Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

AFISA WA POLISI NA RAIA WAWILI WAFARIKI DUNIA KATIKA VURUGU ZA LINDA MWANANCHI, KENYA

By admin
August 18, 2026 2 Min Read
Comments Off on AFISA WA POLISI NA RAIA WAWILI WAFARIKI DUNIA KATIKA VURUGU ZA LINDA MWANANCHI, KENYA

 

Afisa mmoja na raia wawili wamefariki dunia, huku wengine wkijeruhiwa kutokana na ghasia za zilizokumba mkutano wa kisiasa wa Linda Mwananchi katika eneo la Homa Bay, nchini Kenya.

Afisa huyo ambaye alipigwa jiwe kichwani alikimbizwa katika hospitali moja katika Kaunti ya Kisumu, ambako alifariki dunia alipokuwa akipokea matibabu.

Polisi imetoa taarifa na kusema kuwa washukiwa 37 wamekamatwa baada ya kupatikana na silaha mbalimbali za kienyeji, zikiwemo mapanga, kamba, vyuma, visu, marungu, fimbo za polisi na tochi.

Kukamatwa kwao ni sehemu ya operesheni inayoendelea dhidi ya wahalifu na makundi ya vijana wanaosababisha vurugu nchini humo, wakiwemo wale wanaoshukiwa kuhusika na ghasia zilizoshuhudiwa Homa Bay siku ya Jumapili.

Katika taarifa iliyotiwa saini na Msemaji wa Huduma ya Kitaifa ya Polisi (NPS), Muchiri Nyagah, alisema washukiwa hao watachukuliwa hatua za kisheria na kufikishwa mahakamani ili kujibu mashtaka yanayowakabili.

Aliongeza kuwa polisi wanamsaka Oliver Jaoko, anayejulikana kwa jina la “Olivetti,” ambaye ameelezwa kujisalimisha katika kituo cha polisi kilicho karibu ili kusaidia katika uchunguzi unaoendelea. Wakati huo huo, operesheni ya kumkamata yeye pamoja na watu wengine wote wanaoshukiwa kuhusika na vurugu hizo inaendelea.

Vurugu hizo zimezua taharuki kubwa kisiasa huku waandaaji wa vuguvugu la Linda Mwananchi wakiwatuhumu baadhi ya watu wasiotajwa majina katika siasa na usalama kwa kuhusika na kile wanachodai kuwa ni shambulio lililoratibiwa. Hata hivyo, madai hayo hayajathibitishwa kwa njia huru.

Katika taarifa iliyotolewa Jumatatu, vuguvugu hilo lilisema msafara wake ulikumbana na vizuizi barabarani kuanzia mpaka wa Kisumu na Homa Bay, kupitia barabara za Homa Bay–Migori na Migori–Kisii.

Vuguvugu hilo lilidai kuwa makundi yaliyokuwa yakishambulia msafara huo yalionekana kushirikiana na maafisa wa polisi.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Hichilema ashinda tena urais Zambia

Next

HICHILEMA ASHINDA URAIS MUHULA WA PILI ZAMBIA

Recent Posts

  • Upinzani na safari ya ujenzi wa kizazi kipya chenye ushawishi
  • NIKWAMBIE MAMA: Mkulima na mfugaji ni gego na ufizi, havitengani
  • UCHAMBUZI WA MAYALA: Elimu, ujuzi, ubunifu ndiyo msingi wa maendeleo
  • KONA YA MALOTO: Huyu ndiye Brian Mundubile, Tundu Lissu wa Zambia
  • Pilikapilika Stendi ya Magufuli, Latra yatoa kibali kwa shuttle

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme