Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

TBS YALENGA VIFAA BORA NA MATUMIZI SALAMA YA UMEME KUPITIA MEPS

By admin
August 18, 2026 4 Min Read
Comments Off on TBS YALENGA VIFAA BORA NA MATUMIZI SALAMA YA UMEME KUPITIA MEPS

  Na Mwandishi Wetu.

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeweka Viwango vya Chini vya Ufanisi wa Nishati (MEPS) kwa vifaa vinavyotumia umeme, hatua inayolenga kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ya nishati na kuwasaidia wananchi kupata vifaa bora na vyenye ufanisi mkubwa.

Ameyasema hayo leo Agosti 18, 2026 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Candida Shirima, wakati akifungua mafunzo kuhusu viwango vya ufanisi wa nishati na uwekaji wa alama za ufanisi kwa vifaa vya kupikia vya majumbani vinavyotumia umeme, yaliyofanyika katika Ofisi za TBS Makao Makuu, Ubungo, Dar es Salaam.

Alisema viwango hivyo vimeweka kiwango cha chini cha ufanisi ambacho vifaa vya umeme vinapaswa kufikia ili kupunguza matumizi makubwa yasiyo na tija ya umeme.

“Viwango vinawezesha ubora wa vifaa, matumizi madogo ya umeme na uwezekano wa kupunguza gharama za uendeshaji,” alisema.

Dkt. Shirima alisema matumizi bora ya nishati ni muhimu katika kupunguza gharama kwa wananchi, kulinda mazingira na kusaidia Serikali kupunguza mahitaji yasiyo ya lazima ya nishati.

Alisema TBS tayari imeandaa viwango hivyo, imejenga uwezo wa kufanya vipimo na inaendelea kusimamia udhibiti wa vifaa vinavyotumia nishati.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia wa Wizara ya Nishati, Nolasco Mlay, alisema Serikali inaendelea kuweka kipaumbele katika kuhakikisha wananchi wanapata nishati safi, salama na ya gharama nafuu kwa ajili ya kupikia.

Mlay alisema matumizi ya umeme katika kupikia (eCooking) yana nafasi kubwa katika kuongeza matumizi ya nishati safi, kutokana na kuongezeka kwa upatikanaji wa umeme nchini.

Alisema hadi sasa asilimia 28.6 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia, huku Serikali ikiendelea na juhudi za kuongeza kiwango hicho kupitia Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia wa 2024–2034.

Mlay alisema MEPS si kikwazo kwa biashara, bali ni chombo cha kuboresha ubora wa bidhaa, kulinda watumiaji na kupunguza gharama za matumizi ya umeme.

Aidha, alisema uwekaji wa lebo za ufanisi wa nishati utawawezesha wananchi kulinganisha bidhaa na kuchagua vifaa vinavyotumia umeme kwa ufanisi zaidi.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na TBS kwa kushirikiana na Modern Energy Cooking Services (MECS), chini ya ufadhili wa UKAid, yakihusisha wazalishaji, waagizaji, wasambazaji, wauzaji na wadau wengine wa vifaa vya kupikia kwa kutumia umeme.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Hichilema ashinda tena urais Zambia, Mundubile aibua shaka

Next

Tatoa yatishia kupaki malori | Mwananchi

Recent Posts

  • Serikali yatoa siku nane kwa wazalishaji saruji kushusha bei
  • Mchengerwa ataja vipaumbele sita kupunguza vifo vya mama, mtoto
  • Babu adai kupigwa ngwara na mwalimu Bahi
  • Kibwagizo cha wimbo wa ‘kilio cha mtu mzima’ kilivyotumika kesi ya ardhi
  • Mwili wa mtoto wa miaka saba wakutwa shimoni Tabora

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme