Video: Ndejembi Awasalimu Wananchi Moshi, Atoa Ahadi Kwa Rais Samia

Global Publishers
September 1, 2026
1,020 views
0 Comments


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, amewasalimu wananchi wa Mbuyuni wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro, waliokusanyika kumpokea alipokuwa katika ziara binafsi mkoani humo leo, Septemba 1, 2026.

Akizungumza na wananchi hao, Makamu wa Rais amewasihi kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na yeye binafsi, ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mhe. Ndejembi amesema kupitia nguvu ya maombi ataweza kumsaidia Rais Samia kwa hekima na utii katika kutekeleza majukumu ya kuwatumikia wananchi.

Aidha, amesema ataendelea kutekeleza wajibu wake kwa uadilifu, umakini na kujituma, huku akisisitiza utayari wake wa kushirikiana na viongozi pamoja na wananchi katika kutekeleza majukumu ya kitaifa.

Akizungumza kwa msisitizo, Makamu wa Rais amesema:

“Hatawazingua Wana wala hatamzingua Mama,”

kauli ambayo alisema aliitoa pia mkoani Dodoma kwa wananchi wa Chamwino mara baada ya kuapishwa.

Kabla ya kuelekea Mbuyuni, Makamu wa Rais aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ambako alipokelewa na viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kilimanjaro.

 

Vodacom Yaja na Ubunifu Mpya Kuelekea Tanzania 2050

Katika toleo la 12 la Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026, Vodacom Tanzania imezidi kuonyesha jinsi mtandao, ubunifu na ujasiriamali vinavyochangia malengo ya Dira ya Maendeleo Tanzania 2050.

Tukio hili linakutanisha wabunifu wajasiriamali, watunga sera, watafiti, wawekezaji, vijana, wadau wa maendeleo na viongozi wa sekta binafsi chini ya kauli mbiu: “Kutoka Matarajio hadi Mageuzi: Kuibua Njia ya Tanzania Kuelekea Ustawi Jumuishi.”

Katika wiki hii, Vodacom imeshiriki katika mijadala mbalimbali kuhusu uchumi wa wabunifu wa maudhui, banda la maonyesho, mijadala na wanahabari na wadau, uzinduzi wa Vodacom Accelerator Season 5, pamoja na onyesho la moja kwa moja la usalama wa mtandao (cybersecurity) litakalofuatiwa na jopo la majadiliano.

Akizungumza katika majadiliano ya kuziunganisha Sauti za Watanzania: Watengeneza maudhui na Majukwaa Mtandaoni. Mkuu wa Idara ya Chapa na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Yvonne Maruma, alisema thamani ya mtandao inapaswa kupimwa kwa kile unachowawezesha watu kufanya.

“Mtandao ni hatua ya kwanza ya kushiriki katika uchumi wa kidijitali. Lakini thamani yake halisi iko katika kile unachowawezesha watu kufanya: kujifunza, kubuni, kujenga biashara, kufikia hadhira na kusikika,” alisema Maruma.

“Kwa kijana wa Kitanzania, simu janja inaweza kuwa darasa, soko, studio ya ubunifu na chombo cha biashara. Wakati Tanzania ikitekeleza Dira 2050, wabunifu wa maudhui wanapaswa kuonekana zaidi ya njia za kusambaza ujumbe; wao ni washirika wanaoweza kugeuza mawazo ya ujasiriamali, elimu, ujumuishaji wa kifedha na ubunifu kuwa hadithi ambazo watu wanaelewa, wanaziamini na kuzifanyia kazi. Hilo ndilo tunalomaanisha tunaposema Vodacom ni Zaidi ya Mtandao.”

Kupitia mpango wa Vodacom Youth Base (VYB), kampuni inaendelea kushirikiana na watengeneza maudhui mtandaoni na kuwasaidia kubaki mtandaoni wakati wakitengeneza na kusambaza maudhui kwa hadhira zao.

Mpango huu ni sehemu ya jitihada pana za Vodacom za kuhakikisha ujumuishaji wa kidijitali wenye maana, unaowawezesha watu si tu kuunganishwa mtandaoni, bali pia kushiriki, kushindana na kuongoza katika uchumi wa kidijitali.

Katika kilele cha wiki hii, Vodacom Tanzania itazindua programu ya Vodacom accelerator season 5, ambayo imelenga kuwasaidia wajasariamali wa Kitanzania kuanzia hatua zao za mwanzo za wazo hadi kuwa biashara imara. Uzinduzi huu utaambatana na hadithi ya mmoja wa wahitimu wa awali wa mpango huu aliyefanikiwa kutoka wazo hadi biashara.

Ushiriki wa Vodacom katika Wiki ya Ubunifu Tanzania unajengwa juu ya ushirikiano wake na UNDP Tanzania na unaunga mkono malengo ya Dira ya Maendeleo Tanzania 2050: uchumi wa viwanda wenye ushindani wa dola trilioni 1 za Marekani, unaoendeshwa na mtandao jumuishi wa usafirishaji, nishati, sayansi na teknolojia, utafiti na maendeleo, pamoja na mageuzi ya kidijitali.

Kesi ya Lissu Yaahirishwa, Mnyika Kuendelea Kudodoswa Kesho

Kesi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, imeahirishwa hadi kesho, huku Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika, akitarajiwa kuendelea kujibu maswali kutoka upande wa Serikali.

Katika hatua za mwisho za mwenendo wa kesi leo, Mnyika alikabiliwa na maswali kuhusu uelewa wake wa sheria, majukumu yake kama Katibu Mkuu wa CHADEMA, pamoja na kauli na msimamo wa chama kuhusu uchaguzi na vurugu.

Wakili wa Serikali, Nzengeli, alimuuliza Mnyika kama yeye ni mtaalamu wa sheria, ambapo alijibu kuwa si mtaalamu wa sheria.

Mnyika pia alikataa kuwa hana uwezo wowote wa kuchambua nyaraka, akisema anaweza kuchambua mambo kwa uelewa wake, ingawa baadaye alikiri kuwa hana utaalamu wa kisheria.

MNYIKA AULIZWA KUHUSU DEMOKRASIA

Katika dodoso hilo, Mnyika alieleza kuwa endapo mtu anaamini uchaguzi ni wa haki na uhuru, lakini CHADEMA ina msimamo tofauti, mtu huyo anaweza kutokubaliana na msimamo wa chama.

Alisema kutokubaliana na msimamo wa CHADEMA ni suala la maoni ya mtu binafsi.

Wakili Job Mrema naye aliendelea kumuuliza Mnyika maswali akitumia Kamusi Kuu ya Kiswahili, Toleo la Tatu la mwaka 2022, katika kutafuta maana ya baadhi ya maneno yaliyotumika kwenye ushahidi.

Mnyika alithibitisha kuwa kamusi hiyo ni rasmi, ingawa si nakala pekee inayoweza kutumika kutoa tafsiri ya Kiswahili.

Mrema alimuuliza Mnyika kuhusu majukumu yake kama Katibu Mkuu wa CHADEMA.

Mnyika alisema jukumu lake ni kusimamia shughuli zote za kila siku za chama.

Alipoulizwa kama ameshindwa kutaja majukumu yake katika baadhi ya maswali yaliyoulizwa awali, Mnyika alikanusha na kusema amejibu maswali mengi, isipokuwa machache ambayo yalihitaji uelewa zaidi.

Mnyika pia alikanusha madai kwamba nafasi yake ya Katibu Mkuu imekuwa ya kusaidiwa au kwamba amekuwa akibebwa na Mwenyekiti wa CHADEMA.

MNYIKA AULIZWA KUHUSU “FUJO”

Katika sehemu nyingine ya dodoso, Mrema alimuuliza Mnyika maana ya neno “fujo.”

Mnyika awali alijibu kwa kusema, “Fujo ni fujo,” lakini baada ya kuombwa kueleza maana hiyo kwa mujibu wa kamusi aliyokuwa nayo, alisema fujo ni hali ya kutokuwepo kwa utaratibu mzuri au mpango, pamoja na hali ya ghasia na machafuko.

Wakili Mrema alimuuliza Mnyika kama kauli iliyotolewa na Lissu Aprili 3, 2025 kwamba “ataleta fujo” na “atakinukisha” ilikuwa ni fujo yenyewe.

Kutokana na muda, upande wa Serikali uliomba suala hilo liendelee kesho, na Jaji akaelekeza kuwa swali hilo litashikiliwa kwa ajili ya kuendelea na ushahidi.

“SIFAHAMU MIPANGO YA CHADEMA KUHUSU VURUGU”

Katika dodoso jingine, Wakili Katuga alimuuliza Mnyika kuhusu madai ya kuwepo kwa mipango ya vurugu kabla na wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Mnyika alisema hafahamu mipango hiyo.

Alipoulizwa kuhusu madai kwamba baadhi ya wanachama waliwahi kuzungumza na waandishi wa habari na kueleza kuwa kulikuwa na mipango iliyopangwa na kuratibiwa na chama, Mnyika alisema hafahamu.

Pia alisema hafahamu madai ya kuwepo kwa mifumo maalumu ya mawasiliano ambayo ingetumika iwapo mitandao ya simu ingezimwa.

MNYIKA AULIZWA KUHUSU VURUGU ZA UCHAGUZI

Katuga alimuuliza Mnyika kama anafahamu kuwa vurugu za siku ya uchaguzi zilidaiwa kuwa zilipangwa na kuratibiwa.

Mnyika alisema alisikia kuhusu madai hayo.

Alipoulizwa kuhusu watu waliokamatwa kuhusiana na vurugu hizo, Mnyika alisema anafahamu kuwa baadhi yao walikamatwa na baadaye wakaachiwa.

Hata hivyo, alipohojiwa kuhusu madai kwamba watuhumiwa walifanya fujo kituoni kutokana na kauli za kiongozi wao, Tundu Lissu, Mnyika alisema hafahamu.

LISSU AOMBA MWENENDO WA KESI

Baada ya kesi kuahirishwa, Tundu Lissu aliomba apewe mwenendo wa kesi ili aweze kuusoma akiwa aliko.

Upande wa Serikali unatarajiwa kuendelea na dodoso kwa Mnyika kesho, huku kesi ikiendelea kufuatiliwa kwa karibu kutokana na ushahidi unaohusu kauli za viongozi wa CHADEMA, uchaguzi wa mwaka 2025 na madai yanayohusiana na vurugu.

Trump Atishia Kuijibu Iran Kwa Nguvu Baada Ya Mashambulizi Mapya

Rais wa Marekani, Donald Trump, ametishia kuchukua hatua kali dhidi ya Iran baada ya nchi hizo mbili kubadilishana mashambulizi ya kijeshi kwa mara ya kwanza katika kipindi cha takribani mwezi mmoja.

Mvutano huo umeongezeka baada ya Marekani kushambulia vituo vya kurushia makombora vya Iran katika Kisiwa cha Larak, kilichopo kwenye eneo la kimkakati la Mlango wa Hormuz. Marekani ilisema mashambulizi hayo yalilenga vikosi vya Iran vilivyokuwa vikijiandaa kuweka mabomu ya baharini katika njia hiyo muhimu ya usafirishaji.

Iran ilijibu kwa kurusha makombora kuelekea vituo viwili vya kijeshi vinavyotumiwa na Marekani nchini Jordan. Jordan ilisema mifumo yake ya ulinzi wa anga ilifanikiwa kuyadungua makombora manane, huku hakuna majeruhi walioripotiwa katika vituo hivyo.

Baada ya mashambulizi hayo, Trump alitoa onyo kali dhidi ya Iran, akisema Marekani itajibu kwa nguvu.

Trump pia amesema mashambulizi hayo hayamaanishi kwamba Marekani imerejea kwenye vita kamili na Iran, akidai kuwa uwezo wa kijeshi wa Tehran umeathirika kwa kiasi kikubwa.

Hata hivyo, kauli hizo zimeongeza hofu kwamba mapigano yanaweza kuongezeka tena baada ya kipindi ambacho Marekani ilikuwa ikitumia zaidi shinikizo la kiuchumi na vikwazo dhidi ya Tehran.

Kisiwa cha Larak kiko katika eneo la Mlango wa Hormuz, njia muhimu sana kwa biashara ya mafuta duniani.

Marekani imesema ilichukua hatua dhidi ya vituo vya Iran baada ya kubaini maandalizi ya kurushwa kwa mabomu ya baharini ambayo yangeweza kuhatarisha meli zinazopita katika njia hiyo.

Mvutano kuhusu Mlango wa Hormuz umeendelea kuwa sehemu muhimu ya mzozo huo, huku Iran ikisisitiza kuwa njia hiyo haiwezi kufunguliwa kikamilifu bila masharti yake kutekelezwa.

Licha ya kujibu mashambulizi ya Marekani, Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema Tehran haitafuti vita na kwamba kuendelea kwa mapigano hakutakuwa na manufaa kwa Iran, eneo la Mashariki ya Kati wala dunia kwa ujumla.

Pezeshkian pia amesema Iran iko tayari kurejea kwenye mchakato wa mazungumzo iwapo Marekani itatekeleza ahadi zilizowekwa katika makubaliano ya muda yaliyofikiwa mwezi Juni.

Katika hatua nyingine, Trump alichapisha kwenye mitandao ya kijamii video iliyodai kuonyesha mashambulizi dhidi ya Kisiwa cha Kharg, kituo muhimu cha mafuta cha Iran.

Hata hivyo, taarifa zilizothibitishwa zinaonyesha kuwa video hiyo ilikuwa imetengenezwa kwa kutumia teknolojia ya akili bandia (AI), na hakuna ushahidi kwamba shambulio hilo lilifanyika wakati huo.

Kwa sasa, macho yanaelekezwa kwa hatua itakayochukuliwa na Marekani baada ya Trump kuahidi kulipiza kisasi, huku Iran ikiendelea kusisitiza kuwa iko tayari kujibu iwapo itashambuliwa tena.

Ndejembi Awasalimu Wananchi Moshi, Atoa Ahadi Kwa Rais Samia

Global Publishers
September 1, 2026
450 views
0 Comments

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, amewasalimu wananchi wa Mbuyuni wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro, waliokusanyika kumpokea alipokuwa katika ziara binafsi mkoani humo leo, Septemba 1, 2026.

Akizungumza na wananchi hao, Makamu wa Rais amewasihi kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na yeye binafsi, ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mhe. Ndejembi amesema kupitia nguvu ya maombi ataweza kumsaidia Rais Samia kwa hekima na utii katika kutekeleza majukumu ya kuwatumikia wananchi.

Aidha, amesema ataendelea kutekeleza wajibu wake kwa uadilifu, umakini na kujituma, huku akisisitiza utayari wake wa kushirikiana na viongozi pamoja na wananchi katika kutekeleza majukumu ya kitaifa.

Akizungumza kwa msisitizo, Makamu wa Rais amesema:

“Hatawazingua Wana wala hatamzingua Mama,”

kauli ambayo alisema aliitoa pia mkoani Dodoma kwa wananchi wa Chamwino mara baada ya kuapishwa.

Kabla ya kuelekea Mbuyuni, Makamu wa Rais aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ambako alipokelewa na viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kilimanjaro.

 

Ndejembi Awasalimu Wananchi Moshi, Atoa Ujumbe wa Rais Samia

Global Publishers
September 1, 2026
60 views
0 Comments

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, amewasalimu wananchi wa Mbuyuni wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro, waliokusanyika kumpokea alipokuwa katika ziara binafsi mkoani humo leo, Septemba 1, 2026.

Akizungumza na wananchi hao, Makamu wa Rais amewasihi kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na yeye binafsi, ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mhe. Ndejembi amesema kupitia nguvu ya maombi ataweza kumsaidia Rais Samia kwa hekima na utii katika kutekeleza majukumu ya kuwatumikia wananchi.

Aidha, amesema ataendelea kutekeleza wajibu wake kwa uadilifu, umakini na kujituma, huku akisisitiza utayari wake wa kushirikiana na viongozi pamoja na wananchi katika kutekeleza majukumu ya kitaifa.

Akizungumza kwa msisitizo, Makamu wa Rais amesema:

“Hatawazingua Wana wala hatamzingua Mama,”

kauli ambayo alisema aliitoa pia mkoani Dodoma kwa wananchi wa Chamwino mara baada ya kuapishwa.

Kabla ya kuelekea Mbuyuni, Makamu wa Rais aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ambako alipokelewa na viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kilimanjaro.

 

Ndejembi Awasalimu Wananchi Moshi, Atoa Ujumbe Kwa Rais Samia

Global Publishers
September 1, 2026
0 views
0 Comments

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, amewasalimu wananchi wa Mbuyuni wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro, waliokusanyika kumpokea alipokuwa katika ziara binafsi mkoani humo leo, Septemba 1, 2026.

Akizungumza na wananchi hao, Makamu wa Rais amewasihi kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na yeye binafsi, ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mhe. Ndejembi amesema kupitia nguvu ya maombi ataweza kumsaidia Rais Samia kwa hekima na utii katika kutekeleza majukumu ya kuwatumikia wananchi.

Aidha, amesema ataendelea kutekeleza wajibu wake kwa uadilifu, umakini na kujituma, huku akisisitiza utayari wake wa kushirikiana na viongozi pamoja na wananchi katika kutekeleza majukumu ya kitaifa.

Akizungumza kwa msisitizo, Makamu wa Rais amesema:

“Hatawazingua Wana wala hatamzingua Mama,”

kauli ambayo alisema aliitoa pia mkoani Dodoma kwa wananchi wa Chamwino mara baada ya kuapishwa.

Kabla ya kuelekea Mbuyuni, Makamu wa Rais aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ambako alipokelewa na viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kilimanjaro.

 

MEYA KIGOMA UJIJI AKEMEA MMONYOKO WA MAADILI YA JAMII

Na Fadhili Abdallah,Kigoma

MEYA wa maanispaa ya Kigoma Ujiji Mussa Maulid ametoa wito kwa viongozi wa dini mkoani Kigoma katika malezi ya watoto wao na jamii kwa ujumla ili kukabiliana na wimbi kubwa la mmomonyoko wa maadili linaloukabili mkoa huo ikiwemo kukithiri kwa vitendo vya ushoga.

Meya Maulid alisema hayo wakati wa Maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW) yaliyofanyika kwenye msikiti wa Mujahidina Ujiji Manispaa ya Kigoma Ujiji na kubainisha kuwa mmomonyoko wa maadili unapoteza sifa na taswira ya Ustaarab ya mkoa huo hasa ya mji wa Ujiji.

Alisema kuwa mji wa Ujiji kwa miaka mingi ulikuwa unafahamika kama mji wa ustaarab kutokana na idadi kubwa ya watu wake kuishi kwa kufuata misingi ya dini na kuzingatia maadili mema ya jamii lakini la kushangaza kwa sasa Ujiji ndiyo imekuwa ikiongoza kwa mmomonyoko wa maadili ikiwemo kuandaa karamu za ushoga na kualika watu kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania na nje ya Tanzania kuhudhuria karamu hiyo.

“Ujiji imetoa wanazuoni wakubwa wa dini ya kiislam na Mashekhe na wahubiri wengi wa kiislam wamesoma Ujiji, lakini pia lipo kanisa katoliki lililoanzishwa karne ya 13 hayo yalifanya eneo hilo kuwa na ustaarabu na maadili mema lakini yote yameondokana na Ujiji imekuwa mfano mbaya kwa maisha ya vijana wa sasa,”Alisema Meya huyo wa manispaa ya Kigoma Ujiji.

Kwa upande wake Kadhi wa mkoa Kigoma,Abdul Muhsin Kitumba alisema kuwa ni lazima waumin wa kiislam mkoani Kigoma waishi kwenye maadili kama ambavyo wanasherehekea maisha ya Mtume Muhammad (SAW) ambaayee anaapigiwa mfano kuwa binadamu aliyeishi katika maadili ya haali ya juu.

Kitumba alisema kuwa inashangaza kuona mambo machafu yanafanywa na vijana na kufurahiwa ikiwemo kutukana viongozi huku baadhi ya wanaofanya hivyo wanatoka kwenye familia za viongozi wa dini na kwamba hilo halikubaliki ni lazima jambo hilo likemewe na kuachwa mara moja.

mwisho

Pitso Mosimane Apewa Tena Usukani wa Bafana Bafana

Global Publishers
September 1, 2026
0 views
0 Comments

Shirikisho la Soka la Afrika Kusini (SAFA) limemtangaza Pitso Mosimane kuwa kocha mkuu mpya wa timu ya taifa ya Afrika Kusini, Bafana Bafana.

Uteuzi huo unamrejesha Mosimane kwenye benchi la timu hiyo kwa mara ya pili, baada ya awali kuiongoza Bafana Bafana kati ya mwaka 2010 na 2012.

Mosimane anaingia kwenye nafasi hiyo akiwa miongoni mwa makocha wenye uzoefu mkubwa barani Afrika, kutokana na mafanikio aliyowahi kuyapata katika ngazi ya klabu na timu za taifa.

Kocha huyo sasa atakuwa na jukumu la kujenga kikosi imara cha Bafana Bafana na kuhakikisha timu hiyo inapata matokeo mazuri katika mashindano mbalimbali yajayo.

Katika kipindi chake cha kwanza kuiongoza Afrika Kusini, Mosimane alipata uzoefu muhimu wa kufanya kazi katika mazingira ya timu ya taifa, kabla ya kuendelea na safari yake ya ukocha katika klabu mbalimbali.

Katika majukumu yake mapya, anatarajiwa kufanya kazi kwa karibu na benchi lake la ufundi pamoja na viongozi wa SAFA kuhakikisha timu hiyo inafikia malengo yaliyowekwa.

Miongoni mwa majukumu makubwa yanayomsubiri Mosimane ni kuiandaa Bafana Bafana kwa ajili ya AFCON 2027, michuano ambayo Afrika Kusini inatarajiwa kushiriki.

Mosimane atatakiwa kujenga kikosi chenye ushindani na kuhakikisha timu hiyo inakuwa tayari kwa changamoto za michuano hiyo mikubwa ya soka barani Afrika.

Uteuzi wake unakuja baada ya kuondoka kwa Hugo Broos, ambaye aliiongoza Afrika Kusini katika Kombe la Dunia la FIFA 2026.

Sasa macho ya mashabiki wa Bafana Bafana yataelekezwa kwa Mosimane, ambaye anarudi kwenye benchi la timu hiyo akiwa na jukumu la kuendeleza ushindani na mafanikio ya Afrika Kusini katika soka la kimataifa.

Na Florah Anderson | GPL

MUME AUWAWA KWA KUDAI UNYUMBA MOROGORO

 

Na Lilian Kasenene, Morogoro 

Morogoro.FUNDI cherehani Jovita Bategeuye Budyo (30), mkazi wa Mafisa, anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro kwa tuhuma za kumuua mumewe, Abeli Charles (44), mfanyabiashara na mkazi wa Mafisa, Manispaa ya Morogoro.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, ACP Andrew Kantimbo, tukio hilo lilitokea usiku wa Agosti 31, 2026, katika eneo la Mafisa, Kata ya Mafisa.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa mtuhumiwa na marehemu walikuwa wakiishi pamoja.

Aidha alisema wakati wakiwa wanajiandaa kula, kulitokea mgogoro ambao, kwa mujibu wa taarifa ya polisi, ulihusishwa na madai ya marehemu kunyimwa unyumba.

Mgogoro huo ulizua ugomvi mkubwa na inadaiwa mtuhumiwa alimpiga/kumkata marehemu kwa kitu chenye makali katika maeneo ya shingoni na kichwani, hali iliyosababisha majeraha makubwa na hatimaye kupelekea kifo chake.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limeendelea na uchunguzi wa tukio hilo na linamshikilia mtuhumiwa kwa hatua zaidi za kisheria.

Kamanda Kantimbo ametoa wito kwa wananchi kuepuka kutumia nguvu katika kutatua migogoro ya kifamilia na kijamii, badala yake kutumia njia salama za kumaliza tofauti na changamoto za mahusiano.

Pia amewataka wananchi kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuhakikisha usalama unadumishwa, hasa kwa kuwalinda watoto, wazee, watu wenye ulemavu na makundi mengine yaliyo katika mazingira hatarishi.

Taarifa hiyo imetolewa Septemba 1, 2026, na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro. ACP Kantimbo.

Mwisho