Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Subscribe
Close

Search

Habari

VETA IMETAKIWA KUENDELEA KUWASHIRIKISHA WATAALAMU WALIOBOBEA FANI MBALIMBALI

By admin
August 17, 2026 2 Min Read
0

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetakiwa kuendelea kuwashirikisha wataalamu waliobobea katika fani mbalimbali zinazotolewa vyuoni, ili kuwezesha mafunzo kwa vitendo na kujenga umahiri kwa vijana.

Rai hiyo imetolewa Agosti 15, 2026 jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Mhe. Husna Sekiboko, akisema ushirikishwaji huo utawawezesha vijana kupata ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira na jamii.

Amesema vyuo vya VETA havipaswi kujifungia kama kisiwa, wataalamu kutoka Jeshi la Zimamoto, maafisa biashara na sekta nyingine zinaweza kushirikishwa kulingana na mahitaji ya fani.

Mhe. Sekiboko ameipongeza Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutekeleza Ilani ya Uchaguzi kupitia ujenzi na uimarishaji wa vyuo vya VETA, hatua inayolenga kuwawezesha vijana kupata ujuzi na fursa za ajira na kujiajiri.

Aidha, Mwenyekiti huyo amepongeza uanzishwaji wa kampuni tanzu za VETA zinazolenga kuongeza uzalishaji wa bidhaa halisi badala ya vielelezo pekee hatua itawawezesha wanafunzi kujifunza kwa vitendo, kuongeza mapato ya vyuo na kuwajengea vijana uwezo wa kibiashara.

 

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

BAHI IMETENGA MILLION 100 KUTOKA MAPATO YAKE YA NDANI KUSAIDIA VIJANA WA WILAYA KUPATA ELIMU VETA

Next

VETA YAANDAA MTAALA WA MAFUNZO YA MUDA MFUPI WA FANI YA RECYCLING

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • FEASSA 2026 KUFANYIKA MOROGORO, WANAFUNZI 6,800 KUSHIRIKI MASHINDANO
  • Vijana wa Mwanjelwa walivyogeuza kucha, rangi kuwa dili
  • MAGAZETINI LEO JUMATANO AGOSTI 12/2026:TANZANIA NA MAREKANI KUENDELEA KUSHIRIKIANA,RC KHERI APONGEZA UWEKEZAJI HOTELI YA GOLDEN GLOW ..
  • GIZ YAAHIDI KUTOA EURO MILIONI 39.8 KWA AJILI YA KUIMARISHA BIASHARA YA KIKANDA.
  • RC KHERI JAMES COMMENDS GOLDEN GLOW HOTEL INVESTMENT

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme