Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Bunge lasogezwa mbele kupisha sherehe za Maulid

By admin
August 17, 2026 2 Min Read
0

Dar es Salaam. Baada ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) kutangaza kuwa Jumanne Agosti 25 Agosti, 2026 itakuwa ni Sikukuu ya Maulid, mkutano wa nne wa Bunge umesogezwa mbele na sasa utaanza Jumatano Agosti 26.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu Agosti 17,2026 na Kitengo cha Mawasiliano na Elimu kwa Umma ya  ofisi ya Bunge, imeeleza mabadiliko hayo yamefanyika ili kutoa fursa kwa Waislam wote na Watanzania kwa ujumla kusherehekea sikukuu hiyo ambayo kitaifa itafanyika Jijini Dar es Salaam.

“Kwa mujibu wa hoja iliyotolewa bungeni na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Mwigulu  Nchemba Juni 26, 2026, mkutano wa nne wa Bunge la  13 umepangwa kuanza siku ya Jumanne Agosti , 2026.”



“ Hata hivyo, kufuatia taarifa ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) kuutangazia umma kuwa siku ya Jumanne Agosti  25 Agosti, 2026 itakuwa ni Sikukuu ya Maulid.”

“Mheshimiwa Spika kwa mamlaka yake chini ya Kanuni ya 35 (4) na (5) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, 2025 anapenda kuwataarifu Waheshimiwa wabunge na umma wote wa Tanzania, kuwa mkutano wa nne wa Bunge utaanza siku ya Jumatano Agosti 26, 2026 saa 3:00 asubuhi,”imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari leo Agosti 17, 2026, Katibu Mkuu wa Bakwata, Nuhu Mruma, amesema Maulid hayo yatasomwa usiku wa Agosti 24, katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.

Wakati Baraza la Maulid litafanyika Jumanne Agosti 25, 2026 katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC) na mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Agizo la Chalamila Stendi ya Magufuli lapingwa

Next

Wabunifu zaidi ya 300 kushiriki maonyesho Tanga

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • Serikali yatoa siku nane kwa wazalishaji saruji kushusha bei
  • Mchengerwa ataja vipaumbele sita kupunguza vifo vya mama, mtoto
  • Babu adai kupigwa ngwara na mwalimu Bahi
  • Kibwagizo cha wimbo wa ‘kilio cha mtu mzima’ kilivyotumika kesi ya ardhi
  • Mwili wa mtoto wa miaka saba wakutwa shimoni Tabora

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme