Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

KINGU: NDEJEMBI NI KIJANA MZALENDO, MCHAPAKAZI

By admin
August 28, 2026 1 Min Read
Comments Off on KINGU: NDEJEMBI NI KIJANA MZALENDO, MCHAPAKAZI

 

Mbunge wa Ikungi Magharibi, Elibariki Kingu amemmwagia sifa Makamu wa Rais mteule, Deogratius Ndejembi akisema ni kijana mchapakazi, mwenye uzalendo ndani yake na anayeling’arisha Taifa.

Kingu ameyasema hayo leo Agosti 28, 2026 jijini Dodoma wakati akichangia hoja ya kumthibitisha ndejembi kwenye nafasi ya Makamu wa Rais, iliyotolewa na Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba.

Amesema Taifa limepata kijana mwenye kaliba ya unyeyekevu na kujishusha kwa kila mtu na nidhamu katika kazi anazofanya kila siku.

“Ndejembi ni kijana mchapakazi mwenye commitment ya uzalendo ndani yake. Wakati dunia inapita kwenye misukosuko ya kupanda kwa bei ya mafuta, ni kijana huyu Ndejembi aliisimamia Serikali kuhakikisha shirika letu la TPDC (Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania) linapata uhakika wa kupata mafuta kwa kipindi chote ambacho dunia inapita katika misukosuko.

“Ni kwa uzalendo huo wa kijana huyu, ameweza kuling’arisha taifa katika medani za kimataifa. Leo anapokuwa nje ya nchi tunaona uwakilishi wake na utulivu wake namna anavyoliwakilisha taifa letu,” amesema Kingu.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Msukuma Asimulia Ndejembi Alivyopokea Taarifa za Uteuzi wa Makamu wa Rais – Video

Next

Rais Samia Atuma Rambirambi Kifo cha Mfalme wa Norway

Recent Posts

  • Mikakati yasukwa kuvutia wawekezaji wakubwa Ulaya – HabariLeo
  • Majirani jengeni utamaduni wa kutambuana – HabariLeo
  • Bahasha yenye jina la Makamu wa Rais Mteule yatua bungeni – HabariLeo
  • MADIWANI CHUNYA WAONYWA KUTIMIZA WAJIBU WAO.
  • Jina la Makamu wa Rais Mteule lilivyowasilishwa bungeni – HabariLeo

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme