Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Michezo

Hatari iliyofichika kumrusha mtoto hewani wakati wa kumbembeleza

By admin
August 18, 2026 2 Min Read
Comments Off on Hatari iliyofichika kumrusha mtoto hewani wakati wa kumbembeleza

Dar es Salaam. Mtoto anapolia, kukosa utulivu au kutaka kucheza, wazazi na walezi hutumia njia mbalimbali kumtuliza au kumfurahisha. Baadhi humbeba na kumtikisa taratibu, huku wengine wakimrusha hewani wakiamini ni mchezo unaomfurahisha mtoto.

Akizungumza na Mwananchi hivi karibuni, Daktari bingwa wa watoto kutoka Hospitali ya Regency, Rahim Danji amesema shingo ya mtoto bado haijakomaa kikamilifu, hivyo haipaswi kupewa msukumo mkubwa au mtikisiko mkali.

Amesema shingo ina pingili zinazounganisha kichwa na sehemu nyingine ya mwili, lakini kwa watoto wadogo mifupa hiyo huwa bado katika hatua za ukuaji.



“Pingili ya kwanza ya shingo inayoshikamana na fuvu la kichwa kwa mtoto huwa bado haijakomaa vizuri. Hivyo, kumrusha mtoto hewani na kumshika kwa namna inayosababisha kichwa kutikisika kunaweza kuleta madhara,” amesema.

Mtaalamu huyo amesema kichwa cha mtoto ni kizito ikilinganishwa na mwili wake, huku misuli ya shingo ikiwa bado dhaifu. Hali hiyo humfanya mtoto awe katika hatari zaidi pale anapopigwa mtikisiko mkali au kuanguka bila kutarajiwa.

Amesema miongoni mwa madhara yanayoweza kutokea ni kuumia kwa shingo, kichwa au uti wa mgongo.

Amesema hali mbaya zaidi, mtikisiko mkali unaweza kuathiri ubongo na kusababisha majeraha makubwa, hasa iwapo mtoto ni mchanga.

Dk Gaudence Mathew kutoka Kituo cha Huduma za afya cha Decca Polyclinic kilichopo mkoani Dodoma amesema kitendo cha kumurusha mtoto hewani kinaweza kusababisha ubongo wa mtoto kutikisika na kusababisha changamoto mbalimbali ikiwamo kupata ugonjwa wa kifafa na degedege.

“Kitendo hicho pia kinaweza kumsababishia maumivu mtoto katika sehemu mbalimbali za mwili,”amesema.

Amesema mwili wa mtoto ni laini na haujakomaa, hivyo mtoto akibembelezwa kwa mtindo huo wa kurushwa na bahati mbaya akaanguka huweza kusababisa mivunjiko katika maeneo mbalimbali ya mwili na kumsababishia maumivu au hata ulemavu.

“Watoto hawatakiwi kubembelezwa kwa kutumia nguvu au kurushwa rushwa juu ni vyema mzazi kuisoma vyema saikolojia ya mtoto wake ili kufahamu pale anapolia nini hasa ni tatizo na kumbembeleza kwa taratibu na inavyoshauriwa na wataalamu,”amesema.

Mtaalamu wa malezi, Irene Mwakalinga anawashauri wazazi na walezi kuwa, mtoto anapolia ni vyema kabla ya kuanza kumbembeleza kuchunguza nini sababu ya kilio chake.

“Mtoto anapolia, mzazi anapaswa pia kutafuta sababu ya kilio hicho. Anaweza kuwa na njaa, nepi kuwa chafu, kuchoka, kuwa na joto au baridi, au kuwa anahitaji kubebwa. Kutambua hitaji lake kunaweza kusaidia kumtuliza bila kutumia nguvu,”amesema Mwakalinga.

Amesema pale inapolazimika kumbembeleza mtoto ni vyema kutumia njia salama badala ya kuwatingisha kwa nguvu au kuwarusha hewani, hatua inayoweza kuwaweka katika hatari ya kupata majeraha.

“Kumwimbia au kuzungumza naye pia ni njia inayoweza kumsaidia mtoto kutulia. Sauti anayoifahamu kutoka kwa mzazi au mlezi inaweza kumsaidia kupunguza msisimko na kumfanya ajisikie yuko katika mazingira salama,”ameeleza.

Amesema njia nyingine ni kumpapasa mgongoni kwa upole, hasa baada ya kunyonya.

Amesema mzazi anaweza kumbeba mtoto akiwa amemshikilia vizuri na kumpapasa taratibu.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Bandari ya Tanga yapaa, wadau wataka bandari kavu

Next

Sababu wanaume kuvutiwa na wanawake wenye maumbo makubwa

Recent Posts

  • Tatoa yatishia kupaki malori | Mwananchi
  • TBS YALENGA VIFAA BORA NA MATUMIZI SALAMA YA UMEME KUPITIA MEPS
  • Hichilema ashinda tena urais Zambia, Mundubile aibua shaka
  • Bado kiza kimetanda mtoto wa siku moja aliyeibwa Dareda
  • Dola ya Marekani yadhoofika, wawekezaji wakisubiri uamuzi wa Fed

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme