Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

WATOTO 774,459 WALIO CHINI YA MIAKA 10 KUPATIWA CHANJO YA POLIO MKOANI ARUSHA.

By admin
August 18, 2026 2 Min Read
0

 

Na,Jusline Marco;Arusha

Serikali kupitia Wizara ya afya imeanza Kampeni kubwa kwaajili ya kuwakinga watoto dhidi ya Polio zoezi hilo likitekelezwa kwa awamu ya kwanza kwenye Mikoa 7 ya Arusha, Dar Es Salaam, Pwani, Tanga, Kilimanjaro, Manyara pamoja na Mara.

Hatua hiyo imekuja kufuatia kuwepo kwa visa vinavyojitokeza katika maeneo mbalimbali, vya karibuni zaidi vikitokea Mkoani Mwanza ambapo wadudu wa Polio walipatikana kwenye mfumo wa maji machafu licha ya juhudi mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali katika kupambana na ugonjwa wa kupooza kwa watoto maarufu kama Polio.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya wasimamizi wa zoezi hilo ngazi ya Mkoa na Halmashauri za Mkoa wa Arusha mapema wiki hii, Mwakilishi wa Meneja wa Mpango wa Taifa wa Chanjo Dkt. Majaliwa Mtoroki amesema walengwa katika kampeni hiyo ni watoto wote walio chini ya miaka 10.

Dkt. Mtoroki amesema mafunzo hayo ya kuwezeshana yatafanyika kwa siku mbili na baada ya hapo watatawanyika kuelekea ngazi ya Halmashauri ili kuendelea na mafunzo kwa watoaji wa chanzo, wachukua takwimu na wahamasishaji pamoja na kuandaa vikao vya kamati za msingi ngazi ya Halmashauri.

Katibu tawala Mkoa wa Arusha Dkt. Toba Nguvila akifunguaafunzo hayo kwa wasimamizi wa zoezi la Kampeni ya Chanjo dhidi ya Polio, ngazi ya Mkoa na Halmashauri za Mkoa wa Arusha, amebainisha kuwa serikali imeweka lengo la kufikiwa jumla ya watoto 774,459, zoezi litakaloendeshwa kupitia Vituo vyote vya kutolea huduma, Kliniki mkoba, shule za Msingi na kwenye ngazi ya Kaya.

Dkt. Nguvila amesisitiza umuhimu wa chanjo hiyo ya Polio, huku akibainisha kuwa chanjo hiyo pia ni suala la usalama kwani afya za watoto zikiimarika zitasaidia katika ujenzi wa Taifa bora la kesho, kuwanusuru watoto dhidi ya kupooza pamoja na kuipunguzia serikali gharama kubwa za matibabu kwa watu wenye ulemavu nchini.

 Sambamba na hayo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji wake wa zaidi ya Shilingi Bilioni 1.4 kwaajili ya uratibu wa Chanjo ya ugonjwa wa kupooza kwa watoto Chini ya miaka 10 maarufu kama Polio, na kusema kuwa ni wajibu wa kila Kiongozi na watendaji wa Mkoa wa Arusha kuhakikisha zoezi hilo linatekelezwa vyema na thamani ya fedha ionekane kwa kuhakikisha lengo la idadi ya watoto lililowekwa linafikiwa.

Mafunzo hayo ya siku mbili ambayo yamewezeshwa na wataalamu kutoka wizara ya afya yamewajumuisha Wataalamu wa afya ngazi ya Halmashauri, Waganga wakuu wa Wilaya pamoja na Maafisa Elimu ngazi ya Halmashauri.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Vyuo vikuu vinavyohitaji mfumo wa ‘Living Lab’ kwenye utafiti

Next

Mama asimulia gharama za dialisisi zilivyokuwa mzigo kwa familia – 2

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • FIFA IMEJIHARIBIA YENYEWE KWA MPANGO WA KOMBE LA DUNIA – MKUU WA LIGI KUU YA UINGEREZA
  • SERIKALI YATOA MIEZI SITA KUSAJILI MIUNDOMBINU MUHIMU YA TEHAMA
  • MAONESHO YA YST YAIBUA HAMASA YA SAYANSI KWA WANAFUNZI LINDI
  • Ebola yazidi kutikisa DR Congo, vifo vyafikia 2,378
  • ATOLEWA JIWE LA KILO 3.1 KWENYE KIBOFU

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme