Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Bandari ya Tanga yapaa, wadau wataka bandari kavu

By admin
August 18, 2026 2 Min Read
Comments Off on Bandari ya Tanga yapaa, wadau wataka bandari kavu

Tanga.  Maboresho yaliyofanyika katika Bandari ya Tanga yameongeza ufanisi na kusababisha ongezeko la shehena, meli na abiria, hali iliyowafanya wadau kujadili uanzishwaji wa bandari kavu ili kupunguza msongamano na kuboresha huduma.

Maboresho hayo yanahusisha kuongeza kina cha bandari kutoka mita tatu hadi 13 pamoja na kupanua na kuboresha eneo lake, uwekezaji ulioongeza uwezo wa kuhudumia meli na shehena.

Leo Jumanne Agosti 18, 2026, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dk Batilda Burian amesema katika mwaka wa fedha 2025/26, bandari ililenga kuhudumia tani 1,643,363, lakini hadi Juni 2026 imehudumia takribani tani milioni 1.7.



Amesema pia ilipangiwa kuhudumia meli 364, lakini imehudumia 616, sawa na asilimia 196 ya lengo. Kwa abiria, amesema ililenga 59,990 na kufikia 110,356 hukju mapato, lengo lilikuwa Sh85 bilioni, lakini imekusanya Sh 138 bilioni.

Baadhi ya wadau waliokutana kwa ajili ya kujadili mpango wa bandari kavu katika bandari ya Tanga .Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dk Batilda Burian, kulia ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa TPA, Josephat Lukindo na kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TASAC Mohamed Salim. Picha na Mbonea Herman.

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Joseph Lukindo amesema kupitia Mpango Mkakati wa Miaka Mitano, Bandari ya Tanga inalenga kufikisha uwezo wa kuhudumia tani milioni 4.5 ifikapo 2030/31, sawa na ukuaji wa asilimia 19.8 kwa mwaka.

Amesema bandari kavu itasaidia kuongeza maeneo ya kuhifadhi na kusafirisha shehena nje ya bandari, kupunguza msongamano na kuongeza kasi ya mzunguko wa magari na mizigo.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Meli Tanzania (Tasac), Mohamed Salim amesema ukuaji wa shughuli za Bandari ya Tanga umeongeza mahitaji ya maeneo ya kuhifadhia shehena nje ya bandari.

Amesema maeneo hayo yanaweza kutumika kama “port extension” yakipata ridhaa ya TPA na kuendelezwa na wawekezaji.

Salim amesema Tasac imekutana na wadau Tanga kuhakikisha changamoto za msongamano zinazoshuhudiwa Dar es Salaam hazijirudii, huku akisisitiza kuwa lengo si kuwanyima wadau fursa za biashara, bali kuweka utaratibu unaoendana na ukuaji wa bandari.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

TMA yatahadharisha mvua, reli hatarini

Next

Hatari iliyofichika kumrusha mtoto hewani wakati wa kumbembeleza

Recent Posts

  • Serikali yatoa siku nane kwa wazalishaji saruji kushusha bei
  • Mchengerwa ataja vipaumbele sita kupunguza vifo vya mama, mtoto
  • Babu adai kupigwa ngwara na mwalimu Bahi
  • Kibwagizo cha wimbo wa ‘kilio cha mtu mzima’ kilivyotumika kesi ya ardhi
  • Mwili wa mtoto wa miaka saba wakutwa shimoni Tabora

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme