Aunty Ezekiel Afichua Siri Za Mastaa, “Zamani Tulitoka Na Wanaume Wakubwa”
Global Publishers
August 28, 2026
18 views
0 Comments

Msanii wa Bongo Movie, Aunty Ezekiel, amefunguka kuhusu maisha ya mahusiano ya mastaa wenzake, akieleza namna baadhi yao walivyokuwa wakitoka na wanaume waliowazidi umri kipindi cha nyuma, tofauti na ilivyo sasa.
Aunty Ezekiel amesema zamani mastaa hao walikuwa wakiingia kwenye mahusiano kwa misingi ya mapenzi, huku wakitoka na wanaume waliowazidi umri, lakini kwa sasa mambo yamebadilika na baadhi yao wameanza kutoka na vijana wadogo.

Kauli hiyo ameitoa huku akiwapa stori mastaa wenzake, Wema Sepetu (Wolper), Kajala Masanja na Irene Uwoya, akizungumzia mwenendo wa mahusiano yao na namna ulivyobadilika kwa miaka ya hivi karibuni.
Aunty Ezekiel ameeleza kuwa kipindi cha nyuma ilikuwa jambo la kawaida kwa mastaa hao kuwa katika mahusiano na wanaume wenye umri mkubwa kuliko wao, lakini sasa baadhi yao wamekuwa wakihusishwa na vijana wenye umri mdogo.

Kauli hiyo imezua gumzo kwenye mitandao ya kijamii, huku mashabiki wakisubiri kuona namna mastaa hao watakavyoitikia kauli hiyo ya Aunty Ezekiel.
Weekend hii ndani ya DStv ni special sana! Usikose kutazama episode mpya ya kipindi cha A List, mechi za kukatana na shoka za ligi ya England, bila kusahau Jumapili kuanzia saa 4:00 tunaanza kuitazama series mpya ya Spinners ikiwa na lugha ya Kiswahili.
Lipia mapema kifurushi chako kwa kupiga *150*53# ili usipitwe na burudani hii ya kukatana na shoka.
