Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

TMA yatahadharisha mvua, reli hatarini

By admin
August 18, 2026 3 Min Read
Comments Off on TMA yatahadharisha mvua, reli hatarini

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imezitaka mamlaka zinazosimamia miundombinu ya usafiri, ikiwamo reli, kujiandaa kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua za vuli zinazotarajiwa kuwa juu ya wastani hadi wastani katika kipindi cha Oktoba hadi Desemba 2026.

TMA imesema msimu huo wa mvua unatarajiwa kuathiriwa kwa kiwango kikubwa na hali ya El -Nino yenye nguvu, huku mvua za juu ya wastani hadi wastani zikitarajiwa katika maeneo mengi ya Ukanda wa Pwani ya Kaskazini, Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki, Ukanda wa Ziwa Victoria na kaskazini mwa Mkoa wa Kigoma.

Akitoa utabiri huo leo Jumanne, Agosti 18, 2026, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk Ladislaus Chang’a amesema mvua hizo zinatarajiwa kuanza katika wiki ya nne ya Septemba na wiki ya kwanza ya Oktoba 2026 katika maeneo ya Ukanda wa Ziwa Victoria, kabla ya kusambaa taratibu katika maeneo mengine Oktoba.



Amesema vipimo vya joto la bahari katika eneo la Nino 3.4 vimefikia nyuzi joto 2.2 Agosti na vinatarajiwa kuongezeka hadi nyuzi joto 3.6 ifikapo Desemba.

Dk Chang’a, amesema hali hiyo inaweza kuongeza uwezekano wa kutokea kwa mvua kubwa zinazoambatana na upepo mkali na mafuriko katika baadhi ya maeneo, hali inayoweza kuathiri sekta mbalimbali, ikiwamo miundombinu.

Amesema reli ya mwendokasi (SGR), reli ya kawaida (MGR), barabara, madaraja na shughuli za bandari ni miongoni mwa maeneo yanayoweza kuathiriwa na mvua hizo kutokana na mmomonyoko wa udongo na mafuriko.

“Katika reli, mvua kubwa zinaweza kusababisha mmomonyoko na kusomba udongo unaoshikilia miundombinu ya reli, hali inayoweza kuharibu njia za SGR na MGR, kuchelewesha huduma za usafiri na kuongeza gharama za matengenezo,” amesema.

Kwa upande wa barabara na madaraja, TMA imeonya kuhusu uwezekano wa kingo za barabara kuporomoka, barabara kukatika na madaraja kuathiriwa na maji, jambo linaloweza kutenga maeneo na kuvuruga usafirishaji wa abiria na mizigo.

“Shughuli za bandari nazo zinaweza kukumbwa na ucheleweshaji katika upakiaji na upakuaji wa mizigo kutokana na hali mbaya ya hewa,” amesema Dk Chang’a.

Amesema katika Ukanda wa Ziwa Victoria na maeneo ya Kaskazini Magharibi, yakiwamo mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara pamoja na wilaya za Kakonko na Kibondo mkoani Kigoma, mvua zinatarajiwa kuanza kati ya wiki ya nne ya Septemba na wiki ya kwanza ya Oktoba.

Kwa mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Tanga, kaskazini mwa Morogoro, Arusha, Manyara na Kilimanjaro, mvua zinatarajiwa kuanza katika wiki ya kwanza na ya pili ya Oktoba.

Visiwa vya Unguja na Pemba navyo vinatarajiwa kuanza kupata mvua katika kipindi hicho.

“Mvua hizo zinatarajiwa kuimarika zaidi Novemba na katika baadhi ya maeneo kuendelea hadi Januari 2027, huku maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua yakitarajiwa kuanza kupata mvua mapema kuliko ilivyozoeleka,” amesema.

TMA imezitaka pia sekta nyingine kuchukua tahadhari mapema, zikiwamo kilimo, afya na mifugo, kutokana na uwezekano wa athari zinazoweza kujitokeza wakati wa msimu huo.

Akizungumzia hatua za kukabiliana na athari hizo, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi na Menejimenti ya Maafa katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Brigedia Jenerali Hosea Ndagala amesema tayari wamepokea taarifa ya TMA na wanaifanyia kazi.

“Ndiyo, nimepata taarifa ya TMA, tunaifanyia kazi. Wiki ijayo tutaeleza nini tutafanya kukabiliana na hili na wananchi wachukue tahadhari gani,” amesema.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Shekilango ilivyopata sura mpya baada ya mabasi kuondolewa

Next

Bandari ya Tanga yapaa, wadau wataka bandari kavu

Recent Posts

  • Serikali yatoa siku nane kwa wazalishaji saruji kushusha bei
  • Mchengerwa ataja vipaumbele sita kupunguza vifo vya mama, mtoto
  • Babu adai kupigwa ngwara na mwalimu Bahi
  • Kibwagizo cha wimbo wa ‘kilio cha mtu mzima’ kilivyotumika kesi ya ardhi
  • Mwili wa mtoto wa miaka saba wakutwa shimoni Tabora

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme