Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Subscribe
Close

Search

Habari

BAHI IMETENGA MILLION 100 KUTOKA MAPATO YAKE YA NDANI KUSAIDIA VIJANA WA WILAYA KUPATA ELIMU VETA

By admin
August 17, 2026 2 Min Read
0

Halmashauri ya Wilaya ya Bahi imeonyesha mfano wa namna halmashauri zinavyoweza kutumia mapato ya ndani kuwekeza katika elimu ya Amali (ufundi na ufundi stadi) kuwaandalia vijana fursa za ajira kupitia Mfuko wa Elimu. Bahi inatenga shilingi milioni 100 kutoka mapato yake ya ndani kusaidia vijana wa wilaya hiyo kupata elimu na ujuzi katika Chuo cha Ufundi Stadi VETA Bahi.  

Hayo yameelezwa Agosti 15, 2026 na Katibu Tawala wa Wilaya ya Bahi, Mwanamvua Muyonga, wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo katika chuo cha Ufundi Stadi cha Wilaya ya Bahi.

Amesema kati ya wanafunzi 90 waliodahiliwa chuoni hapo, 45 wanalipiwa ada na halmashauri hiyo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Elimu na juhudi za kuhakikisha vijana wanapata elimu inayowawezesha kushiriki katika shughuli za kiuchumi.  

“Halmashauri yetu haiishii kwenye kulipa ada tu, tumejenga mfumo wa kuunganisha mafunzo, uwezeshaji na fursa za kiuchumi. Kupitia ushirikiano na VETA, vijana 127 wamepatiwa mafunzo ya udereva na baadaye kuwezeshwa mikopo yenye thamani ya takribani shilingi milioni 210, pamoja na kukabidhiwa pikipiki kwa ajili ya kujiajiri,” amesema DAS Muyonga.  

Ameeleza kuwa mfumo huo pia unaonekana katika mafunzo ya muda mfupi yanayotolewa kulingana na mahitaji ya jamii, ambapo vijana wa Bahi wamepatiwa mafunzo katika fani mbalimbali ikiwemo uchomeleaji na upishi. Baadhi ya waliohitimu mafunzo ya uchomeleaji wameunda vikundi na kuanza kushiriki katika shughuli za kiuchumi.  

Aidha, juhudi hizo zimeenda sambamba na kuwaunganisha vijana wenye ujuzi na fursa za manunuzi ya umma. Baadhi ya vikundi vya vijana vilivyopata mafunzo na mikopo kutoka halmashauri vimeanza kupata kazi katika miradi inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, ikiwamo ujenzi wa madarasa, uchomeleaji, utengenezaji wa milango na madirisha. Hatua hiyo imewezesha fedha zinazotengwa kurejea tena katika uchumi wa eneo kupitia shughuli za uzalishaji.  

“Halmashauri ya Wilaya ya Bahi imeendelea kuwa na ushirikiano na VETA katika kuangalia mahitaji ya vijana kabla ya kuamua aina ya mafunzo yanayohitajika. Pale inapobainika kuwa kundi la vijana linahitaji ujuzi fulani, halmashauri hushirikiana na chuo kuwezesha mafunzo hayo. Tunaweza kuona kwa vijana wetu waliohitaji mafunzo ya ulishi, chuo kiliandaa mafunzo hayo kuhakikisha vijana wanapata ujuzi katika eneo hilo,” amesisitiza Muyonga.

 

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

*WAKULIMA WA KITOMONDO WANUFAIKA NA HUDUMA YA MAWASILIANO*

Next

VETA IMETAKIWA KUENDELEA KUWASHIRIKISHA WATAALAMU WALIOBOBEA FANI MBALIMBALI

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • FEASSA 2026 KUFANYIKA MOROGORO, WANAFUNZI 6,800 KUSHIRIKI MASHINDANO
  • Vijana wa Mwanjelwa walivyogeuza kucha, rangi kuwa dili
  • MAGAZETINI LEO JUMATANO AGOSTI 12/2026:TANZANIA NA MAREKANI KUENDELEA KUSHIRIKIANA,RC KHERI APONGEZA UWEKEZAJI HOTELI YA GOLDEN GLOW ..
  • GIZ YAAHIDI KUTOA EURO MILIONI 39.8 KWA AJILI YA KUIMARISHA BIASHARA YA KIKANDA.
  • RC KHERI JAMES COMMENDS GOLDEN GLOW HOTEL INVESTMENT

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme