Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

CCM WAAGIZA KUFANYIKA UKARABATI WA SAKAFU BWENI LA ANNE MAKINDA SEKONDARI NJOMBE

By admin
August 19, 2026 2 Min Read
Comments Off on CCM WAAGIZA KUFANYIKA UKARABATI WA SAKAFU BWENI LA ANNE MAKINDA SEKONDARI NJOMBE

NA MWANDISHI WETU.

NJOMBE.Wakati serikali kupitia mfuko wa maendeleo Tassaf ikitekeleza mradi wa bweni la Shule ya  wasichana Anne Makinda Kata ya Ihanga kwa takribani shilingi milioni 160,Chama Cha mapinduzi  CCM mkoa wa Njombe kimeelekeza kufanyika kwa marekebisho ya sakafu na maji ili kuiweka sawa shule hiyo.

‎Katika ukaguzi wa utekelezaji wa Ilani ya CCM chini ya Kamati ya siasa mkoa ikiongozwa na katibu wa CCM mkoa Julius Peter Imeelekeza kufanyika kwa marekebisho ya baadhi ya miundombinu hususani maji ndani ya bweni Hilo ili kuwanusuru wanafunzi na magonjwa ya mlipuko.

Aidha Amemtaka mkuu wa wilaya ya Njombe kuhakikisha bweni hilo linafanyiwa marekebisho ya sakafu ambayo imeanza kufumuka miezi minne tangu kukamilika kwa ujenzi na kuanza kulitumia kwani inapaswa kuendana na hadhi ya jengo.

‎‎Awali mkuu wa wilaya ya Njombe Juma Sweda Amesema kutokana na changamoto ya mlundikano wa wanafunzi kwenye mabweni Serikali  iliamua kupeleka fedha ili kujenga bweni Hilo huku taarifa ya shule hiyo iliyosomwa na Shadrack Kiyeyeu  Makamu mkuu wa shule hiyo imeeleza kuwa Tasaf wametoa milioni 130 huku Halmashauri ikitoa takribani shilingi milioni 30 katika ujenzi wa bweni Hilo.

Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi wa Anne Makinda Sekondari akiwemo Elvina Mhando Wamekiri kuwa Bweni Hilo limepunguza changamoto ya mlundikano huku wakiomba kutatuliwa kwa changamoto ya Maji.

Sanjari na bweni Hilo lakini pia kamati hiyo imetembelea na kukagua mabweni katika shule ya sekondari Kifanya ambayo yamekamilika na yameanza kutumika.

 

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Sababu, suluhu kupanda kwa bei ya saruji

Next

JWTZ kutoa matibabu bure | Mwananchi

Recent Posts

  • Polisi Maswa yatoa msaada kwa wagonjwa
  • Pande mbili utekelezaji agizo la Chalamila kuhusu malori
  • Saratani ya mlango wa kizazi yaongoza kwa vifo Tanzania
  • Makandarasi, kampuni za ujenzi walalamikia faini TRA
  • Waziri wa zamani wa Ukraine ataka uchaguzi vitani

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme