Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Burudani

Kesi ya Uhaini ya Lissu Yaendelea leo;- Maswali Mazito Yaibuka Katika Dodoso la Serikali

By admin
August 27, 2026 4 Min Read
Comments Off on Kesi ya Uhaini ya Lissu Yaendelea leo;- Maswali Mazito Yaibuka Katika Dodoso la Serikali

Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, imeendelea leo Agosti 27, 2026  katika Mahakama jijini Dar es Salaam, baada ya mwenendo wake kuahirishwa jana.

Katika mwenendo wa jana, upande wa Serikali uliendelea na hatua ya kumuuliza Lissu maswali ya dodoso baada ya kuwasilisha ushahidi wake wa kujitetea.

Mwendesha mashtaka Katuga alianza kwa kumuuliza Lissu kuhusu vielelezo alivyowasilisha mahakamani, ambapo Lissu alithibitisha kuwa vielelezo D1 hadi D15 ni vyake na kwamba ameridhika vitumike katika utetezi wake.

Katika sehemu nyingine ya mahojiano, Katuga alimuuliza Lissu kuhusu maana ya ulinzi wa mashahidi, ambapo Lissu alisema ni mashahidi wa kificho au wanaolindwa.

Lissu pia alihojiwa kuhusu madai yake kwamba baadhi ya watu waliokuwa ndani ya mahakama huenda walikuwa mashahidi waliolindwa. Alipoulizwa kama madai hayo yalikuwa ushahidi au hisia, Lissu alisisitiza kuwa ni ushahidi kwa sababu watu hao hawakujulikana na umma.

Lissu: Ni vyangu kwa sababu mimi ndiye niliyeomba viingizwe mahakamani.

Katuga: Je, nikisema kwamba uliomba vipokelewe mahakamani kama vielelezo vyako, umeridhika na yaliyomo ndani ya vielelezo hivyo?

Lissu: Ndiyo, nimeridhika.

Katuga: Umeridhika vitumike kama vielelezo vyako, na unaridhika na vielelezo ulivyovitoa?

Lissu: Nimeridhika vitumike katika utetezi wangu.

Katuga: Waheshimiwa Majaji, tunaomba vielelezo D1 hadi D15 …

Katuga: Naona tutakaa hapa siku mbili

Lissu: Unanitisha na siku mbili nimekaa ndani mwaka na miezi mitano

Katuga: Iambie mahakama ulinzi wa mashahidi maana yake nini

Lissu: Ni mashahidi wa kificho/ ni mashahidi wanaolindwa

Katuga: Iambie mahakama, Je, ulisema baadhi ya watu huenda tulikuwa nao humu ndani. Je, huu ni ushahidi au hisia tupu?

Lissu: Ndio ni shahidi wangu sababu hawajulikani hakuna anayewajua isipokua nyie

Katuga: Je ushahidi wa kwamba hawa ni mapolisi. Je, ni ushahidi au fununu tu?

Lissu: Ni ushahidi sababu hawajulikani na yeyote

Katuga: Sasa shahidi tunataka majibu sahihi ni kweli au sio kweli. Ushahidi wa kwamba baadhi ya mashahdi huenda tulikuwa nao humu ndani. JE, ni kweli, sio kweli, sio wa kuona wala kusikia?

Lissu: Sio Kweli

Katuga: Iambie mahakama kama ni kweli au sio kweli unatuhuma nyingie za kuchapisha uongo mtandaoni

Lissu: Ni kweli

Katuga: Iambie mahakama unakumbuka ulisomewa hoja za awali na ikaanza kusikilizwa

Lissu: Ndio nianakumbuka

Katuga: Unakumbuka uliposomewa hoja za wali ulisema majaji ni ma-CCM

Lissu: Sikumbuki

Katuga: Iambie mahakama hii katika hotuba yako pia ulitangaza kutokugombea kwa chama chako

Lissu: Sikumbuki, nakumbuka nilisema tutahamasisha ….

Katuga: Hapana, hukumbuki nimsekia ukijiita mwenyekiti wa Chadema. Iambie mahakama kama chama chako kilishiriki uchaguzi mwaka jana

Lissu: Hapana hakikushiriki

Katuga: Je, ni kweli kwamba uliposema mahakamani hakuendeki huna imani na mahakama

Lissu: Kwenye maswala haya ya uchaguzi sina imani na mahakama

Katuga: Kwenye zile njia ulizotuambia jana. Je, nitakuwa sahihi kwamba hukupanga kabisa kuiomba mahakama kutumia sheria

Lissu: Sikupanga kabisa

Katuga: Kwa hiyo ni sahihi kwamba swala la kupinga sheria kwa njia ya mahakama sio njia mbadala wala ya kidemokrasia

Lissu: Hapana

Katuga: Kwa hiyo kukinukisha ni njia ya kidemokrasia?

Lissu: Ndio ni njia ya kidemokrasia

Katuga: Kuhamasisha uasi ni njia ya kidemokrasia?

Lissu: Ndio ni njia ya kidemokrasia

Katuga: Uko Timamu mzee wangu

Lissu: Kimya

Katuga: Kama nilikusia ulitamka vifungu vya 55, 63, 52 kifungu cha 52 cha sheria ya habari. Ni kweli kwamba sheria ya habari iliundwa kwa ajili ya kuendesha tasnia ya habari?

Lissu: Ndio

Katuga: Kama nilikusikia vyema ulisema kuikosoa serikali sio kosa

Lissu: Nilisema kuipinga serikali sio kosa

Katuga: Kama una kanuni yako ya adhabu hapo kwa ridhaa ya mahakama hiki kifungu cha 55, yale maneno uliyotumbua, ‘ya kuzuia uchaguzi’ waambie majaji kuzuia uchaguzi ni kuipinga serikali au kuzuia uchaguzi?

Lissu: NI kuzuia uchaguzi

Katuga: Kuhamasisha uasi, kukinukisha nikupinga serikali au kupanga kuipindua serikali?

Lissu: Ni kuipinga serikali, sikuwa nazungumza habari ya serikali tulikuwa tunapanga kuzuia uchaguzi

Katuga: Unakumbuka umesema kwenye hotuba yako ulikuwa huzungumzii serikali

Lissu: Ndio sikuwa napinga serikali nilikua nazungumza habari za uchaguzi

Katuga: Kama nikikusikia vyema uliwaambia waheshimiwa hawa mashahidi wanaotoka jeshi la polisi, kasoro mmoja, wote wamejiandikia maelezo kitu ambacho ni kinyume cha sheria. Waambie majaji kama uliwatajia kifungu cha sheria na sheria yenyewe

Lissu: Sikuwaambia kifungu lakini kipo

Katuga: Unajua kwamba askari aliyemuandika shahidi maelezo na yeye ni shahidi kama huyo shahdi hata fika mahakani

Lissu: Sikumbuki

Katuga: Kama nilikusikia vyema uliiambia mahakama hii kwamba shahidi PW1 hakusema kama alivyogundua ni kosa la uhaini hakuwasiliana na ngazi za juu akiwemo DCI, kwamba ilipelelezwa vibaya

Lissu: nilisema ilipelelezwa vibaya

Katuga: Iambie mahakama kama sheria inaelekeza ukigundua kosa la uhaini lazima uwasiliane na hizo mamlaka zote, imabie mahakama kama ulitaja kifungu

Lissu: Hapana sikutaja kifungu

Katuga: Je unakumbuka ulisema kuna kutoelewana kati yako na Kingai (Kamishna wa Polisi Ramadhani Kingai ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) nchini Tanzania) pamoja na IGP Wambura (Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Camillius Wambura)

Lissu: Ni kweli nimekamatwa mara kadhaa bila kuzingatia taratibu

Katuga: Umekuwa mwanasheria muda mrefu na mwana siasa miaka 24. Je, ushawafunguliwa wawili hawa mashitaka?

Hapana: Sijawafungulia

Katuga: Kama nimekusikia vizuri uliambia mahakama hii kwamba wale mashahdi walioletwa ni mashahidi ambao walikuwa ni washitakiwa

Lissu: Nilisema walikiri kupanga uhalifu

Katuga: Je, kuna sheria inayozuia mtu aliyefanya uhalifu kuja kutoa ushahidi?

Lissu: Hapana

Katuga: Katika ushahidi wa mashahidi toka Jeshi la polisi walieleza walikamata wote

Lissu: Waliokamata waliweza kuwatambua

Katuga: Kwa ushahidi huo ina maana inawezekana kukawa na wengine

Lissu: Hawakutambuliwa au hawakukamatwa

Katuga: Nakukumbusha ile kauli yako si ndio uliambia mahakama mtu yeyote anaweza kutafsiri vyovyote vile na wale walisema wamehamasika kutokana na nini

Lissu: Maneno yangu

Katuga: Kwa hiyo nitakuwa sahihi nikisema walielewa hotuba yako na kufanyia kazi maneno yako kwa jinsi walivyoelewa

Lissu: Hapana siwezi sema sababu siwajui na siwezi kuwasemea

Katuga: Je, uliiambia mahakama hawa mashahidi ni waongo na hawastahili kuaminiwa na mahakama?

Lissu: Ndio, niliambia mahakama hawapaswi kuaminiwa wao na ushahidi wao

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Nafasi za Kazi Wezesha Mzawa Microfinance – Loan Officer, Mwisho wa Maombi Agosti 31, 2026

Next

Droo ya UEFA Champions League Msimu wa 2026/27 Kufanyika Leo Monaco

Recent Posts

  • Dili la Sh Bilioni 418! Liverpool Yafikia Makubaliano na PSG kwa Barcola
  • Droo ya UEFA Champions League Msimu wa 2026/27 Kufanyika Leo Monaco
  • Kesi ya Uhaini ya Lissu Yaendelea leo;- Maswali Mazito Yaibuka Katika Dodoso la Serikali
  • Nafasi za Kazi Wezesha Mzawa Microfinance – Loan Officer, Mwisho wa Maombi Agosti 31, 2026
  • Safari Mpya Imeanza! Fahamu Mchezo wa 3 Fisher Cats Meridianbet

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme