Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Mwenge wa uhuru wapongeza ujenzi wa wodi ya wazazi Kakola – HabariLeo

By admin
August 23, 2026 2 Min Read
Comments Off on Mwenge wa uhuru wapongeza ujenzi wa wodi ya wazazi Kakola – HabariLeo

SHINYANGA: KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, ameweka Jiwe la Msingi katika jengo la wodi ya wazazi katika Kituo cha Afya Kakola, Kata ya Bulyanhulu, Halmashauri ya Msalala, Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, lililogharimu zaidi ya Sh milioni 269.

Akisoma taarifa ya ujenzi huo kabla ya kuwekwa kwa jiwe hilo, Mganga Mfawidhi wa kituo hicho, Dk  Emanuel Boniface, amesema ujenzi ulianza rasmi Oktoba 2025 na kukamilika Julai 2026.

Amesema Serikali Kuu ilitoa Sh milioni 250 kwa ajili ya ujenzi huo, huku halmashauri ya Msalala ikitoa zaidi ya Sh milioni 19 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya kituo hicho.

Mbunge wa Jimbo la Msalala, Mabula Magangila, amesema kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, Kata ya Kakola ina takribani wakazi 51,000, ambao awali walikuwa wakitegemea zahanati kutokana na kutokuwepo kwa kituo cha afya.

Mwang’onda ameipongeza halmashauri ya Msalala kwa usimamizi mzuri wa ujenzi na wakandarasi, akisema jengo hilo limejengwa kwa kiwango kizuri.

Aidha, ameitaka halmashauri hiyo kuhakikisha miradi mingine inayotekelezwa inasimamiwa kwa umakini ili iweze kukamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyokidhi mahitaji ya wananchi.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

*DKT. MWIGULU: TUENDELEE KULIOMBEA TAIFA NA KUDUMISHA AMANI*

Next

Hull City Yaibuka na Ushindi wa Mabao 2-0 dhidi ya Manchester United

Recent Posts

  • Doumbia Bado Anajitafuta! Ashindwa Kutamba Dhidi ya Coastal
  • WANANCHI URU KUSINI WACHANGIA ZAIDI YA MILIONI 200 KUKARABATI SHULE
  • UN YAITAKA TANZANIA KUSITISHA UHAMISHAJI WA WAMASAI NGORONGORO NA LOLIONDO
  • ‘NCHIMBI SIO CHAWA’ – WARIOBA
  • TUME YA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI YAANZA UKAGUZI KWA WAKUSANYAJI NA WACHAKATAJI WA TAARIFA HIZO NCHINI.

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme