Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar Akutana na Araqchi Tehran

By admin
August 27, 2026 1 Min Read
Comments Off on Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar Akutana na Araqchi Tehran

Global Publishers
August 27, 2026
18 views
0 Comments

 

Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar, Mohammed bin Abdulrahman Al Thani, amekutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, mjini Tehran Alhamisi jioni, katika ziara inayofanyika wakati juhudi za kidiplomasia kuhusu hali ya Mashariki ya Kati zikiendelea.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyombo vya habari vya Iran, viongozi hao wamefanya mazungumzo, ingawa maelezo ya kina kuhusu masuala yaliyojadiliwa katika mkutano huo bado hayajawekwa wazi.

Kabla ya ziara hiyo, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei, alisema Al Thani angejadili na maafisa wa Iran mwendelezo wa juhudi za Qatar za upatanishi pamoja na masuala mengine yanayoendelea katika eneo hilo.

Ziara ya Waziri huyo wa Qatar imekuja siku mbili baada ya Kamanda wa Jeshi la Pakistan, Field Marshal Asim Munir, kufanya ziara nchini Iran.

Qatar na Pakistan ni miongoni mwa nchi zilizohusika katika juhudi za kidiplomasia za upatanishi wakati wa kusainiwa kwa hati ya makubaliano kati ya Iran na Marekani.

Hata hivyo, hadi sasa hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kuhusu matokeo ya mazungumzo kati ya Al Thani na Araqchi.

Kutokana na hali hiyo, taarifa kuhusu iwapo viongozi hao wamefikia makubaliano au kufanya maamuzi yoyote katika mkutano huo bado hazijathibitishwa rasmi.

Stori na Na: Ilankize Godfrey | GPL TUDACO

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Rais Samia Ateua na Kuhamisha Wakuu Wa Mikoa, Makatibu Tawala

Recent Posts

  • Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar Akutana na Araqchi Tehran
  • Rais Samia Ateua na Kuhamisha Wakuu Wa Mikoa, Makatibu Tawala
  • RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI NA UHAMISHO WA WAKUU WA MIKOA
  • Mavunde Ampongeza Ndejembi “Ni Kiongozi Kijana, Mwadilifu na Mzalendo” – Video
  • MWABUKUSI: KUFUKUZWA CCM KWA NCHIMBI HAKUMVUI MOJA KWA MOJA UMAKAMU WA RAIS

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme