Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

JAMII YAHIMIZWA KUTUMIA VYAKULA VYA MIMEA ASILI KUIMARISHA KINGA ZA MWILI

By admin
August 28, 2026 2 Min Read
Comments Off on JAMII YAHIMIZWA KUTUMIA VYAKULA VYA MIMEA ASILI KUIMARISHA KINGA ZA MWILI

 

Na Lilian Kasenene, Morogoro

Matukio Daima Media

JAMII imehimizwa kutumia vyakula vitokanavyo na mimea, mbegu na matunda ya asili ili kuimarisha kinga za mwili na kujikinga na magonjwa sugu.

Mkurugenzi wa HOPECA Products na Amra Gogondi, Dk Manimba Daniel, alisema vyakula vinavyotokana na mimea na mbegu za asili vina vitamini na virutubisho muhimu vinavyosaidia kutunza na kurekebisha mwili.

Alisema jamii inapaswa kubadilisha mtindo wa maisha kwa kutumia vyakula vya asili, kufanya mazoezi mepesi na endelevu kwa ajili ya kuchangamsha mwili, pamoja na kuhakikisha inapata muda wa kutosha wa kupumzika.

Dk Daniel alisema unga wa HOPECA ni tiba lishe unaotokana na mchanganyiko wa aina 20 za mbegu za mimea pamoja na matunda mbalimbali ya asili, hivyo kuwa na virutubisho mbalimbali muhimu mwilini.

“HOPECA ni mchanganyiko wa vitamini C, nyuzinyuzi na madini ambayo yanasaidia kuimarisha kinga ya mwili, kuboresha homoni na kusaidia kuondoa uchafu mwilini,” alisema Mkurugenzi huyo.

Akizungumza kwenye Tamasha la Utamaduni wa Tanzania lilnalo3nd3lea mkoani Morogoro, Dk Daniel alisema pia unga wa tunda la Amra Gogondi, ambalo ni tundapori, unasaidia kusafisha damu na kuondoa mafuta yasiyofaa mwilini.

“Chai ya Amra inachangamsha mwili, inayeyusha mafuta kwenye damu, inapunguza cholesterol na kusaidia kuondoa uchafu kwenye utumbo unaotokana na mabaki ya vyakula,” alisema Dk Daniel.

Alisema unga wa Amra pia unasaidia kukarabati mwili kwa kuchochea uzalishaji wa chembe hai mpya zinazosaidia mwili kupambana na maradhi.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Doumbia Bado Anajitafuta! Ashindwa Kutamba Dhidi ya Coastal

Next

BONANZA LA BUNGE KULENGA AFYA NA MSHIKAMANO WA WATUMISHI

Recent Posts

  • Thunder Riches: Fortune Eagle, Mchezo Mpya Watingisha Meridianbet
  • BONANZA LA BUNGE KULENGA AFYA NA MSHIKAMANO WA WATUMISHI
  • JAMII YAHIMIZWA KUTUMIA VYAKULA VYA MIMEA ASILI KUIMARISHA KINGA ZA MWILI
  • Doumbia Bado Anajitafuta! Ashindwa Kutamba Dhidi ya Coastal
  • WANANCHI URU KUSINI WACHANGIA ZAIDI YA MILIONI 200 KUKARABATI SHULE

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme