Global Publishers
August 29, 2026
12 views
0 Comments



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepiga picha ya pamoja na viongozi wakuu wa Serikali baada ya hafla ya kumuapisha Deogratius John Ndejembi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katika picha hiyo, Rais Samia ameonekana akiwa pamoja na Makamu wa Rais Ndejembi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, pamoja na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwigulu Lameck Nchemba.
Picha hiyo imepigwa leo, Jumamosi, Agosti 29, 2026, katika Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma, mara baada ya kukamilika kwa hafla ya uapisho wa Ndejembi.

