Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

HICHILEMA ASHINDA URAIS MUHULA WA PILI ZAMBIA

By admin
August 18, 2026 2 Min Read
Comments Off on HICHILEMA ASHINDA URAIS MUHULA WA PILI ZAMBIA

 

Rais Hakainde Hichilema ametangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais wa Zambia wa mwaka 2026 baada ya kupata zaidi ya asilimia 60 ya kura zilizopigwa.

Tume ya Uchaguzi ya Zambia (ECZ) ilitangaza matokeo ya mwisho yaliyojumuishwa kutoka majimbo yote 226, yakionyesha kuwa Hichilema, wa chama cha United Party for National Development, alipata kura 2,965,326 (asilimia 60.49). Mpinzani wake mkuu, Brian Mundubile wa chama cha National Reconciliation Party for Unity and Prosperity, alipata kura 1,856,217 (asilimia 37.87). Tofauti ya kura kati ya Hichilema na mpinzani wake ni kura 1,109,109.

Jumla ya wapiga kura 8,786,300 walisajiliwa kushiriki uchaguzi huo. Wagombea wengine walikuwa nyuma sana, wakiongozwa na Harry Kalaba (Citizens First) aliyepata kura 19,070 na Kelvin Fube Bwalya (Zambia Must Prosper) aliyepata kura 17,078.

Ushindi wa Hichilema unampa muhula wa pili wa miaka mitano. Chini ya mfumo wa uchaguzi wa Zambia, mgombea anahitaji zaidi ya asilimia 50 ya kura hili kushinda katika duru ya kwanza na kuepuka duru ya pili.

Matokeo haya yanakuja baada ya mchakato uliokabiliwa na changamoto na malalamiko. Mundubile alikuwa amedai ushindi akiegemea kwenye hesabu huru za kura zilizofanywa na timu yake ya kampeni na kudai kuwepo kwa kasoro nyingi, ikiwemo tofauti kati ya matokeo ya vituo vya kupigia kura na yale yaliyotangazwa na ECZ, pamoja na madai ya kuhusika kwa jeshi katika vituo vya kujumlisha kura.

Pia aliishutumu Tanzania kwa kutuma watu kuingilia kati uchaguzi huo, madai ambayo serikali ya Tanzania iliyakanusha na kuyataja kuwa ya uongo.

Bado haijabainika ikiwa upinzani utapinga matokeo hayo ya uchaguzi.

Siku moja baada ya upigaji kura, ECZ ilisitisha kwa muda zoezi la kuhesabu na kutangaza matokeo, ikitaja ripoti za vurugu dhidi ya wafanyakazi wa uchaguzi na wizi wa karatasi za kura zilizopigwa katika baadhi ya maeneo. Kusitishwa huko kuliondolewa siku hiyo hiyo.

Waangalizi wa uchaguzi wa kikanda na kimataifa walielezea Siku ya Uchaguzi kuwa ya amani kwa kiasi kikubwa katika vituo walivyofuatilia na kuzitaka pande zote kuwa watulivu na kuheshimu mchakato rasmi. Hichilema sasa anatarajiwa kuanza muhula wake wa pili kama rais wa Zambia.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

AFISA WA POLISI NA RAIA WAWILI WAFARIKI DUNIA KATIKA VURUGU ZA LINDA MWANANCHI, KENYA

Next

RC CHALAMILA AFANYA ZIARA YA KIMKAKATI TEMEKE

Recent Posts

  • MAGAZETINI LEO JUMATANO AGOSTI 19/2026,MAJI CF YAWAINUA WAJASIRIAMALI WENGI WAANZISHA WATEJA WAKIMBILIA..
  • Serikali yatoa siku nane kwa wazalishaji saruji kushusha bei
  • Mchengerwa ataja vipaumbele sita kupunguza vifo vya mama, mtoto
  • Babu adai kupigwa ngwara na mwalimu Bahi
  • Kibwagizo cha wimbo wa ‘kilio cha mtu mzima’ kilivyotumika kesi ya ardhi

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme