Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar Akutana na Araqchi Tehran

Global Publishers
August 27, 2026
18 views
0 Comments

 

Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar, Mohammed bin Abdulrahman Al Thani, amekutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, mjini Tehran Alhamisi jioni, katika ziara inayofanyika wakati juhudi za kidiplomasia kuhusu hali ya Mashariki ya Kati zikiendelea.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyombo vya habari vya Iran, viongozi hao wamefanya mazungumzo, ingawa maelezo ya kina kuhusu masuala yaliyojadiliwa katika mkutano huo bado hayajawekwa wazi.

Kabla ya ziara hiyo, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei, alisema Al Thani angejadili na maafisa wa Iran mwendelezo wa juhudi za Qatar za upatanishi pamoja na masuala mengine yanayoendelea katika eneo hilo.

Ziara ya Waziri huyo wa Qatar imekuja siku mbili baada ya Kamanda wa Jeshi la Pakistan, Field Marshal Asim Munir, kufanya ziara nchini Iran.

Qatar na Pakistan ni miongoni mwa nchi zilizohusika katika juhudi za kidiplomasia za upatanishi wakati wa kusainiwa kwa hati ya makubaliano kati ya Iran na Marekani.

Hata hivyo, hadi sasa hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kuhusu matokeo ya mazungumzo kati ya Al Thani na Araqchi.

Kutokana na hali hiyo, taarifa kuhusu iwapo viongozi hao wamefikia makubaliano au kufanya maamuzi yoyote katika mkutano huo bado hazijathibitishwa rasmi.

Stori na Na: Ilankize Godfrey | GPL TUDACO

Rais Samia Ateua na Kuhamisha Wakuu Wa Mikoa, Makatibu Tawala

Global Publishers
August 27, 2026
54 views
0 Comments

Dar es Salaam, Agosti 27, 2026 — Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi na uhamisho wa Wakuu wa Mikoa pamoja na Makatibu Tawala wa Mikoa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari S. Machumu, uteuzi na uhamisho huo umefanyika kama ifuatavyo:

UTEUZI WA WAKUU WA MIKOA
  1. CP. Salum Rashid Hamduni, aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.
  2. Alexander Pastory Mnyeti ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita.
  3. Stanslaus Haroon Nyongo ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
  4. Jumanne Abdallah Sagini ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.
UHAMISHO WA WAKUU WA MIKOA
  1. Martine Reuben Shigela amehamishwa kutoka Mkoa wa Geita kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara.
  2. Said Mohamed Mtanda amehamishwa kutoka Mkoa wa Mwanza kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, akichukua nafasi ya Anamringu Macha ambaye amestaafu.
  3. Abubakar Mussa Kunenge amehamishwa kutoka Mkoa wa Pwani kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe, akichukua nafasi ya Jabiri Omari Makame, ambaye atapangiwa majukumu mengine.
  4. Beno Moris Malisa amehamishwa kutoka Mkoa wa Mbeya kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora. Anachukua nafasi ya Paul Matiko Chacha, ambaye aliteuliwa kuwa Katibu wa NEC – Idara ya Oganaizesheni ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
  5. Adam Kighoma Malima amehamishwa kutoka Mkoa wa Morogoro kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, akichukua nafasi ya Zainab Telack, ambaye amestaafu.
  6. Queen Cuthbert Sendiga amehamishwa kutoka Mkoa wa Manyara kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
UTEUZI NA UHAMISHO WA MAKATIBU TAWALA WA MIKOA

Uteuzi

Richard Marcellino Kayombo ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani.

Uhamisho

  1. Bw. Balandya Mayuganya Elikana amehamishwa kutoka Mkoa wa Mwanza kwenda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya.
  2. Dkt. Fatuma Ramadhan Mganga amehamishwa kutoka Mkoa wa Singida kwenda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza.
  3. Pili Hassan Mnyema amehamishwa kutoka Mkoa wa Pwani kwenda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga.
  4. Rodricks Lazaro Mpogolo amehamishwa kutoka Mkoa wa Mbeya kwenda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa upashaji wa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa wateule utafanyika kwa tarehe itakayopangwa baadaye.

Uteuzi na uhamisho huo umetangazwa na Ikulu, Dar es Salaam, Agosti 27, 2026.

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI NA UHAMISHO WA WAKUU WA MIKOA

 

NA MATUKIO DAIMA MEDIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi na uhamisho wa Wakuu wa Mikoa pamoja na Makatibu Tawala wa Mikoa katika mabadiliko yaliyotangazwa leo, Agosti 27, 2026.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari S. Machumu, mabadiliko hayo yamehusisha uteuzi wa Wakuu wa Mikoa wanne na uhamisho wa wengine sita.

Katika uteuzi huo, CP. Salum Rashid Hamduni, aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, huku Alexander Pastory Mnyeti akiteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Aidha, Stanslaus Haroon Nyongo ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, wakati Jumanne Abdallah Sagini akiteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

Katika uhamisho wa Wakuu wa Mikoa, Martine Reuben Shigela amehamishwa kutoka Geita kwenda Manyara, huku Said Mohamed Mtanda akihamishwa kutoka Mwanza kwenda Simiyu, akichukua nafasi ya Anamringi Macha ambaye amestaafu.

Vilevile, Abubakar Mussa Kunenge amehamishwa kutoka Pwani kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe, akichukua nafasi ya Jabiri Omari Makame ambaye atapangiwa majukumu mengine.

Beno Moris Malisa amehamishwa kutoka Mbeya kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, akichukua nafasi ya Paul Matiko Chacha ambaye aliteuliwa kuwa Katibu wa NEC – Idara ya Organizesheni ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Naye Adam Kighoma Malima amehamishwa kutoka Morogoro kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, akichukua nafasi ya Zainab Telack ambaye amestaafu, huku Queen Cuthbert Sendiga akihamishwa kutoka Manyara kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

MABADILIKO YA MAKATIBU TAWALA

Katika hatua nyingine, Rais Samia amemteua Richard Marcellino Kayombo kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani.

Pia, Barahindya Mavuganya Elikana amehamishwa kutoka Mwanza kwenda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya; Dkt. Fatuma Ramadhan Mganga amehamishwa kutoka Singida kwenda Mwanza; Pili Hassan Mnyema amehamishwa kutoka Pwani kwenda Shinyanga; na Rodrick Lazaro Mpogolo amehamishwa kutoka Mbeya kwenda kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida.

Taarifa ya Ikulu imeeleza kuwa uapisho wa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa walioteuliwa utafanyika katika tarehe itakayopangwa baadaye.

Taarifa hiyo imetolewa Dar es Salaam, Agosti 27, 2026.

Mavunde Ampongeza Ndejembi “Ni Kiongozi Kijana, Mwadilifu na Mzalendo” – Video

Global Publishers
August 27, 2026
36 views
0 Comments

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amempongeza Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, kufuatia kuteuliwa kwake kushika nafasi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mavunde ametoa pongezi hizo leo, Alhamisi, Agosti 27, 2026, wakati viongozi mbalimbali wakiendelea kutoa pongezi kwa Ndejembi baada ya jina lake kupitishwa kwa ajili ya kujaza nafasi hiyo.

Nafasi hiyo imekuwa wazi kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Emmanuel Nchimbi.

Akizungumza kuhusu uteuzi huo, Mavunde amemuelezea Ndejembi kuwa ni kiongozi kijana, mwadilifu na anayelipenda Taifa, akisema amepokea kwa furaha uteuzi wake katika nafasi hiyo ya juu ya uongozi wa nchi.

Mavunde amesema sifa na uwezo alionao Ndejembi vitamsaidia kutekeleza majukumu yake mapya kwa ufanisi na kuendelea kulitumikia Taifa.

Ameongeza kuwa uteuzi huo ni hatua muhimu kwa Ndejembi na amemtakia kila la heri katika majukumu yake mapya ya kitaifa.

Uteuzi wa Ndejembi umeendelea kuzua pongezi kutoka kwa viongozi na wadau mbalimbali, huku akitarajiwa kuanza jukumu hilo jipya baada ya kukamilika kwa taratibu zinazohitajika kikatiba.

MWABUKUSI: KUFUKUZWA CCM KWA NCHIMBI HAKUMVUI MOJA KWA MOJA UMAKAMU WA RAIS

NA MATUKIO DAIMA MEDIA

Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Wakili Boniface Mwabukusi, amesema hatua ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumvua uanachama Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi haimaanishi moja kwa moja kwamba amepoteza nafasi yake ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kauli hiyo imekuja wakati kukiwa na mjadala kuhusu athari za kikatiba za uamuzi wa CCM kumfukuza Dkt. Nchimbi uanachama, huku barua yake ya kujiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais ikieleza kuwa kujiuzulu kwake kutaanza rasmi Septemba 4, 2026. 

Taarifa za kujiuzulu kwake na tarehe hiyo zimethibitishwa pia na vyombo mbalimbali vya habari.

Kwa mujibu wa maoni ya Mwabukusi yaliyochapishwa katika ukurasa wa Mwananchi Digital, Katiba haijaweka kufukuzwa uanachama wa chama cha siasa kuwa sababu inayomwondoa moja kwa moja mtu katika nafasi ya Makamu wa Rais.

Mwabukusi amesema kwa kuwa Dkt. Nchimbi aliwasilisha barua ya kujiuzulu kwa Rais na kueleza kuwa uamuzi huo utaanza kutumika Septemba 4, 2026, na Rais akakubali kujiuzulu kwake kuanzia tarehe hiyo, basi kwa mtazamo wake anaendelea kuwa Makamu wa Rais hadi kufikia tarehe hiyo, isipokuwa kama kutakuwa na utaratibu mwingine wa kikatiba utakaofuatwa.

Dkt. Nchimbi alitangaza kujiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais na kustaafu siasa pamoja na utumishi wa umma, huku uamuzi wake ukitarajiwa kuanza rasmi Septemba 4, 2026.

Siku iliyofuata, CCM ilitangaza kumvua uanachama Dkt. Nchimbi baada ya vikao vya chama kupitia masuala ya nidhamu na maadili yaliyomhusu. 

Chama pia kilimpitisha Waziri wa Nishati na Mbunge wa Chamwino, Deogratius Ndejembi, kuwa mgombea wa kujaza nafasi ya Makamu wa Rais.

Mwabukusi amesisitiza kuwa CCM ina mamlaka ya kumvua Dkt. Nchimbi uanachama kwa mujibu wa taratibu zake, lakini chama chenyewe hakiwezi kumwondoa katika ofisi ya Makamu wa Rais nje ya misingi na taratibu zilizowekwa na Katiba.

Amesema hali hiyo inaibua hoja ya kikatiba inayohitaji tafsiri kuhusu maudhui ya Ibara ya 47 na 50 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa Mwabukusi, suala hilo linahitaji tafsiri muhimu ya kisheria, ambayo amesema inaweza kutolewa na Mahakama.

Wakati huo huo, Katiba inaweka utaratibu wa kujaza nafasi ya Makamu wa Rais inapokuwa wazi. 

Rais anatakiwa kumteua Makamu wa Rais mwingine ndani ya siku 14 baada ya nafasi kuwa wazi, na uteuzi huo kuthibitishwa na Bunge kwa kura ya wabunge walio wengi.

MWISHO

Dili la Sh Bilioni 418! Liverpool Yafikia Makubaliano na PSG kwa Barcola

Global Publishers
August 27, 2026
6 views
0 Comments

Liverpool imefikia makubaliano ya awali yenye thamani ya takribani Shilingi bilioni 418 (£120 milioni) na Paris Saint-Germain (PSG) kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa pembeni wa Ufaransa, Bradley Barcola.

Makubaliano hayo bado hayajakamilishwa rasmi, lakini hatua hiyo imeelezwa kuwa ni mafanikio makubwa katika mazungumzo ya muda mrefu kati ya Liverpool na PSG kuhusu uhamisho wa nyota huyo.

Kwa muda wote wa dirisha hili la usajili, kumekuwa na tofauti kubwa katika tathmini ya thamani ya Barcola kati ya klabu hizo mbili. PSG ilikuwa ikimtaka Liverpool ilipe kiasi cha karibu £145 milioni, sawa na takribani Shilingi bilioni 505, ili kumruhusu mchezaji huyo kuondoka.

Hata hivyo, Liverpool sasa imepiga hatua kubwa baada ya kufikia makubaliano ya kimsingi ya £120 milioni, ambayo ni takribani Shilingi bilioni 418.

Barcola amekuwa akitajwa kuwa miongoni mwa wachezaji wanaolengwa na Liverpool katika dirisha hili la usajili, huku klabu hiyo ikitaka kuongeza nguvu na chaguo katika safu yake ya ushambuliaji.

Mchezaji huyo wa PSG amekuwa na nafasi muhimu katika kikosi cha mabingwa hao wa Ufaransa, jambo lililofanya klabu hiyo kuweka thamani kubwa kwake.

Pamoja na kufikiwa kwa dili hilo la awali, bado kuna hatua za mwisho zinazopaswa kukamilishwa kabla ya uhamisho huo kuthibitishwa rasmi na pande zote mbili.

Iwapo makubaliano hayo yatakamilika kwa thamani ya Sh bilioni 418, Barcola atakuwa miongoni mwa wachezaji wenye thamani kubwa zaidi kusajiliwa katika historia ya Liverpool.

Liverpool sasa inatarajiwa kukamilisha mazungumzo ya mwisho na PSG pamoja na taratibu nyingine za uhamisho kabla ya Barcola kuweza kuanza rasmi safari yake mpya katika Premier League.

Droo ya UEFA Champions League Msimu wa 2026/27 Kufanyika Leo Monaco

Droo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League) msimu wa 2026/27 inafanyika leo, Alhamisi Agosti 27, 2026, mjini Monaco, ambapo timu 36 zitajua wapinzani wao katika hatua ya ligi.

Droo hiyo itaanza majira ya saa 1:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki, huku mashindano yakiendelea kutumia mfumo mpya ambao umeondoa makundi ya kawaida yenye timu nne.

Katika mfumo huo, timu zote 36 zitakuwa kwenye ligi moja, ambapo kila klabu itacheza jumla ya michezo minane dhidi ya wapinzani tofauti. Kila timu itakutana na timu mbili kutoka kila moja ya pot nne za upangaji.

Miongoni mwa vigogo waliopo kwenye droo hiyo ni Real Madrid, Barcelona, Liverpool, Manchester City, Arsenal, Bayern Munich, Paris Saint-Germain, Inter Milan na Atlético Madrid, ambao wamewekwa kwenye Pot 1.

Pot 2 ina timu kubwa kama Manchester United, Borussia Dortmund, Roma, Porto, Aston Villa na PSV, wakati Pot 3 ikiwa na Napoli, RB Leipzig, Villarreal, Galatasaray na Fenerbahçe.

Kwa upande wa Pot 4, timu zinazotarajiwa kushiriki droo hiyo ni pamoja na Stuttgart, LASK, Como, Lens na Slavia Prague.

Michezo ya hatua ya ligi ya Champions League inaanza Septemba 8, 2026, huku ratiba kamili ya kila timu ikitarajiwa kutolewa kabla au ifikapo Agosti 29.

Fainali ya msimu huu imepangwa kufanyika katika Uwanja wa Estadio Metropolitano, Madrid, Hispania, Juni 5, 2027.

Droo hiyo inatarajiwa kuvuta hisia kubwa kutokana na uwezekano wa vigogo kama Real Madrid, Liverpool, Barcelona, Arsenal na Manchester City kukutana na ratiba ngumu mapema katika safari yao ya kuwania ubingwa wa Ulaya.

Na Ashura Karimu, DSJ.

 

Kesi ya Uhaini ya Lissu Yaendelea leo;- Maswali Mazito Yaibuka Katika Dodoso la Serikali

Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, imeendelea leo Agosti 27, 2026  katika Mahakama jijini Dar es Salaam, baada ya mwenendo wake kuahirishwa jana.

Katika mwenendo wa jana, upande wa Serikali uliendelea na hatua ya kumuuliza Lissu maswali ya dodoso baada ya kuwasilisha ushahidi wake wa kujitetea.

Mwendesha mashtaka Katuga alianza kwa kumuuliza Lissu kuhusu vielelezo alivyowasilisha mahakamani, ambapo Lissu alithibitisha kuwa vielelezo D1 hadi D15 ni vyake na kwamba ameridhika vitumike katika utetezi wake.

Katika sehemu nyingine ya mahojiano, Katuga alimuuliza Lissu kuhusu maana ya ulinzi wa mashahidi, ambapo Lissu alisema ni mashahidi wa kificho au wanaolindwa.

Lissu pia alihojiwa kuhusu madai yake kwamba baadhi ya watu waliokuwa ndani ya mahakama huenda walikuwa mashahidi waliolindwa. Alipoulizwa kama madai hayo yalikuwa ushahidi au hisia, Lissu alisisitiza kuwa ni ushahidi kwa sababu watu hao hawakujulikana na umma.

Lissu: Ni vyangu kwa sababu mimi ndiye niliyeomba viingizwe mahakamani.

Katuga: Je, nikisema kwamba uliomba vipokelewe mahakamani kama vielelezo vyako, umeridhika na yaliyomo ndani ya vielelezo hivyo?

Lissu: Ndiyo, nimeridhika.

Katuga: Umeridhika vitumike kama vielelezo vyako, na unaridhika na vielelezo ulivyovitoa?

Lissu: Nimeridhika vitumike katika utetezi wangu.

Katuga: Waheshimiwa Majaji, tunaomba vielelezo D1 hadi D15 …

Katuga: Naona tutakaa hapa siku mbili

Lissu: Unanitisha na siku mbili nimekaa ndani mwaka na miezi mitano

Katuga: Iambie mahakama ulinzi wa mashahidi maana yake nini

Lissu: Ni mashahidi wa kificho/ ni mashahidi wanaolindwa

Katuga: Iambie mahakama, Je, ulisema baadhi ya watu huenda tulikuwa nao humu ndani. Je, huu ni ushahidi au hisia tupu?

Lissu: Ndio ni shahidi wangu sababu hawajulikani hakuna anayewajua isipokua nyie

Katuga: Je ushahidi wa kwamba hawa ni mapolisi. Je, ni ushahidi au fununu tu?

Lissu: Ni ushahidi sababu hawajulikani na yeyote

Katuga: Sasa shahidi tunataka majibu sahihi ni kweli au sio kweli. Ushahidi wa kwamba baadhi ya mashahdi huenda tulikuwa nao humu ndani. JE, ni kweli, sio kweli, sio wa kuona wala kusikia?

Lissu: Sio Kweli

Katuga: Iambie mahakama kama ni kweli au sio kweli unatuhuma nyingie za kuchapisha uongo mtandaoni

Lissu: Ni kweli

Katuga: Iambie mahakama unakumbuka ulisomewa hoja za awali na ikaanza kusikilizwa

Lissu: Ndio nianakumbuka

Katuga: Unakumbuka uliposomewa hoja za wali ulisema majaji ni ma-CCM

Lissu: Sikumbuki

Katuga: Iambie mahakama hii katika hotuba yako pia ulitangaza kutokugombea kwa chama chako

Lissu: Sikumbuki, nakumbuka nilisema tutahamasisha ….

Katuga: Hapana, hukumbuki nimsekia ukijiita mwenyekiti wa Chadema. Iambie mahakama kama chama chako kilishiriki uchaguzi mwaka jana

Lissu: Hapana hakikushiriki

Katuga: Je, ni kweli kwamba uliposema mahakamani hakuendeki huna imani na mahakama

Lissu: Kwenye maswala haya ya uchaguzi sina imani na mahakama

Katuga: Kwenye zile njia ulizotuambia jana. Je, nitakuwa sahihi kwamba hukupanga kabisa kuiomba mahakama kutumia sheria

Lissu: Sikupanga kabisa

Katuga: Kwa hiyo ni sahihi kwamba swala la kupinga sheria kwa njia ya mahakama sio njia mbadala wala ya kidemokrasia

Lissu: Hapana

Katuga: Kwa hiyo kukinukisha ni njia ya kidemokrasia?

Lissu: Ndio ni njia ya kidemokrasia

Katuga: Kuhamasisha uasi ni njia ya kidemokrasia?

Lissu: Ndio ni njia ya kidemokrasia

Katuga: Uko Timamu mzee wangu

Lissu: Kimya

Katuga: Kama nilikusia ulitamka vifungu vya 55, 63, 52 kifungu cha 52 cha sheria ya habari. Ni kweli kwamba sheria ya habari iliundwa kwa ajili ya kuendesha tasnia ya habari?

Lissu: Ndio

Katuga: Kama nilikusikia vyema ulisema kuikosoa serikali sio kosa

Lissu: Nilisema kuipinga serikali sio kosa

Katuga: Kama una kanuni yako ya adhabu hapo kwa ridhaa ya mahakama hiki kifungu cha 55, yale maneno uliyotumbua, ‘ya kuzuia uchaguzi’ waambie majaji kuzuia uchaguzi ni kuipinga serikali au kuzuia uchaguzi?

Lissu: NI kuzuia uchaguzi

Katuga: Kuhamasisha uasi, kukinukisha nikupinga serikali au kupanga kuipindua serikali?

Lissu: Ni kuipinga serikali, sikuwa nazungumza habari ya serikali tulikuwa tunapanga kuzuia uchaguzi

Katuga: Unakumbuka umesema kwenye hotuba yako ulikuwa huzungumzii serikali

Lissu: Ndio sikuwa napinga serikali nilikua nazungumza habari za uchaguzi

Katuga: Kama nikikusikia vyema uliwaambia waheshimiwa hawa mashahidi wanaotoka jeshi la polisi, kasoro mmoja, wote wamejiandikia maelezo kitu ambacho ni kinyume cha sheria. Waambie majaji kama uliwatajia kifungu cha sheria na sheria yenyewe

Lissu: Sikuwaambia kifungu lakini kipo

Katuga: Unajua kwamba askari aliyemuandika shahidi maelezo na yeye ni shahidi kama huyo shahdi hata fika mahakani

Lissu: Sikumbuki

Katuga: Kama nilikusikia vyema uliiambia mahakama hii kwamba shahidi PW1 hakusema kama alivyogundua ni kosa la uhaini hakuwasiliana na ngazi za juu akiwemo DCI, kwamba ilipelelezwa vibaya

Lissu: nilisema ilipelelezwa vibaya

Katuga: Iambie mahakama kama sheria inaelekeza ukigundua kosa la uhaini lazima uwasiliane na hizo mamlaka zote, imabie mahakama kama ulitaja kifungu

Lissu: Hapana sikutaja kifungu

Katuga: Je unakumbuka ulisema kuna kutoelewana kati yako na Kingai (Kamishna wa Polisi Ramadhani Kingai ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) nchini Tanzania) pamoja na IGP Wambura (Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Camillius Wambura)

Lissu: Ni kweli nimekamatwa mara kadhaa bila kuzingatia taratibu

Katuga: Umekuwa mwanasheria muda mrefu na mwana siasa miaka 24. Je, ushawafunguliwa wawili hawa mashitaka?

Hapana: Sijawafungulia

Katuga: Kama nimekusikia vizuri uliambia mahakama hii kwamba wale mashahdi walioletwa ni mashahidi ambao walikuwa ni washitakiwa

Lissu: Nilisema walikiri kupanga uhalifu

Katuga: Je, kuna sheria inayozuia mtu aliyefanya uhalifu kuja kutoa ushahidi?

Lissu: Hapana

Katuga: Katika ushahidi wa mashahidi toka Jeshi la polisi walieleza walikamata wote

Lissu: Waliokamata waliweza kuwatambua

Katuga: Kwa ushahidi huo ina maana inawezekana kukawa na wengine

Lissu: Hawakutambuliwa au hawakukamatwa

Katuga: Nakukumbusha ile kauli yako si ndio uliambia mahakama mtu yeyote anaweza kutafsiri vyovyote vile na wale walisema wamehamasika kutokana na nini

Lissu: Maneno yangu

Katuga: Kwa hiyo nitakuwa sahihi nikisema walielewa hotuba yako na kufanyia kazi maneno yako kwa jinsi walivyoelewa

Lissu: Hapana siwezi sema sababu siwajui na siwezi kuwasemea

Katuga: Je, uliiambia mahakama hawa mashahidi ni waongo na hawastahili kuaminiwa na mahakama?

Lissu: Ndio, niliambia mahakama hawapaswi kuaminiwa wao na ushahidi wao

Nafasi za Kazi Wezesha Mzawa Microfinance – Loan Officer, Mwisho wa Maombi Agosti 31, 2026

Global Publishers
August 27, 2026
8,256 views
0 Comments

We are seeking a motivated, experienced Loan officer/ Credit officer to join our growing company. In this position, you will evaluate and approve or deny loan applications. You will act as liaison between financial institutions, individuals, and businesses applying for loans as well as process loan applications, solicit loans, and act as intermediary for creditors and borrowers.

Loan Officer Job Duties:

  • Evaluates loan applications and documentation by confirming credit worthiness.
  • Improves loan applications and documentation by informing applicant of additional requirements.
  • Rejects loans by explaining deficiencies to applicants.
  • Approves loans by issuing checks or forwarding applications to loan committee.
  • Completes loan contracts by explaining provisions to applicant; obtaining signatures and notarizations; collecting fees.
  • Helps customers by answering questions; responding to requests.
  • Maintains customer confidence by keeping loan information confidential.
  • Accomplishes Company mission by completing related results as needed.

Qualification;

  • Bachelor of finance, economics, Marketing, Business, Banking or related field
  • Experience in the relevant field will be an added advantage
  • Proficient computer skills, including Microsoft Office Suite
  • Able to analyze financial records and transfer data

Additional Knowledge, Skills & Abilities

  • Excellent customer service skills, attentiveness, and information retention.
  • Detail oriented, high degree of accuracy.
  • Familiar with banking regulations and responsibilities relating to each including a working.
  • Self-starter, ability to work independently.
  • Strong communication & organizational skills.
  • Competence with computers.
  • Ability to work in a fast-paced environment & under pressure as needed.
  • The ability to make sound decisions. This may include making on-the-spot decisions regarding customer transactions; weighing customer satisfaction issues with the Bank’s exposure to loss or fraud and the ability to think through and rationalize decisions.

All applications should be filed through the following email address or the physical address with necessary certified attachments befor August 31, 2026.

WEZESHA MZAWA MICROFINANCE,

P.O.BOX 7534, SINZA-MORI,

OPPOSITE WANYAMA HOTEL

DAR ES SALAAM, TANZANIA.

EMAIL: [email protected]

Safari Mpya Imeanza! Fahamu Mchezo wa 3 Fisher Cats Meridianbet

Global Publishers
August 27, 2026
60 views
0 Comments

Kama unafikiri uvuvi ni wa wavuvi pekee, 3 Fisher Cats kutoka Amigo imekuja kubadilisha mtazamo huo. Meridianbet imeleta mchezo unaowaleta paka watatu wenye ujanja wa kuvua samaki na kutafuta hazina zinazoweza kujitokeza kwenye kila raundi. Ni safari yenye mvuto wake, ikichanganya wahusika wa kuchekesha, mandhari ya uvuvi na burudani inayoweza kuanza mara tu unapozungusha.

Kwenye mchezo huu, kila paka ana jukumu lake huku ndoano zikiwa tayari kuingia majini. Kila mzunguko unafungua ukurasa mpya wa safari, na jambo la kuvutia ni kwamba huwezi kutabiri kitakachotokea kabla ya raundi kuendelea. Mchezo unakupa nafasi ya kufuatilia harakati za paka hao huku ukisubiri kuona kama safari yao imeleta samaki, zawadi au sapraizi nyingine.

Vilevile, meridianbet wana michezo mingi ya kasino mtandaoni na mechi za kimataifa za kubashiri zenye ushindani mkubwa wa odds. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

3 Fisher Cats pia inajenga msisimko kupitia mfumo wake wa kucheza unaokufanya utake kuona kinachofuata. Kila raundi ni fursa ya kuchunguza mchezo zaidi na kufurahia vipengele vyake vya kipekee. Kama mvuvi anavyosubiri kuvutwa kwa ndoano baada ya muda wa kusubiri, ndivyo kila mzunguko unavyoweza kuleta matarajio mapya ndani ya mchezo.

Kwa wapenzi wa michezo mipya, hii ni nafasi ya kuingia kwenye safari ambayo haijafanana na nyingine. Paka hao watatu wamechukua jukumu la wavuvi, bahari imekuwa uwanja wao wa kazi na kila mzunguko unaleta nafasi ya kuendelea na burudani. Meridianbet inakupa mazingira ya kuufurahia mchezo huu huku ukigundua taratibu kila kitu ambacho Amigo imekiweka ndani yake.

Hivyo basi, usisubiri paka hao watatu warudi ufukweni bila wewe. Shika nafasi yako kwenye 3 Fisher Cats, zungusha raundi zako na fuatilia safari ya paka hao wajanja. Kila raundi ina simulizi yake, na kila safari huanza kwa hatua moja tu. Safari ya uvuvi imehamia Meridianbet, ni wakati wa kuingia ndani.