‘NCHIMBI SIO CHAWA’ – WARIOBA

 

Waziri Mkuu wa zamani na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Tanzania, Joseph Warioba, amesema aliyekuwa Makamu wa Rais Emmanuel Nchimbi sio “chawa” wa viongozi, akisema misimamo yake ya kisiasa imetokana na kile anachoamini.

Akizungumza kwenye Jukwaa la Demokrasia Tanzania lililofanyika leo Agosti 28, 2026, makao makuu ya chama cha wanasheria Tanganyika (TLS), jijini Dar es Salaam, Warioba amesema kwa muda wote ambao amekuwa akimfahamu Nchimbi, hajawahi kumwona akimsifia kiongozi kwa lengo la kujipendekeza, akisema msimamo huo ameendelea nao tangu alipokuwa kijana ndani ya Chama Cha Mapinduzi, CCM.

“Navyomfahamu Nchimbi, kitu kimoja, Nchimbi si chawa wa aina yoyote. Alipokuwa kwenye chama hakuwa chawa na vijana wenzake na ameendelea hivyo hivyo,” amesema Warioba.

Amesema kauli mbalimbali zilizotolewa na Nchimbi katika nafasi zake za uongozi zilikuwa zikieleza mtazamo wake binafsi kuhusu namna siasa zilivyopaswa kuendeshwa nchini.

Warioba ametaja tukio la kukamatwa kwa baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Chadema, akiwemo John Heche, ambapo Nchimbi akiwa Katibu Mkuu wa CCM alitoa wito wa kuachiliwa kwa viongozi hao.

“Kuna wakati kina viongozi wa Chadema walikamatwa, kina Heche. Nchimbi akiwa Katibu Mkuu alisema, waachieni, tushindane kisiasa,” amesema Warioba.

Ameeleza pia kwamba wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2024, Nchimbi alizungumza kuhusu hatua alizochukua baada ya kumuona Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Rais wa Tanzania.

Kwa mujibu wa Warioba, Nchimbi alitaka kile alichokiita “mambo madogo madogo” yaachwe na vyama vishindane kisiasa.

Kwa mujibu wa Warioba, kauli hizo zilikuwa sehemu ya misimamo ya Nchimbi kuhusu uongozi na ushindani wa kisiasa.

“Ni misimamo alikuwa anaitoa, tofauti ya uongozi,” amesema.

Warioba pia amenukuu kauli ambayo amesema Nchimbi aliwahi kuitoa kuhusu namna ya kukosoa makosa ndani ya CCM, akirejea ahadi ya wana-CCM “Nitasema kweli daima, fitina mwiko, iko kwenye ahadi zetu”, anasema Warioba na kuongeza “lakini siku hizi ukisema ukwlei umeanzisha fitina”.

Nchimbi alitangaza kujiuzulu nafasi ya makamu wa Rais wiki hii, kabla ya kuvuliwa uanachama wa CCM, akisema ameamua kustaafu siasa pia. CCM ilisema imemfukuza kwa sababu za kinidhamu.

TUME YA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI YAANZA UKAGUZI KWA WAKUSANYAJI NA WACHAKATAJI WA TAARIFA HIZO NCHINI.

 Na Mwandishi Wetu.

Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) imeanza zoezi la ukaguzi wa uzingatiaji wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Sura ya 44, kwa kutembelea taasisi, mashirika na wafanyabiashara wanaokusanya na kuchakata taarifa binafsi nchini.

Hayo yameelezwa leo, Agosti 28, 2026 jijini Dodoma na Mkurugenzi Mkuu wa PDPC, Dkt. Emmanuel Mkilia wakati akizungumza na vyombo vya habari ambapo amesema ukaguzi huo wa kutembelea taasisi, mashirika na wafanyabiashara mbalimbali nchini unalenga kujiridhisha iwapo wakusanyaji na wachakataji wa taarifa binafsi wanazingatia matakwa ya sheria katika shughuli zao.

Miongoni mwa mambo yatakayokaguliwa ni usajili wa taasisi katika rejesta ya Tume, utekelezaji wa majukumu ya Afisa Ulinzi wa Taarifa (DPO) katika taasisi husika, pamoja na namna taarifa binafsi zinavyokusanywa, kuchakatwa na kuhifadhiwa ili kuhakikisha taratibu zilizowekwa kisheria zinafuatwa.

Eneo jingine litakalokaguliwa ni utaratibu unaotumika kusafirisha taarifa binafsi nje ya nchi, kwa kuzingatia masharti yaliyowekwa chini ya Vifungu vya 31 na 32 vya Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi.

Aidha, PDPC imeeleza kuwa itachunguza hatua zinazochukuliwa na taasisi katika kulinda taarifa binafsi dhidi ya upotevu, uteketezaji, ubadilishaji au kuchakatwa bila idhini, kama inavyoelekezwa katika Kifungu cha 27(1) cha sheria hiyo.

Ukaguzi huo ni moja ya majukumu ya Tume na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya taasisi, mashirika au wafanyabiashara watakaobainika kutokidhi matakwa ya sheria, ikiwamo kutolewa kwa adhabu na faini kwa mujibu wa sheria.

HALMASHAURI YA MAFINGA MJINI HATUJAFUKUZA WATUMISHI WA AFYA BADO TUNAUHITAJI -KAIMU MKURUGENZI

 

  

NA MATUKIO DAIMA MEDIA 

MAFINGA.

Halmashauri ya Mji Mafinga imekanusha taarifa iliyotolewa na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mji Mafinga, Dkt. Victor Msafiri, kuhusu madai ya kufukuzwa kazi kwa madaktari saba waliokuwa wakihudumu katika hospitali hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa mafinga  Peter ngussa alieleza kuwa taarifa hiyo ilitolewa katika mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini,Dickson Nathan Lutevele ‘Villa’, uliofanyika Agosti 24, 2026, wakati wa kusikiliza kero za wananchi na wafanyabiashara wa Soko Kuu la Mafinga.

Katika mkutano huo, ilidaiwa kuwa madaktari saba waliokuwa wakifanya kazi katika Hospitali ya Mji Mafinga wamefukuzwa kazi, huku baadhi yao wakielezwa kupangiwa majukumu ya kufanya kazi kwenye gari la Halmashauri linalotumika kubeba taka.

Aidha, katika taarifa hiyo ilidaiwa kuwa kuna madaktari wengine ambao mchakato wa kinidhamu dhidi yao unaendelea kutokana na tuhuma mbalimbali za kiutumishi.

“Hakuna daktari yeyote aliyefukuzwa kazi na kwamba madaktari wote waliopo katika Halmashauri hii wanaendelea na ajira zao na majukumu yao kama kawaida,Halmashauri pia imekanusha taarifa kwamba kuna watumishi walioondolewa kwenye majukumu ya kada zao na kupewa majukumu mengine, ikiwemo kufanya kazi ya ukusanyaji au usafirishaji wa taka kwa kutumia magari ya Halmashauri”alisema

Aidha, Ngusa  amesema hakuna mchakato wowote wa kinidhamu unaoendelea dhidi ya wataalamu wa afya, hivyo taarifa zilizotolewa kuhusu suala hilo hazina ukweli kwa mujibu wa ufafanuzi uliotolewa na mamlaka hiyo.

Kutokana na taarifa hizo zinazodaiwa kupotosha na kusababisha taharuki miongoni mwa wananchi, Halmashauri ya Mji Mafinga imeomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza, huku ikieleza kuwa itachukua hatua kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu zinazosimamia Utumishi wa Umma.

TAZAMA VIDEO YA KAIMU MKURUGENZI BOFYA HAPA

Halmashauri imesisitiza kuwa pale inapobainika mtumishi ana tuhuma au amefanya kosa la kiutumishi, hatua za kinidhamu huchukuliwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma, na kwamba hatua hizo hazipaswi kutafsiriwa au kuwasilishwa kwa umma kwa namna inayoweza kusababisha upotoshaji na taharuki.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Mafinga Reginant Kivinge  akizungumzia taarifa hiyo katika Mkutano maalumu wa baraza la madiwani wa kujadili rasimu ya taarifa za hesabu za halmashauri ya mji wa mafinga kwa mwaka wa fedha unaoishia june 30,2026. 

Amesema taarifa zinazoeleza kuwa Halmashauri ya Mafinga imewafukuza baadhi ya watumishi si za kweli na hazipaswi kuchukuliwa kama taarifa rasmi kutoka kwenye mamlaka husika.

Aidha, amezitaka vyombo vya habari na wananchi kutopotoshwa na taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu hali ya watumishi katika halmashauri hiyo.

 “Kwa niaba ya Baraza la Madiwani na kwa niaba ya Halmashauri, kama Mwenyekiti wa Halmashauri nakanusha taarifa hiyo, Hatujafukuza watumishi na hakuna watumishi walioondolewa kwa suala lolote la utovu wa nidhamu,” amesema.

Ameongeza kuwa watumishi waliopo katika idara mbalimbali wanaendelea na majukumu yao kama kawaida na wamekuwa wakitekeleza kazi zao kwa weledi.

“Changamoto zinazojitokeza katika utendaji zimekuwa zikishughulikiwa kwa njia ya mazungumzo kati ya watumishi, viongozi wa halmashauri na Baraza la Madiwani,licha ya kuwepo kwa changamoto mbalimbali katika utendaji, viongozi, madiwani na watumishi wamekuwa wakishirikiana katika kuzitatua na kujengana kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora”alisema

Mwenyekiti amesema Halmashauri ya Mafinga inaendelea kufanya kazi kwa utulivu na ushirikiano, huku watumishi katika idara mbalimbali wakiendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi.

Mwenyekiti huyo ameeleza kuwa lengo kubwa la halmashauri ni kuhakikisha Mafinga inafikia maendeleo yanayotarajiwa na wananchi, hususan katika utoaji wa huduma kwa jamii.VIDEO YA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA MJI MAFINGA BOFYA HAPA

Aidha, amezitaka vyombo vya habari na wananchi kutopotoshwa na taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu hali ya watumishi katika halmashauri hiyo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mufindi George Kavenuke amewataka Madiwani kuendelea kushirikiana na wakuu wa Idara pamoja na wataalamu wa halimashauri hiyo ili kuendelea kutekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi.

“ushirikiano wa chama na serikali ni mzuri katika Halmashauri ya Mufindi kuhakikisha miradi inafanikiwa kwa manufaa ya wananchi,hasa katika utendaji wa fedha nampongeza mhasiku amewasirisha taarifa vizuri kuhusu hali ya kifedha, madeni na mapato na matumizi”alisema Kavunike

TAZAMA BARAZA ZIMA LA MADIWANI BOFYA LINK HII

MWISHO.

SERIKALI KUTUMIA SH1.39 TRILIONI KUKARABATI VIFAA TIBA

Na Hamida Ramadhan,Matukio Daima Media DODOMA.

 SERIKALI inatarajia kutumia Sh1.39 trilioni hadi mwaka 2036 katika matengenezo ya vifaa tiba nchini, hatua inayolenga kuhakikisha mashine zinazotumika hospitalini zinaendelea kufanya kazi na wananchi kupata huduma za afya kwa wakati.

Kaimu Mganga Mkuu wa Serikali, Dk. Eliudi Eliakimu, amesema fedha hizo zitatumika katika kuimarisha matengenezo ya vifaa tiba, huku akibainisha kuwa Serikali inakadiriwa kutumia wastani wa Sh139.5 bilioni kwa mwaka katika eneo hilo.

Dk. Eliakimu amesema hayo Alhamisi, Agosti 27, 2026, jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa Mwongozo wa Usimamizi wa Vifaa Tiba pamoja na mafunzo kwa wahandisi na watumiaji wa vifaa hivyo.

Amesema pamoja na Serikali kuendelea kununua na kusambaza vifaa tiba katika vituo vya afya na hospitali za ngazi mbalimbali, baadhi ya vifaa vimekuwa vikisimama kufanya kazi vinapoharibika kutokana na ukosefu wa fedha za matengenezo.

Kutokana na hali hiyo, amewaagiza Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Wakurugenzi wa hospitali kutenga asilimia 10 ya mapato ya hospitali kwa ajili ya matengenezo ya vifaa tiba.

“Ni aibu kwa hospitali kuwa na vifaa tiba vya kisasa lakini havifanyi kazi kutokana na kukosa fedha za matengenezo.

Ninawaagiza leo RMO, DMO na Wakurugenzi Watendaji kuhakikisha

 mnatenga asilimia 10 ya mapato yenu na kuielekeza kwenye matengenezo ya vifaa tiba ili wananchi wasikose huduma,” amesema Dk. Eliakimu.

Aidha, amesema hospitali zinapaswa kutenga asilimia moja ya mapato yake kwa ajili ya kujenga uwezo wa wahandisi na mafundi wa vifaa tiba, ili waweze kufanya matengenezo ya vifaa vinapoharibika.

Mshauri Mwelekezi kutoka Wizara ya Afya, Gerald Mrema, amesema Mwongozo wa Usimamizi wa Vifaa Tiba utasaidia kuweka utaratibu wa kuhakikisha vifaa vilivyonunuliwa vinaendelea kutumika badala ya kuachwa vinapoharibika.

Amesema utekelezaji wa mwongozo huo utasaidia kupunguza malalamiko ya wananchi wanaokosa huduma kutokana na mashine kuharibika, kwa kuwa hospitali zitakuwa na mipango na bajeti maalumu za matengenezo.

“Kwenye hospitali zetu kuna vifaa vingi ambavyo havifanyi kazi wengine hawana hata ofisi za watumishi kufanyia kazi, lakini kuna vyumba maalumu vya kuhifadhi mashine mbovu baada ya mwongozo huu hatutarajii kukuta mashine haifanyi kazi kutokana na ubovu,” amesema Mrema.

Kwa upande wake, Mhandisi wa Vifaa Tiba kutoka Taasisi ya Ifakara Health Institute, Hope Peter, amesema taasisi hiyo inaunga mkono jitihada za Serikali za kuboresha usimamizi na matengenezo ya vifaa tiba nchini.

Amesema kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, wamekuwa wakitoa mafunzo ya matengenezo ya vifaa tiba kwa wahandisi na mafundi kutoka vituo 25 vya kutolea huduma za afya.

“Mwongozo huu utasaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha utendaji kazi wa wahandisi wa vifaa tiba na hospitali kwa ujumla, kuhakikisha vifaa vinakuwa katika hali nzuri na huduma zinapatikana pale zinapohitajika,” amesema Peter.

Hata hivyo, amesema sekta hiyo bado inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa wahandisi na mafundi wa vifaa tiba, mazingira duni ya kufanyia kazi pamoja na uhaba wa vipuri.

Amesema vifaa vingi vya tiba hununuliwa kutoka nje ya nchi na vinapoharibika, upatikanaji wa vipuri huwa changamoto, hali inayosababisha baadhi ya mashine kukaa muda mrefu bila kufanya kazi.

Peter ameshauri Serikali kuongeza idadi ya wataalamu wa vifaa tiba, kutenga bajeti maalumu ya matengenezo na ununuzi wa vipuri, pamoja na kuboresha mazingira ya kazi kwa kujenga karakana na maeneo salama ya kuhifadhi na kufanyia matengenezo vifaa hivyo.

Amesema hatua hizo zitasaidia kuongeza muda wa matumizi ya vifaa tiba, kuboresha ufanisi wake na kuhakikisha wananchi wanapata huduma wanazohitaji kwa wakati.

Mwisho

Crystal Palace dhidi ya Manchester City Kutimua Vumbi EPL

Leo usiku, saa 22:00, mashabiki wa mpira wa miguu watashuhudia mechi ya kuvutia kati ya Crystal Palace na Manchester City katika Ligi Kuu Uingereza, ikichezwa Selhurst Park. Hii ni mechi ya wiki ya pili ya msimu, na pande zote mbili zinaingia na hamasa tofauti kabisa kutokana na matokeo ya mechi zao za ufunguzi.

Upande wa Crystal Palace, msimu haujaanza vizuri. Timu ilifungwa 2-0 mbali dhidi ya Everton, ikifungwa mabao katika kipindi cha kwanza kupitia Kiernan Dewsbury-Hall na Thierno Barry. Kocha Pierre Sage atakuwa na shinikizo la kuhakikisha timu yake inarudi na matokeo mazuri mbele ya mashabiki wao wenyewe, hasa baada ya kuanza msimu wakiwa chini kabisa ya msimamo.

Manchester City kwa upande mwingine wanaingia mechi hii na kishindo, baada ya kupata ushindi wa kusisimua dhidi ya Bournemouth wiki iliyopita. Walikuwa nyuma kwa bao moja kabla ya kufunga mabao mawili ya mwisho kupitia Marc Guéhi dakika ya 83 na Joško Gvardiol dakika ya 90 kuiba ushindi 2-1.

Chini ya uongozi mpya wa Enzo Maresca, City wanaonekana kuwa na mtindo wa moja kwa moja zaidi wa kushambulia, ingawa ulinzi wao bado unaonekana kuwa na mapungufu kidogo ukilinganisha na enzi za Guardiola.

Meridianbet inasema kuna michezo kama Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli. Ingia katika kasino ya mtandaoni ya Meridianbet na ujiokotee mkwanja mapema.  Jiunge sasa au Tembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kimbinu, mifumo inayotarajiwa kuchezea inaonyesha Palace watakuwa na muundo wa ulinzi imara wa 3-4-2-1, huku Jean-Philippe Mateta akiwa mtu wa kutegemewa mbele. City watategemea nguvu ya Erling Haaland pamoja na ubunifu wa Phil Foden na Antoine Semenyo katika muundo wao wa 4-2-3-1. Wachezaji wawili muhimu Chadi Riad (Palace) na Jérémy Doku (City) watakosa mechi hii kutokana na majeraha.

Takwimu za kihistoria zinaonyesha wazi ubora wa City dhidi ya Palace kati ya mechi 27 zilizopita, City wameshinda mara 20, huku Palace wakiwa na ushindi 4 tu na sare 5. Msimu uliopita pekee, City waliwafunga Palace mabao 3-0 mara mbili mfululizo.

BIBI ANAYEISHI NA WATOTO WENYE CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI AFUTWA MACHOZI NA DKT.TULIA

 

Na Matukio Daima Media, Mbeya

 BIBI Grace Deya (70), mkazi wa Mtaa wa Tembela, Kata ya Tembela katika Jimbo la Uyole mkoani Mbeya amefutwa machozi baada ya Taasisi ya Tulia Trust kuamua kumjengea nyumba kutokana na hali ngumu ya maisha anayokabiliana nayo pamoja na watoto wake watatu wenye changamoto za afya ya akili.

Bibi huyo amekuwa akiishi katika nyumba chakavu na kutegemea msaada kutoka kwa majirani, huku akitakiwa kuwahudumia watoto wake ambao ni watu wazima na wenye changamoto za afya ya akili.

Akizungumza na waandishi wa habari Agosti 27,2026 kuhusu mpango wa ujenzi wa nyumba hiyo, Ofisa Uhusiano na Mahusiano wa Taasisi ya Tulia Trust, Joshua Mwakanolo, amesema uamuzi wa kumsaidia Bibi Deya umefikiwa baada ya uongozi wa Mtaa na Kata ya Tembela kufanya tathmini na kubaini kuwa familia hiyo inakabiliwa na changamoto kubwa.

Mwakanolo amesema ujenzi huo ni sehemu ya shughuli za Taasisi ya Tulia Trust katika kuadhimisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake, huku wakilenga kuhakikisha nyumba hiyo inakamilika na kukabidhiwa kwa familia hiyo ifikapo Septemba 25, 2026.

«“Sisi Taasisi ya Tulia Trust kwa kushirikiana na uongozi wa kata hii tumeangalia changamoto alizonazo huyu bibi na kubaini kuwa ni kubwa zaidi kuliko familia nyingine. Kwa kuwa tunaadhimisha miaka 10 ya Tulia Trust, tunaamini nyumba hii itajengwa kwa haraka zaidi na tutaikabidhi Septemba 25 mwaka huu, siku moja kabla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 10 ya Tulia Trust,” amesema Mwakanolo.»

Amesema hadi sasa Taasisi hiyo imejenga jumla ya nyumba 26 katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Mbeya, ambapo nyumba mbili zimejengwa mkoani Morogoro na nyingine mkoani Ruvuma.

Akizungumza kupitia mkalimani, Diwani wa Kata ya Tembela, kutokana na kutokujua kuzungumza Kiswahili, Bibi Deya amesema amekuwa akikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kupata chakula, mavazi, malazi na mahitaji mengine muhimu ya kila siku.

«“Nawashukuru sana ndugu zangu na hasa Tulia kwa kuniona mimi, kwa sababu maisha yangu yalikuwa magumu. Nilikuwa naishi kwa kuomba. Mume wangu alifariki miaka 10 iliyopita na watoto wangu wana changamoto za afya ya akili,” amesema.»

Kwa upande wake, ndugu wa Bibi Deya, Kimaro Mwayonga, amesema bibi huyo amekuwa akipitia maisha magumu kutokana na kuishi na watoto wake ambao ni watu wazima na wenye changamoto za afya ya akili.

«“Watoto hawa walikuwa wanamfanyia vitu vibaya mama yao na kumtesa. Kwa ujumla, hali ya huyu mama ni ngumu. Amekuwa akiishi kwa kuomba kwa majirani ili maisha yaweze kuendelea yeye na watoto wake ambao ni watu wazima,” amesema.»

Diwani wa Kata ya Tembela, Frank Mwasyoke, amesema mbali na ujenzi wa nyumba hiyo, Dkt. Tulia amekuwa akisaidia wananchi katika huduma za afya, ambapo zaidi ya wananchi 300 wamewezeshwa kupata bima ya afya tangu alipoanza kutoa msaada huo.

«“Mheshimiwa Dkt. Tulia anafanya mambo makubwa katika kata yetu. Tuna kila sababu ya kumshukuru na kumuombea Mungu amwongoze zaidi. Katika historia ya wabunge waliowahi kuongoza Jimbo la Mbeya, tunaona namna ambavyo amegusa maisha ya wananchi wa chini. Leo wana Tembela tunatabasamu kwa msaada huu,” amesema Mwasyoke.

Mwisho.

Tanzania, DR Congo wakubaliana kuwarejesha wakimbizi – HabariLeo

LUBUMBASHI: Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), pamoja na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), zimeazimia kuanza mchakato wa kuwarejesha wakimbizi wa DRC wanaohifadhiwa nchini Tanzania ambao wako tayari kwa hiari yao kurejea nchini kwao.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Ayoub Mohammed Mahmoud, wakati akihutubia Mkutano wa Kamisheni ya Pande Tatu (Tripartite Commission Meeting) uliofanyika jijini Lubumbashi leo

Ayoub amesema Tanzania itaendelea kuhakikisha wakimbizi wanaoamua kurejea nchini kwao wanafanya hivyo kwa hiari na utaratibu wa kuwarejesha utazingatia usalama na utu wao na pia Tanzania haitawahamasisha au kuwashawishi wakimbizi hao kurejea nyumbani.

Ayoub ameeleza kuwa kwa wale ambao bado hawajawa tayari kurejea DRC, Tanzania itaendelea kuwapa hifadhi na kuwahudumia kulingana na rasilimali zilizopo, katika Kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu mkoani Kigoma.

Aidha, amesisitiza kuwa kuanza kwa mchakato wa urejeshaji wa hiari hakutaizuia Tanzania kuendelea kupokea waomba hifadhi wapya wanaokimbilia Tanzania kutokana na ukosefu wa usalama katika baadhi ya maeneo ya DRC.

Aidha, ametoa Wito kwa viongozi wa DRC kutembelea Kambi ya Nyarugusu ili kukutana moja kwa moja na raia wao, kusikiliza mahitaji yao ili wajisikie kuwa sehemu ya taifa lao. Amesema ziara hizo hazipaswi kuwa za kuwashawishi wakimbizi kurejea, bali kujenga uhusiano na matumaini kwa raia hao.

 

Kadhalika, pande zote zimekubaliana kuweka mazingira wezeshi kwa wakimbizi waliotayari kurejea nchini kwao ili kuungana na familia zao na kushiriki katika ujenzi na maendeleo ya taifa lao.

POLISI YAWATAKA WANANCHI KUWAJUA JIRANI ZAO

 Na Lilian Kasenene, Morogoro

maipacarusha20@gmail.com

JESHI la Polisi nchini limewataka wananchi kuwajua majirani zao na wageni wanaoingia katika maeneo yao ili kulinda amani na kukomesha uhalifu. 

Kamishna wa Polisi Jamii Tanzania, CP Alex Mukama, alisema hayo katika Tamasha la Nne la Utamaduni wa Tanzania linaloendelea mkoani Morogoro.

Alisema ni muhimu kila mwananchi kumtambua jirani yake na kufahamu wageni wanaoingia katika eneo lake, pamoja na kujua iwapo wapo nchini kihalali.

“Huku kuna Polisi Jamii, Uhamiaji wana kaulimbiu ya ‘Mjue Jirani’ na sisi ni nyumba moja. Lengo ni kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa mlinzi wa amani popote alipo,” alisema CP Mukama.

Alisema wakati Jeshi hilo likiadhimisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwa Polisi Jamii, limeendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kutunza amani, kupinga vitendo vya uhalifu na kufanya shughuli za kuinua uchumi.

“Hatuwakatai wageni, lakini ni lazima tujue kama wageni hao wako nchini kwa kufuata sheria na taratibu na kama shughuli zao zinatambulika,” alisema CP Mukama.

CP Mukama alilitaka Jeshi la Polisi kuendelea kutoa elimu kwa wananchi na kushirikiana na Polisi Jamii katika kukomesha uhalifu kwenye maeneo yao na taifa kwa ujumla.

Aliongeza kuwa Jeshi hilo pia linaendelea kutoa elimu kuhusu madhara ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya kwa lengo la kulinda jamii, hasa vijana.

TAMASHA LA UTAMADUNI

Wakizungumza katika tamasha hilo, baadhi ya washiriki walilishukuru Serikali kwa kuanzisha tamasha hilo, wakisema linasaidia kuikumbusha jamii umuhimu wa kulinda na kutunza utamaduni wa Tanzania.

“Mikusanyiko ya aina hii ni muhimu ili kuwaonyesha vijana umuhimu wa kulinda mila na tamaduni za jamii zetu,” alisema Yusuphu Kilulu kutoka mkoani 

Alisema kizazi cha sasa kimeanza kupuuza matumizi ya vyakula na vinywaji vya asili kwa kuviona kuwa ni vya kizamani, huku akisisitiza umuhimu wa kurejea kwenye vyakula vya 

“Utandawazi umeathiri kizazi cha sasa. Vijana wanaiga tamaduni za kigeni wakiona za kwetu ni za kishamba, lakini hata huko wanakoiga wana tamaduni na mila ambazo wanazitunza,” alisema Kilulu.

Mwisho.

Kitawaka EPL Wikiendi Hii, Macho Yatakuwa Liverpool, United, Arsenal

Ligi Kuu ya England, Premier League, inaendelea wikiendi hii kwa michezo mbalimbali huku timu kubwa zikitarajiwa kushuka dimbani kuwania pointi muhimu katika mbio za mapema za msimu wa 2026/27.

Miongoni mwa michezo inayosubiriwa kwa hamu ni Liverpool dhidi ya Nottingham Forest, huku Liverpool ikilenga kuendeleza kasi nzuri na kuhakikisha inapata matokeo yatakayoipa nafasi nzuri katika msimamo wa ligi.

Nayo Tottenham Hotspur itakuwa mwenyeji wa Newcastle United katika mchezo mwingine unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa. Timu hizo zinahitaji pointi tatu ili kujiweka katika nafasi nzuri katika msimamo wa ligi.

Macho pia yataelekezwa kwenye mchezo wa Brighton dhidi ya Chelsea, ambapo Chelsea itakuwa ikitafuta ushindi muhimu dhidi ya Brighton. Mchezo huo unatarajiwa kuwa na mvuto kutokana na ushindani wa timu hizo katika soka la England.

Katika mchezo mwingine mkubwa, Aston Villa itakutana na Arsenal, huku Arsenal ikitarajiwa kuwa na kazi ya kuhakikisha inapata matokeo mazuri katika uwanja wa Villa.

Kwa upande wa Manchester United, timu hiyo itakuwa ugenini dhidi ya Ipswich Town katika mchezo utakaokuwa muhimu kwa kikosi hicho, hasa baada ya kuanza msimu kwa matokeo yasiyoridhisha.

Wakati huo huo, michezo mingine ya wikiendi itawakutanisha Bournemouth na Everton, Sunderland na Fulham, pamoja na Leeds United dhidi ya Brentford.

Kwa ujumla, wikiendi hii inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku kila timu ikisaka pointi tatu katika hatua za mwanzo za msimu wa Premier League.

Mechi za EPL wikiendi hii — 29–31 Agosti 2026

Ijumaa, Agosti 28

  • Crystal Palace vs Manchester City — saa 4:00 usiku (Tanzania)

Jumamosi, Agosti 29

  • Liverpool vs Nottingham Forest — saa 2:30 jioni
  • Bournemouth vs Everton — saa 5:00 jioni
  • Coventry City vs Hull City — saa 5:00 jioni
  • Tottenham Hotspur vs Newcastle United — saa 7:30 usiku

Jumapili, Agosti 30

  • Sunderland vs Fulham
  • Brighton vs Chelsea
  • Leeds United vs Brentford
  • Aston Villa vs Arsenal

Jumatatu, Agosti 31

  • Ipswich Town vs Manchester United

Ratiba hii ni ya wikiendi ya pili ya Premier League 2026/27.

Wiki hii ndani ya DStv ni special sana! Usikose kutazama episode mpya ya kipindi cha A List, mechi za kukatana na shoka za ligi ya England, bila kusahau Jumapili kuanzia saa 4:00 tunaanza kuitazama series mpya ya Spinners ikiwa na lugha ya Kiswahili.

Aunty Ezekiel Afichua Siri Za Mastaa, “Zamani Tulitoka Na Wanaume Wakubwa”

Global Publishers
August 28, 2026
18 views
0 Comments

Msanii wa Bongo Movie, Aunty Ezekiel, amefunguka kuhusu maisha ya mahusiano ya mastaa wenzake, akieleza namna baadhi yao walivyokuwa wakitoka na wanaume waliowazidi umri kipindi cha nyuma, tofauti na ilivyo sasa.

Aunty Ezekiel amesema zamani mastaa hao walikuwa wakiingia kwenye mahusiano kwa misingi ya mapenzi, huku wakitoka na wanaume waliowazidi umri, lakini kwa sasa mambo yamebadilika na baadhi yao wameanza kutoka na vijana wadogo.

Kauli hiyo ameitoa huku akiwapa stori mastaa wenzake, Wema Sepetu (Wolper), Kajala Masanja na Irene Uwoya, akizungumzia mwenendo wa mahusiano yao na namna ulivyobadilika kwa miaka ya hivi karibuni.

Aunty Ezekiel ameeleza kuwa kipindi cha nyuma ilikuwa jambo la kawaida kwa mastaa hao kuwa katika mahusiano na wanaume wenye umri mkubwa kuliko wao, lakini sasa baadhi yao wamekuwa wakihusishwa na vijana wenye umri mdogo.

Kauli hiyo imezua gumzo kwenye mitandao ya kijamii, huku mashabiki wakisubiri kuona namna mastaa hao watakavyoitikia kauli hiyo ya Aunty Ezekiel.

Weekend hii ndani ya DStv ni special sana! Usikose kutazama episode mpya ya kipindi cha A List, mechi za kukatana na shoka za ligi ya England, bila kusahau Jumapili kuanzia saa 4:00 tunaanza kuitazama series mpya ya Spinners ikiwa na lugha ya Kiswahili.

Lipia mapema kifurushi chako kwa kupiga *150*53# ili usipitwe na burudani hii ya kukatana na shoka.