Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

MZOZO WA UKRAINE: URUSI YAIONYA UINGEREZA – KUNANI?

By admin
August 18, 2026 1 Min Read
Comments Off on MZOZO WA UKRAINE: URUSI YAIONYA UINGEREZA – KUNANI?

 

Urusi imeishutumu Uingereza kwa “kuchochea mzozo wa Ukraine” kufuatia uthibitisho kwamba ndege zisizo na rubani zilizotengenezwa Uingereza zilitumika kushambulizi maeneo yaliyolengwa nchini Urusi.

“Kwa kufanya hivyo, Uingereza inashiriki kama msaidizi na mhusika mwenza katika uhalifu wa umwagaji damu na mashambulizi ya kigaidi,” ilisema taarifa kutoka Ubalozi wa Urusi nchini Uingereza.

“London bila shaka italazimika kuwajibikia hatua yake,” ilisema taarifa hiyo, huku ikiongeza kuwa kadiri inavyozidi kujihusisha na mgogoro huo, “ndivyo gharama itakayolipa itakavyokuwa kubwa zaidi.”

Msemaji wa Wizara ya Ulinzi (MoD) amembia BBC kuwa Uingereza inasimama “bega kwa bega” na Ukraine.

“Urusi haipaswi kuwa na shaka yoyote kuhusu azimio la Serikali hii la kupinga uchokozi wa wake, iwe ni nchini Ukraine au dhidi ya Uingereza na washirika wetu,” alisema msemaji huyo katika taarifa.

Uingereza iliongeza kuwa “imejitolea kutoa vifaa ambavyo Ukraine inahitaji ili kujilinda dhidi ya uvamizi haramu wa [Rais wa Urusi Vladimir] Putin”.

Ndege hizo zisizo na rubani zilizotengenezwa na kampuni mbili tofauti za Uingereza zimetumika kushambulia kwa mafanikio vituo vya kijeshi na viwandandani ya Urusi, ikiwemo mitambo ya kusafisha mafuta na maghala ya kampuni ya mauzo ya mtandaoni ya Wildberries.

Ukraine imekuwa ikilenga mara kwa mara kampuni hiyo —ambayo inajulikana kama toleo la Urusi la Amazon—na kusema kuwa vituo saba kati ya 10 vikubwa zaidi vya usafirishaji na uhifadhi bidhaa vya Wildberries “vimesambaratishwa”.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

RC CHALAMILA AFANYA ZIARA YA KIMKAKATI TEMEKE

Next

DC Magoti awaahidi ajira vijana wa Mgambo Kisarawe

Recent Posts

  • MAGAZETINI LEO JUMATANO AGOSTI 19/2026,MAJI CF YAWAINUA WAJASIRIAMALI WENGI WAANZISHA WATEJA WAKIMBILIA..
  • Serikali yatoa siku nane kwa wazalishaji saruji kushusha bei
  • Mchengerwa ataja vipaumbele sita kupunguza vifo vya mama, mtoto
  • Babu adai kupigwa ngwara na mwalimu Bahi
  • Kibwagizo cha wimbo wa ‘kilio cha mtu mzima’ kilivyotumika kesi ya ardhi

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme