Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Wabunifu zaidi ya 300 kushiriki maonyesho Tanga

By admin
August 17, 2026 2 Min Read
0

Tanga. Wabunifu zaidi ya 300 kutoka maeneo mbalimbali nchini wanatarajiwa kushiriki Maonyesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yatakayofanyika kwa wiki mbili kuanzia kesho, Agosti 18, 2026, katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara mkoani Tanga.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa maonesho hayo, huku Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba akitarajiwa kuyafunga Agosti 24, 2026.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dk Batilda Burian akizungumza leo ofisini kwake jijini Tanga, amesema maandalizi ya maonyesho hayo yanaendelea vizuri na zaidi ya washiriki 300 tayari wamewasili mkoani humo na wameanza kuandaa mabanda yao.



Amesema washiriki watapata fursa ya kuonyesha bunifu, bidhaa na shughuli mbalimbali zinazohusiana na elimu, ujuzi na teknolojia.

“Maonyesho haya yanalenga pia kutoa fursa kwa wabunifu kuonyesha kazi zao, kubadilishana uzoefu na kupata fursa za kukuza bunifu zao,” amesema mkuu huyo wa mkoa.

Kwa upande wake, Kaimu Mratibu wa Kituo cha Ubunifu katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Flavian Sanga, amesema chuo hicho kitashiriki kwa kuonesha bunifu mbalimbali zinazolenga kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dk Batilda Burian akizingumza na waandishi wa habari kwenye maonesho ujuzi elimu na ubunifu katika viwanja vya shule ya sekondari Usagara jijini Tanga   

Amesema sehemu kubwa ya bunifu hizo inalenga kuboresha huduma katika sekta ya afya na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma.

Naye Shaphii Hamisi kutoka Chuo cha Uhandisi na Teknolojia cha Al-Maktoum, amesema wamewasilisha bunifu zinazolenga kusaidia kupunguza msongamano wa magari katika maeneo yenye taa za barabarani.

Amesema pia wamekuja na mfumo wa kuuza maji kwenye vioski bila kuhitaji uwepo wa muuzaji wakati wote.

Kwa mujibu wa waandaaji, maonyesho hayo yatatoa nafasi kwa wabunifu kutoka sekta mbalimbali kukutana, kujifunza kutoka kwa wenzao na kutafuta fursa za kuendeleza kazi zao.

Aidha, yanatarajiwa kuwa jukwaa la kuonesha namna elimu, ujuzi, teknolojia na ubunifu vinavyoweza kutumika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi na kuchochea maendeleo ya Taifa.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Bunge lasogezwa mbele kupisha sherehe za Maulid

Next

NAIBU WAZIRI NDERIANANGE AWATIA MOYO WENYE ULEMAVU IRINGA ATAKA WACHANHAMKIE FURSA YA MIKOPO

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • Serikali yatoa siku nane kwa wazalishaji saruji kushusha bei
  • Mchengerwa ataja vipaumbele sita kupunguza vifo vya mama, mtoto
  • Babu adai kupigwa ngwara na mwalimu Bahi
  • Kibwagizo cha wimbo wa ‘kilio cha mtu mzima’ kilivyotumika kesi ya ardhi
  • Mwili wa mtoto wa miaka saba wakutwa shimoni Tabora

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme