Bahasha yenye jina la Makamu wa Rais Mteule yatua bungeni – HabariLeo
DODOMA; Spika wa Bunge, Mussa Azzan Zungu, leo Agosti 28 , 2026 amepokea rasmi jina la Makamu wa Rais Mteule, Deogratius John Ndejembi, lililopendekezwa na Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Jina hilo limewasilishwa kwa Spika na Katibu wa Rais Balozi Ali Jabir Mwadini akiwa ameambatana na Mpambe wa Rais (ADC) Brigedia Jenerali, Nyamburi Mashauri kwa ajili ya kuthibitishwa na Bunge.
Mapokezi ya Jina hilo yameshuhudiwa na Naibu Spika, Daniel Sillo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari, pamoja na Katibu wa Bunge , Baraka Leonard.Wengine ni Wenyeviti wa Bunge, Deogratius Mwanyika, Najma Giga na Cecilia Pareso.
