Watu Wawili Wafariki Baada ya Kujinyonga Dagailoi, Babati – Video
Global Publishers
August 28, 2026
6 views
0 Comments

Watu wawili, wakazi wa Kijiji cha Dagailoi, Kata ya Sigino, Wilaya ya Babati, mkoani Manyara, wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti baada ya kujinyonga.
Tukio la kwanza lilitokea Agosti 22, 2026, ambapo mwanaume aliyefahamika kwa jina la Petro Moya anadaiwa kujinyonga baada ya kutokea mvutano kuhusu bili ya maji ya Shilingi 6,000 kati yake na mama yake mzazi.
Inadaiwa kuwa Petro alipewa fedha hizo na mama yake kwa ajili ya kulipia bili ya maji, lakini alizitumia kwa shughuli nyingine. Baada ya mama yake kumdai fedha hizo, Petro alichukua uamuzi wa kujinyonga.
Tukio la pili limetokea asubuhi ya leo, Agosti 27, 2026, ambapo mwanaume mwingine aliyefahamika kwa jina la Mohamed Abdilai amefariki dunia baada ya kujinyonga.
Inadaiwa kuwa Mohamed alichukua uamuzi huo baada ya baba yake mzazi kumtaka arejee nyumbani, kufuatia kushindwa kulipa kodi ya nyumba ya Shilingi 10,000.
Mwandishi wa Global TV, Hosea El Nino, amefika katika Kitongoji cha Dagailoi kufuatilia undani wa matukio hayo.