Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Mwili wa mtoto wa miaka saba wakutwa shimoni Tabora

By admin
August 18, 2026 2 Min Read
Comments Off on Mwili wa mtoto wa miaka saba wakutwa shimoni Tabora

Tabora. Mtoto Yusra Juma (7), mkazi wa Mtakuja, Kata ya Malolo, Manispaa ya Tabora, amekutwa amefariki dunia ndani ya shimo la kuchimbwa mchanga, huku Jeshi la Polisi likisema uchunguzi wa awali umebaini alinyongwa na watu ambao hawajafahamika.

Akizungumza kuhusu tukio hilo leo, Jumanne Agosti 18, 2026, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Twaha Lulengelule amesema: “Tukio hili limetokea jana majira ya saa nane mchana baada ya kutoka shuleni, tunaendelea na uchunguzi ili kuwabaini waliofanya kitendo hiki.”

Amesema mtoto huyo alikuwa mwanafunzi wa darasa la pili katika Shule ya Msingi Mawiti iliyopo Malolo Manispaa ya Tabora.



Kamanda Lulengelule amesema kifo cha mtoto huyo kilibainika baada ya bibi yake kuona muda umeenda bila kurejea nyumbani ndipo akatoka kufuatilia na hatimaye kuukuta mwili wake kwenye shimo.

Wananchi katika kata ya Malolo wakiwa eneo la tukio alipouawa mtoto Yusra.

“Ufuatiliaji wa bibi yake ndio uliosababisha kuupata mwili wa mtoto huyo mapema, uchunguzi wa madaktari unaeleza kuwa, mtoto huyo amefariki kwa kukosa hewa baada ya kushikwa shingo,” amesema.

Diwani wa Malolo, Manispaa ya Tabora, Naomi Kasanga amelaani tukio hilo akisema ni la kinyama na halikubaliki katika jamii.

Ameliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini waliohusika na tukio hilo na kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria.

“Mtoto huyu ametuumiza sana, kwanza mdogo halafu sasa hana hatia kabisa, kwa nini mtu amuue kinyama hivi,” amesema Kasanga.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Mtakuja, Hamisi Ibrahim amelaani tukio hilo akisema ni la kinyama na halivumiliki katika jamii.

Amesema mauaji hayo ni miongoni mwa matukio mabaya yanayohitaji hatua za haraka za kisheria.

“Hatupaswi kuwa na mazingira ya kuogofya kiasi hiki, lazima amani iwepo, watoto hawa ni hazina yetu lazima waishi kwa amani, kifupi tumeumizwa sana,” amesema.

Beatrice Katatula, mkazi wa Malolo amesema tukio la Yusra sio la kwanza kwa Kata ya Malolo kwa sababu miezi kadhaa nyuma alipoteza maisha mtoto mwingine katika mazingira ya kinyama.

“Mpaka tunaogopa sasa jamani maana hatuwezi kwenda na watoto kazini, na ni lazima pia waende shule, sasa kama shule njiani tena usalama hakuna, hii inatuumiza na kutuvuruga kwa kweli,” amesema.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

WRRB, MIKOA NA HALMASHAURI KUIMARISHA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA

Next

Kibwagizo cha wimbo wa ‘kilio cha mtu mzima’ kilivyotumika kesi ya ardhi

Recent Posts

  • Serikali yatoa siku nane kwa wazalishaji saruji kushusha bei
  • Mchengerwa ataja vipaumbele sita kupunguza vifo vya mama, mtoto
  • Babu adai kupigwa ngwara na mwalimu Bahi
  • Kibwagizo cha wimbo wa ‘kilio cha mtu mzima’ kilivyotumika kesi ya ardhi
  • Mwili wa mtoto wa miaka saba wakutwa shimoni Tabora

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme