ijumaa, Agosti 28, kamati hiyo ilieleza wasiwasi kuhusu madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu dhidi ya jamii hiyo, ikiwemo kufukuzwa na kuhamishwa kwa nguvu, pamoja na vikwazo vya kupata ardhi za mababu, maeneo ya makazi na rasilimali za asili.

CERD pia iliitaka serikali ya Tanzania kuchunguza na kushughulikia madai ya ukiukwaji wa sheria yaliyoripotiwa, yakiwemo kukamatwa holela kwa baadhi ya wakazi na matumizi ya nguvu kupita kiasi na vyombo vya dola.

Kamati hiyo ilisema Tanzania inapaswa kurejesha na kuboresha upatikanaji wa huduma za msingi katika maeneo husika, zikiwemo elimu, huduma za afya, maji safi na huduma za usafi wa mazingira.

Aidha, ilitoa wito kwa mamlaka za Tanzania kuhakikisha mazingira salama kwa watetezi wa haki za binadamu, mashirika ya kiraia, wanaharakati, wanasheria na waandishi wa habari wanaoshughulikia masuala yanayohusu haki za jamii za wenyeji.

Katika mapendekezo yake, CERD iliitaka Tanzania kutangaza haraka matokeo na mapendekezo ya tume mbili za rais zilizoundwa Februari 2025 kuchunguza sera za matumizi ya ardhi, uhamishaji wa wakazi na uhifadhi ndani ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.

Kamati hiyo pia ilisisitiza umuhimu wa kuhakikisha jamii ya Wamasai inashirikishwa kikamilifu katika maamuzi yanayohusu mustakabali wa maeneo wanayoishi na kuyategemea kwa maisha yao.

Serikali ya Tanzania mara kadhaa imekuwa ikisisitiza kuhusu matumizi ya maeneo hayo kwa manufaa ya umma, ikizingatia sheria na masuala ya haki za binadamu.