Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Burudani

WAZIRI MKUU: NDEJEMBI ANATOSHA KUMSAIDIA RAIS

By admin
August 28, 2026 2 Min Read
Comments Off on WAZIRI MKUU: NDEJEMBI ANATOSHA KUMSAIDIA RAIS

 

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Mchemba, amewaomba wabunge kuunga mkono na kuthibitisha uteuzi wa Deogratius Ndejembi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akisema ana sifa na uzoefu unaomwezesha kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan katika kutekeleza majukumu ya Serikali.

Dkt. Mwigulu amesema Ndejembi ana sifa zote muhimu za kushika nafasi hiyo, akieleza kuwa majukumu ya Makamu wa Rais yanahitaji mtu mwenye busara, mchapa kazi na anayefahamu mwenendo wa Serikali pamoja na mahitaji ya wananchi.

“Sina shaka kwamba tumepata mtu sahihi wa kumsaidia Rais katika majukumu ya kuendesha Serikali,” amesema Dkt. Mwigulu.

Amesema kwa kuzingatia Ibara ya 47(1) ya Katiba, Makamu wa Rais ndiye Msaidizi Mkuu wa Rais katika mambo yote ya Jamhuri ya Muungano kwa ujumla, huku Ibara ya 47(8) ikieleza kuwa Makamu wa Rais hutekeleza madaraka yake chini ya uongozi na usimamizi wa Rais na kuwajibika kwa mambo anayokabidhiwa.

Dkt. Mwigulu amesema Ndejembi si mgeni katikaChama Cha Mapinduzi

(CCM), huku akieleza kuwa tangu aingie Bungeni mwaka 2020 kama Mbunge wa Chamwino, ameendelea kuaminiwa katika majukumu mbalimbali. 

Amesema katika kipindi ambacho amefanya kazi serikalini, Ndejembi ambaye pia ana elimu nzuri, amepata uzoefu katika sekta mbalimbali zenye majukumu muhimu ya kitaifa, pamoja na uzoefu wa uwakilishi wa wananchi.

“Kwa kuzingatia sifa na uzoefu wake mpana wa mfumo wa Serikali na mahitaji ya wananchi, naamini anatosha kuwa Msaidizi muhimu wa Rais,” amesema Waziri Mkuu. 

Waziri Mkuu ametoa ombi hilo wakati wa mchakato wa Bunge kuthibitisha uteuzi wa Makamu wa Rais mpya kwa mujibu wa Ibara ya 50(4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Ibara hiyo inaweka utaratibu wa Rais kumteua mtu mwingine kuwa Makamu wa Rais pale nafasi hiyo inapokuwa wazi, na uteuzi huo kuthibitishwa na Bunge.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

UEFA Yaandaa Kesi ya Jinai Dhidi ya Infantino, Mashabiki Wamlipua

Next

Mafuriko Yaua Watu 100 Nepal, Zaidi ya 1500 Hawajulikani Walipo

Recent Posts

  • Rais Samia Atuma Rambirambi Kifo cha Mfalme wa Norway
  • KINGU: NDEJEMBI NI KIJANA MZALENDO, MCHAPAKAZI
  • Msukuma Asimulia Ndejembi Alivyopokea Taarifa za Uteuzi wa Makamu wa Rais – Video
  • Jamhuri Yakamilisha Kumuhoji Lissu Katika Kesi ya Uhaini Leo – Video
  • Mafuriko Yaua Watu 100 Nepal, Zaidi ya 1500 Hawajulikani Walipo

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme