Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Subscribe
Close

Search

Habari

VETA YAANDAA MTAALA WA MAFUNZO YA MUDA MFUPI WA FANI YA RECYCLING

By admin
August 17, 2026 2 Min Read
0

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeandaa mtaala maalum wa kozi fupi za recycling kwa lengo la kuwawezesha vijana kupata ujuzi wa kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika sekta ya taka na kuongeza thamani ya taka zinazoweza kurejelewa.

Hayo yameelezwa Agosti 15, 2026 jijini Dodoma na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Hussein Mohammed Omari, wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo katika Chuo cha VETA wilaya ya Bahi.

Amesema hatua hiyo imekuja baada ya tafiti kubaini kuwa baadhi ya vijana wanaojihusisha na shughuli za taka wanakabiliwa na changamoto za kiafya na kiusalama, hivyo kuhitajika kwa mtaala mahsusi utakaowawezesha kukabiliana na mazingira ya kazi.

Dkt. Omari amesema mtaala huo umeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji ya wadau katika mnyororo wa thamani wa taka, kuanzia ukusanyaji hadi uchakataji, kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, sekta binafsi, vyuo vya walimu na waajiri.

Aidha, amesema VETA inaendelea kushirikiana na wataalamu wa sekta mbalimbali kuunganisha ujuzi wa vitendo na mafunzo ya vyuoni. Ametolea mfano ushirikiano na mtaalamu wa samani, Edo Sama, anayerejeleza zaidi ya asilimia 50 ya mbao zilizokuwa zikitupwa na kuzitumia kutengeneza samani, hivyo kuongeza thamani ya taka na kupunguza upotevu wa rasilimali.

Ameongeza kuwa VETA inaendelea kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi, ikiwemo kampuni ya Hans Paul ya Arusha inayotengeneza magari ya utalii, ili kuwawezesha wanafunzi kupata ujuzi wa vitendo. Amesema hatua hiyo inaendana na msisitizo wa Serikali wa kushirikisha sekta binafsi katika kukuza ujuzi na ajira kwa vijana.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

VETA IMETAKIWA KUENDELEA KUWASHIRIKISHA WATAALAMU WALIOBOBEA FANI MBALIMBALI

Next

SEKTA YA MADINI YAVUTIA UWEKEZAJI WA TRILIONI 9 NDANI YA MIAKA MINNE*

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • Vijana wa Mwanjelwa walivyogeuza kucha, rangi kuwa dili
  • MAGAZETINI LEO JUMATANO AGOSTI 12/2026:TANZANIA NA MAREKANI KUENDELEA KUSHIRIKIANA,RC KHERI APONGEZA UWEKEZAJI HOTELI YA GOLDEN GLOW ..
  • GIZ YAAHIDI KUTOA EURO MILIONI 39.8 KWA AJILI YA KUIMARISHA BIASHARA YA KIKANDA.
  • RC KHERI JAMES COMMENDS GOLDEN GLOW HOTEL INVESTMENT
  • MATUKIO KATIKA PICHA ZIARA YA WANAFUNZI SHULE ZA ST DOMINIC SAVIO IRINGA ,ZANZIBAR

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme