Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

WRRB, MIKOA NA HALMASHAURI KUIMARISHA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA

By admin
August 18, 2026 2 Min Read
Comments Off on WRRB, MIKOA NA HALMASHAURI KUIMARISHA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA

 

Na Matukio Daima Media DODOMA

BODI ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imesema itaendelea kushirikiana kwa karibu na Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri nchini ili kuimarisha utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRS), kuongeza tija kwa wakulima na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, ameyasema hayo leo Agosti 18, 2026, wakati akizungumza na Maafisa Biashara katika Kikao cha Tatu cha Wizara ya Viwanda na Biashara na Maafisa Biashara, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma.

Bw. Bangu amesema utekelezaji wenye tija wa mfumo huo katika mikoa na halmashauri unahitaji ushiriki wa karibu wa Maafisa Biashara, hususan katika usimamizi wa shughuli zinazohusiana na maghala pamoja na minada ya mazao inayofanyika katika maeneo yao.

Amesema Maafisa Biashara wana nafasi muhimu katika kuhakikisha taarifa sahihi kuhusu mahitaji ya maghala katika maeneo yao zinapatikana, sambamba na kufuatilia hali, matumizi na uhitaji wa maghala katika halmashauri na mikoa ili kuwezesha Mfumo wa Stakabadhi za Ghala kutekelezwa kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano kwa Umma na Mawasiliano wa WRRB, Bw. Dionis Musseru, amesema utoaji wa elimu kwa umma umeendelea kuongeza uelewa na ushiriki wa wadau katika mfumo huo, ambapo hadi sasa mazao 11 yanauzwa kupitia WRS.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Tatoa yatishia kupaki malori | Mwananchi

Next

Mwili wa mtoto wa miaka saba wakutwa shimoni Tabora

Recent Posts

  • Serikali yatoa siku nane kwa wazalishaji saruji kushusha bei
  • Mchengerwa ataja vipaumbele sita kupunguza vifo vya mama, mtoto
  • Babu adai kupigwa ngwara na mwalimu Bahi
  • Kibwagizo cha wimbo wa ‘kilio cha mtu mzima’ kilivyotumika kesi ya ardhi
  • Mwili wa mtoto wa miaka saba wakutwa shimoni Tabora

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme