Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Rais Samia Atuma Rambirambi Kifo cha Mfalme wa Norway

By admin
August 28, 2026 1 Min Read
Comments Off on Rais Samia Atuma Rambirambi Kifo cha Mfalme wa Norway

Shechambo Chris
August 28, 2026
6 views
0 Comments

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za rambirambi kwa wananchi na Serikali ya Norway kufuatia kifo cha aliyekuwa Mfalme wa taifa hilo, Harald V, aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 89.

Kupitia ujumbe wake rasmi, Rais Samia ameeleza kusikitishwa kwake na taarifa hizo huku akiihakikishia familia ya kifalme na wananchi wa Norway kuwa Tanzania ipo pamoja nao katika kipindi hiki cha simanzi kuu.

“Nimesikitishwa sana na taarifa za kifo cha Mheshimiwa Mfalme Harald V wa Norway. Kwa niaba ya Serikali na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninatuma rambirambi zetu za dhati kabisa kwa Mheshimiwa Mfalme Haakon VIII, Familia ya Kifalme, na wananchi wa Ufalme wa Norway,” alisema Rais Samia.

Mfalme Harald V, aliyekuwa mfalme wa umri mkubwa zaidi barani Ulaya, amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Oslo (Rikshospitalet). Kufuatia msiba huo, Mwana wa Mfalme, Prince Haakon, anatarajiwa kuchukua mikoba ya uongozi kama Mfalme mpya wa taifa hilo.

Ikumbukwe kuwa Tanzania na Norway zimekuwa na ushirikiano wa muda mrefu wa kidiplomasia na kiuchumi, na ujumbe wa Rais Samia unadhihirisha mshikamano thabiti kati ya mataifa haya mawili.

 

Na Hasina Thabit

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

KINGU: NDEJEMBI NI KIJANA MZALENDO, MCHAPAKAZI

Next

Hatua ya Mwisho kwa Ndejembi Bungeni, Waziri Ammwagia Sifa (Picha +Video)

Recent Posts

  • Mwang’oda aagiza usimamizi miradi ya CSR – HabariLeo
  • Kagera yapokea vifaa kilimo cha umwagiliaji – HabariLeo
  • Mikakati yasukwa kuvutia wawekezaji wakubwa Ulaya – HabariLeo
  • Majirani jengeni utamaduni wa kutambuana – HabariLeo
  • Bahasha yenye jina la Makamu wa Rais Mteule yatua bungeni – HabariLeo

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme