RAIS SAMIA ARIDHIA OMBI LA DKT. NCHIMBI KUJIUZULU

NA MATUKIO DAIMA MEDIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepokea rasmi barua ya ombi la kujiuzulu kwa Makamu wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, na kuridhia ombi hilo.

Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa leo, Agosti 25, 2026, na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Nchimbi ameomba kujiuzulu katika nafasi hiyo kuanzia Septemba 4, 2026.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Rais Samia ameridhia ombi hilo na kwamba taratibu za kikatiba za kumpata Makamu wa Rais mwingine zitachukuliwa.

Taarifa hiyo imesainiwa na Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka, Katibu Mkuu Kiongozi.

Ikulu Yathibitisha Dkt. Nchimbi kujiuzulu Umakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Global Publishers
August 25, 2026
0 views
0 Comments

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepokea na kuridhia ombi la kujiuzulu kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, kuanzia tarehe 4 Septemba 2026.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi leo, Agosti 25, 2026, Rais Samia amekubali ombi hilo la Nchimbi la kujiuzulu nafasi hiyo.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa taratibu za kikatiba za kumpata Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwingine zitachukuliwa.

Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka, tarehe 25 Agosti 2026.

Dk Kiruswa achangia Sh milioni 6 ujenzi darasa la awali – HabariLeo

ARUSHA: Juhudi za wananchi wa Kitongoji cha Lailupa, Kijiji cha Meirugoi, Kata ya Gelai-Meirugoi wilayani Longido mkoani Arusha, za kujitolea kujenga darasa la shule ya awali (chekechea) lenye thamani ya Sh milioni 12, zimemgusa Mbunge wa Jimbo hilo, Dk Steven Kiruswa, ambaye ameamua kugharamia hatua ya mwisho ya ukamilishaji wa jengo hilo kwa Sh milioni 6 kutoka kwenye fedha zake binafsi.

Wananchi hao walimweleza Mbunge huyo ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini, wakati akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika kata hiyo, ambapo walimsimamisha na kumueleza changamoto ya watoto wao kusoma chini ya mti bila kujali mvua au jua.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Lailupa, Ndung’anak Mepukor, alisema jitihada za akina mama, vijana pamoja na viongozi wa mila maarufu kama Laigwanani, ziliwezesha kumshawishi Mbunge huyo kufika eneo hilo na kujionea hali halisi ya mazingira ambayo watoto walikuwa wakipata elimu.

Alisema baada ya kufika eneo hilo, Kiruswa aliona wananchi walikuwa wamefanya sehemu kubwa ya kazi, lakini ujenzi ulikuwa haujakamilika kutokana na kukosekana kwa mlango mmoja, madirisha sita, mabati 60, madawati 20, mbao pamoja na hatua za upigaji plasta.

“Wananchi tulijitahidi kwa nguvu zetu wenyewe, kila kaya ilitoa mchango wa fedha, wengine waliuza mifugo na wengine walishiriki katika uchimbaji wa msingi, ujenzi na kubeba matofali ili watoto wetu wapate sehemu salama ya kusomea,” alisema Mepukor.

Alisema baada ya kuona jitihada hizo na changamoto ya watoto kusoma chini ya mti, Mbunge Kiruswa aliamua kubeba gharama za kukamilisha ujenzi huo kwa Sh milioni 6.

Akizungumza baada ya kutoa ahadi hiyo, Kiruswa aliwapongeza wananchi wa Lailupa kwa moyo wa kujitolea na kusema hatua hiyo imempa faraja kubwa kwa kuona jamii ikishiriki katika kuboresha elimu.

Alisema ameamua kuchangia kukamilika kwa darasa hilo ili kuwawezesha watoto kusoma karibu na makazi yao na kuondokana na adha ya kutembea umbali mrefu kufuata elimu.

Kiruswa alisema suala la kuhakikisha watoto wanapata elimu bora ni jukumu la kila mwananchi, huku akieleza kuwa juhudi za wananchi zinapaswa kuungwa mkono na serikali pamoja na viongozi wao.

Aidha, alisema atahakikisha shule hiyo ya awali inasajiliwa na kupata mwalimu mwenye sifa, kwani kwa sasa inategemea mwalimu wa kujitolea ambaye hana sifa rasmi za ualimu.

“Lengo langu ni kuhakikisha ifikapo Januari mwakani shule hii inakuwa imesajiliwa, inatambulika na serikali na watoto wanafundishwa na mwalimu mwenye sifa,” alisema.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Gelai-Meirugoi, Daniel Nasinda, alisema watoto wa Kitongoji cha Lailupa walikuwa wakitembea zaidi ya kilomita 10 kwenda na kurudi kutafuta elimu, hali iliyokuwa hatarishi kutokana na uwepo wa wanyama wakali katika eneo hilo.

Alisema uamuzi wa wananchi kujenga darasa hilo umeleta matumaini mapya kwa watoto na wazazi, kwani sasa watapata mazingira salama ya kujifunzia karibu na makazi yao.

Rais Samia Awatakia Waislamu Kheri katika Maadhimisho ya Maulid

Global Publishers
August 25, 2026
48 views
0 Comments

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewatakia Waislamu na Watanzania wote kheri na baraka katika Maadhimisho ya Sikukuu ya Maulid.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Rais Samia amesema Maulid inapaswa kuwa ukumbusho wa kuendelea kuishi kwa upendo, huruma, uvumilivu na kuwajali wengine katika jamii.

Amesisitiza umuhimu wa Watanzania kusherehekea Maulid kwa amani na furaha, huku wakidumisha umoja na mshikamano unaoendelea kuijenga Tanzania.

Rais Samia pia amemuomba Mwenyezi Mungu kuendelea kuibariki Tanzania, kuitunza katika amani na utulivu, pamoja na kuwawezesha wananchi kuijenga nchi kwa maendeleo na ustawi wa wote.

“Tusherehekee kwa amani na furaha huku tukidumisha umoja na mshikamano wetu. Mwenyezi Mungu Mtukufu aendelee kuibariki nchi yetu, kuitunza katika amani na utulivu, na kutuwezesha kuijenga kwa maendeleo na ustawi wa wote,” amesema Rais Samia.

Dk Nchimbi Atangaza Kujiuzulu Umakamu wa Rais na Kustaafu Siasa

Global Publishers
August 25, 2026
828 views
0 Comments

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Emmanuel John Nchimbi, ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo na kustaafu siasa pamoja na utumishi wa umma.

Dk Nchimbi ametoa taarifa hiyo leo Jumanne, Agosti 25, 2026, akisema amemwandikia Rais Samia Suluhu Hassan barua ya kumjulisha kuhusu uamuzi wake wa kujiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais, kuanzia Septemba 4, 2026.

Katika taarifa yake, Dk Nchimbi amesema uamuzi huo umetokana na ahadi aliyompa Rais Samia wakati alipoteuliwa kushika nafasi hiyo, kwamba angeendelea kumsaidia katika majukumu yake kwa uaminifu na uwezo wake wote, na angeachia nafasi hiyo iwapo angehisi Rais anahitaji mabadiliko.

“Nimejiridhisha pasipo shaka kuwa Mhe. Rais anatamani mabadiliko, hivyo nimeamua kutimiza ahadi yangu,” amesema Dk Nchimbi katika taarifa yake.

Aidha, amemshukuru Rais Samia pamoja na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa imani waliyoonyesha kwake, huku akiwashukuru Watanzania kwa ushirikiano na kumuunga mkono katika kipindi chake cha utumishi.

Dk Nchimbi amesisitiza kuwa licha ya kustaafu siasa na utumishi wa umma, ataendelea kuwa raia mwema na kulitumikia taifa katika nafasi nyingine.

Kujiuzulu kwake kunakuja ikiwa ni takribani mwaka mmoja tangu alipoanza kushika nafasi ya Makamu wa Rais, na endapo uamuzi huo utaidhinishwa, hatua hiyo itakuwa miongoni mwa matukio ya kipekee katika historia ya uongozi wa Tanzania.

Video: Simanzi Kihesa, Mrembo wa Miaka 23 Afariki Ndani ya Chumba Chake

Global Publishers
August 25, 2026
48 views
0 Comments


Mkazi wa Mtaa wa Kihesa, Halmashauri ya Mji wa Njombe, Edina Chaula, mwenye umri wa miaka 23, amefariki dunia baada ya kudaiwa kupata tatizo la kupaliwa na chakula akiwa ndani ya chumba chake.

Tukio hilo liliripotiwa Agosti 23, 2026, katika Mtaa wa Kihesa, mkoani Njombe.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Kamishna Msaidizi Mahamoud Banga, Edina alikutwa amefariki dunia ndani ya chumba chake baada ya kupata tatizo la kupaliwa na chakula.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa chakula hicho kilidaiwa kuziba njia yake ya hewa na kusababisha hali ya dharura iliyosababisha kifo chake.

Tukio hilo limeacha simanzi kwa ndugu, jamaa na wakazi wa eneo hilo.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe linaendelea na taratibu za uchunguzi ili kubaini kwa undani mazingira ya tukio hilo na kuthibitisha chanzo cha kifo.

Tukio hilo linakumbusha umuhimu wa kuchukua tahadhari wakati wa kula na kutoa msaada wa haraka kwa mtu anayepaliwa, kwani kuziba kwa njia ya hewa ni hali ya dharura inayoweza kuhatarisha maisha.

Marekani Yaiondoa Syria Kwenye Orodha ya Wafadhili wa Ugaidi

WASHINGTON — Marekani imeiondoa rasmi Syria kwenye orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi, hatua inayowakilisha mabadiliko makubwa katika sera ya Washington kuelekea taifa hilo la Mashariki ya Kati.

Syria iliwekwa kwenye orodha hiyo mwaka 1979, na kwa miongo kadhaa hatua hiyo iliambatana na vikwazo mbalimbali vya kiuchumi, kifedha na kibiashara.

Uamuzi huo unakuja wakati serikali mpya ya Syria chini ya Rais Ahmed al-Sharaa ikijaribu kujenga upya uhusiano wa nchi hiyo na mataifa ya Magharibi baada ya miaka ya vita na migogoro.

Washington imeeleza kuwa mabadiliko katika uongozi na sera za Damascus, pamoja na hatua za kupambana na ugaidi, yamekuwa miongoni mwa mambo yaliyozingatiwa katika kubadili msimamo wake.

Kuondolewa kwa Syria kwenye orodha hiyo kunaweza kufungua fursa zaidi za kiuchumi kwa nchi hiyo, ikiwamo kuvutia uwekezaji wa kimataifa, kuimarisha biashara na kurahisisha baadhi ya miamala ya kifedha. Hata hivyo, hatua hiyo haimaanishi kwamba vikwazo vyote vinavyolenga Syria na watu au taasisi maalumu vimeondolewa.

Kwa mujibu wa taarifa za serikali ya Marekani, Syria imekuwa ikikabiliwa na vikwazo mbalimbali tofauti na uteuzi wake kama nchi inayofadhili ugaidi. Baadhi ya hatua hizo zililenga mali za maafisa na watu waliotuhumiwa kuhusika na ukiukaji wa haki za binadamu au shughuli nyingine zilizolengwa na Marekani.

Hatua hiyo pia inakuja sambamba na mabadiliko katika mtazamo wa Marekani kuhusu Hay’at Tahrir al-Sham (HTS), kundi lililokuwa likihusishwa na al-Qaeda na ambalo liliwekwa kwenye orodha ya mashirika ya kigaidi ya Marekani mwaka 2014.

Kwa ujumla, uamuzi wa Washington unaashiria kuondoka taratibu kwenye sera ya muda mrefu ya kuitenga Syria na kuelekea katika ushirikiano unaolenga usalama, utulivu wa kisiasa na ujenzi wa uchumi wa nchi hiyo.

Hata hivyo, Marekani bado inatoa tahadhari kali kuhusu usalama nchini Syria kutokana na vitisho vya ugaidi, utekaji nyara, machafuko na mapigano katika baadhi ya maeneo.

Kwa Syria, kuondolewa kwenye orodha hiyo kunaweza kuwa hatua muhimu katika juhudi za kuirejesha nchi hiyo kwenye mfumo wa uchumi wa kimataifa. Kwa Marekani, ni ishara kwamba sera yake kuelekea Damascus imeanza kubadilika kwa kiwango kikubwa baada ya zaidi ya miongo minne ya Syria kuwa chini ya hadhi ya nchi inayofadhili ugaidi.

Stori Na Erick Elibariki | GPL -TUDACO

BREAKING..DKT NCHIMBI AJIUZULU SIASA NA UTUMISHI WA UMMA

Makamu wa Rais Dr Emmanuel John Nchimbi amemwandikia barua Rais wa JMT kuwa ameamua kustaafu siasa na utumishi wa Umma hivyo ni sahihi kusema amejiuzulu nafasi yake ya Umakamu wa Rais kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri.

Taarifa imechapishwa kwenye ukurasa wake rasmi ila bado kurasa rasmi za Ofisi ya Makamu wa Rais hazijapandisha taarifa hiyo.

Visima kuongeza upatikanaji maji Nyang’hwale – HabariLeo

GEITA: WAKALA wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) imesema Mradi wa Maji wa Visima 5 vya Jimbo wilayani Nyang’hwale mkoani Geita umeongeza upatikanaji wa maji kutoka asilimia 77.4 hadi asilimia 79.6

Meneja wa RUWASA wilayani Nyang’hwale, Mhanidisi Suzana Mabula ametoa taarifa hiyo mbele ya viongozi wa mbio za Mwenge kitaifa kwa mwaka 2026 katika kata ya Kanegele wilyani humo.

Amesema mradi huo umetekelezwa katika Vijiji vya Kanegele, Mwingiro, Shabaka, Wavu na Lubando na unazalisha jumla ya lita 21,150 kwa saa ambapo takribani wananchi 5,000 ambapo watapata huduma ya maji safi na salama.

“Mkataba wa Ujenzi wa Vioski ulianza rasmi mnamo Julai 01/2025 na ulitarajiwa kukamilika Septemba 02, 2026 lakini hadi kufika Agosti 10, 2026 mradi ulikuwa tayari umekamilika”, amesema Suzana.

Suzana amesema gharama za utekelezaji wa Mradi wa Maji katika Vijiji hivi vitano (5) ni sh milioni 336 na hadi sasa Jumla ya kiasi cha sh milioni 245 kimekwisha kutumika.

“Chanzo cha fedha za Mradi huu ni kupitia Mpango wa Malipo kulingana na Matokeo (PforR) na Fedha Maalum (Special Fund)”, amesema Mhandisi Suzana.

Ametaja miongoni mwa shughuli zilizofanyika ununuzi wa matenki ya plastiki yenye ujazo wa lita 10,000 na kulaza mabomba na kufukia umbali wa mita 9,467, Ujenzi wa chemba kubwa tano na ndogo sita za maji.

“Uendeshaji wa mradi huu upo chini ya Jumuiya ya Watoa Huduma ya Maji ngazi ya Jamii(CBWSO’s) ya Nyamtukuza visima Vitatu na JWPP visima Viwili”, amesema Suzana.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Mwaka 2026, Wazo Michael Mwang’oda amezindua mradi huo na kusisitiza kuwa dhamira ya serikali na kuhakikisha wananchi wake wnaapata maji safi na salama hivo usimamizi thabiti wa mradi huo ufanyike.

Amesema wilaya ya Nyang’hwale ni miongoni mwa maeneo ambayo serikali inaendeelea kuwekeza ujenzi wa mbalimbali kwa maslahi ya jamii na hivo viongozi wanapaswa kusimamia kikamirifu ili malengo ya utatuzi wa changamoto za kijami yafikiwe.

Fahamu Kiumbe Cha Bahari Chenye Siri Nyingi Za Kushangaza, Soma Hapa

Pweza ni kiumbe cha baharini chenye maajabu mengi ikiwemo kuwa na mioyo 3 ambapo moyo mmoja husukuma damu kwenda sehemu mbalimbali za mwili na mioyo 2 husukuma damu kupitia matamvua yake.

Tofauti na viumbe wengine wenye damu nyekundu, Pweza ana damu ya rangi ya bluu kwa sababu ana “copper-based protein”.

Pweza ni miongoni mwa viumbe wenye akili zaidi duniani, mstaarabu na msafi. Anayo mikia au mikono nane na macho mawili makubwa. Jamii za samaki pweza ni zaidi ya jamii 289 kulingana na chapisho la World Animal Foundation.

Pweza wa kawaida huwa anakuwa na urefu wa inchi 12-36 na uzito wa kilo 3-10. Pweza mkubwa zaidi duniani anapatikana katika Bahari ya Pacific, jamii ya Enteroctopus dofleini anakuwa mkubwa hadi mita 5 urefu na kilo hadi 50 kwa mujibu wa World animal foundation.

Pweza anakula nyama tu (carnivores), hupendelea kula jamii ya dagaa kamba (uduvi) na samaki, akiwinda kwa kutumia mikono yake nane.

Pweza anauwezo wa kubadili rangi kama kinyonga kulingana na mazingira aliyopo, unaweza kubadilika katika rangi tafauti kama kuwa rangi ya bluu, pinki, rangi ya ugoro au kijani ili kujificha na kufanana na mazingira yaliyomzunguka kutokana na maadui.

Pweza pia humwaga wino na kukimbia kwa kasi sana na kumfanya adui asimuone kwa sababu ya maji kuchanganyikana na wino na kufanya hali kama ukungu.

Uzalianaji wa pweza huwa ni wa kutaga mayai na kuyalinda mpaka kutotolewa. Pweza ni kiumbe asiyekuwa na wivu wa kimapenzi, jike moja hupandwa na madume zaidi ya 10 wakiwa wamemzunguka kwa kuweka duara na kumuweka katikati kisha madume kuachiana zamu ya kujamiiana.

Pweza dume huwa na mkono mmoja kati ya 8 mahususi kwa kupitisha mbegu za uzazi. Pweza dume baada ya kumaliza kujamiiana na jike hukaa muda mfupi na kufa kwa sababu huwa anamaliza akili na nguvu za kutafuta chakula na hatimaye kuishiwa nguvu na kufa.

Pweza jike ana uwezo wa kutaga mayai Zaidi ya (200,000 – 400,000) inategemeana na jamii ya pweza. Pweza jike hulalia na kulinda mayai mpaka mayai yatotolewe au kuanguliwa pia huwalinda watoto wake kwa muda mpaka wakue.

Makala na Elvan Stambuli, Global Digital