Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Mafuriko Yaua Watu 100 Nepal, Zaidi ya 1500 Hawajulikani Walipo

By admin
August 28, 2026 2 Min Read
Comments Off on Mafuriko Yaua Watu 100 Nepal, Zaidi ya 1500 Hawajulikani Walipo

Shechambo Chris
August 28, 2026
12 views
0 Comments

 

Idadi ya watu waliopoteza maisha kutokana na mafuriko makubwa yaliotokea nchini Nepal imefikia 165, huku wengine 1,300 bado hawajulikani walipo,  mafuriko hayo yamesababisha uharibifu mkubwa katika maeneo ya mpakani mwa Nepal na China.

Mafuriko hayo yalitokea Jumatano, Agosti 26, yakisababisha vifo, uharibifu wa miundombinu na kutoweka kwa mamia ya watu katika maeneo yaliyoathirika. Vifo vingine vitatu pia vimeripotiwa upande wa Tibet, China.

Janga hilo lilisababishwa na kuporomoka kwa barafu kubwa kutoka kwenye milima ya Himalaya, na kusababisha maji mengi, vipande vya barafu, mawe na matope kusukumwa kwa nguvu kuelekea kwenye mfumo wa mito na kuvamia maeneo ya makazi.

Utafiti wa Jiolojia wa Marekani (USGS) umeeleza kuwa ishara ya awali ya mtikisiko iliyodhaniwa kuwa ni tetemeko la ardhi haikusababishwa na tetemeko, bali ilitokana na kuporomoka kwa barafu pamoja na mabaki ya miamba na udongo.

Mafuriko hayo yamesababisha uharibifu mkubwa wa nyumba, barabara na madaraja, huku baadhi ya maeneo yaliyoathirika yakibaki kuwa magumu kufikika kutokana na miundombinu kuharibiwa.

 

Timu za uokoaji zimeendelea na operesheni za kuwatafuta manusura na watu waliopotea kwa kutumia helikopta, ndege zisizo na rubani (drones), mbwa maalumu wa utafutaji na vifaa vingine vya dharura.

Mamlaka zimeripoti kuwa  madaraja 19 na takribani kilomita 40 za barabara zimesombwa na maji nchini Nepal, hali inayozidi kufanya shughuli za uokoaji kuwa ngumu.

Waokoaji wanaendelea na juhudi za utafutaji katika maeneo mbalimbali, huku mamlaka zikionya kuwa idadi ya waliofariki inaweza kuongezeka kutokana na uwepo wa watu wengi ambao bado hawajulikani walipo.



Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

WAZIRI MKUU: NDEJEMBI ANATOSHA KUMSAIDIA RAIS

Next

Jamhuri Yakamilisha Kumuhoji Lissu Katika Kesi ya Uhaini Leo – Video

Recent Posts

  • KINGU: NDEJEMBI NI KIJANA MZALENDO, MCHAPAKAZI
  • Msukuma Asimulia Ndejembi Alivyopokea Taarifa za Uteuzi wa Makamu wa Rais – Video
  • Jamhuri Yakamilisha Kumuhoji Lissu Katika Kesi ya Uhaini Leo – Video
  • Mafuriko Yaua Watu 100 Nepal, Zaidi ya 1500 Hawajulikani Walipo
  • WAZIRI MKUU: NDEJEMBI ANATOSHA KUMSAIDIA RAIS

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme