Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Michezo

Manchester United Yakamilisha dili la Carlos Baleba kwa Bilioni 253

By admin
August 22, 2026 2 Min Read
Comments Off on Manchester United Yakamilisha dili la Carlos Baleba kwa Bilioni 253

Global Publishers
August 22, 2026
414 views
0 Comments

MANCHESTER: Manchester United imefikia makubaliano ya kumsajili kiungo wa Brighton, Carlos Baleba, kwa ada ya jumla ya pauni milioni 70 sawa na  TSh bilioni 253.2.

Manchester United imekubali kulipa pauni milioni 65 pamoja na pauni milioni 5 zitakazotokana na vigezo maalum vya mkataba, huku Brighton ikikubali ofa hiyo.

Baleba, mwenye umri wa miaka 22, amekuwa akihusishwa kwa muda mrefu na uhamisho wa kwenda Old Trafford, na sasa amefanya hatua muhimu kuelekea kujiunga na kikosi cha Manchester United.

Mchezaji huyo alisafiri kwenda Manchester Ijumaa usiku kwa ajili ya vipimo vya afya, hatua ambayo inatarajiwa kutanguliwa na kusaini mkataba wake mpya.

Baleba anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka mitano, ukiwa na chaguo la kuongeza mwaka mmoja zaidi. Brighton pia imeweka kipengele cha kupata sehemu ya fedha endapo mchezaji huyo atauzwa na Manchester United hapo baadaye.

Hata hivyo, kiungo huyo kwa sasa yuko nje ya uwanja kutokana na jeraha la kifundo cha mguu alilolipata katika mchezo wa kirafiki wa maandalizi ya msimu dhidi ya Strasbourg.

Mazungumzo kati ya Manchester United na Brighton yalirejea baada ya vipimo kuonyesha kuwa jeraha hilo, alilolipata mwanzoni mwa Agosti, halikuwa kubwa kama ilivyohofiwa awali.

Baleba anatarajiwa kurejea uwanjani mwishoni mwa Septemba, huku Manchester United ikimtarajia kuongeza nguvu na ushindani katika eneo la kiungo.

Usajili huo unaongeza chaguo la kocha Michael Carrick katika eneo la kiungo, wakati Manchester United ikiendelea kujenga kikosi chenye ushindani zaidi kwa msimu mpya.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Mradi mpya kupunguza msongamano bandari ya Dar – HabariLeo

Next

NaCoNGO MKOMBOZI WA MAENDELEO MUFINDI -MAKALA

Recent Posts

  • BONANZA LA BUNGE KULENGA AFYA NA MSHIKAMANO WA WATUMISHI
  • JAMII YAHIMIZWA KUTUMIA VYAKULA VYA MIMEA ASILI KUIMARISHA KINGA ZA MWILI
  • Doumbia Bado Anajitafuta! Ashindwa Kutamba Dhidi ya Coastal
  • WANANCHI URU KUSINI WACHANGIA ZAIDI YA MILIONI 200 KUKARABATI SHULE
  • UN YAITAKA TANZANIA KUSITISHA UHAMISHAJI WA WAMASAI NGORONGORO NA LOLIONDO

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme