Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Michezo

Barcelona Yamsajili Livaković kwa Mkataba wa Miaka Minne

By admin
August 28, 2026 1 Min Read
Comments Off on Barcelona Yamsajili Livaković kwa Mkataba wa Miaka Minne

Global Publishers
August 28, 2026
60 views
0 Comments

Klabu ya Barcelona imekamilisha usajili wa kipa wa kimataifa wa Croatia, Dominik Livaković, kutoka Fenerbahçe kwa mkataba wa miaka minne utakaomuweka klabuni hapo hadi Juni 2030.

Livaković, mwenye umri wa miaka 31, amejiunga na Barcelona kwa ada ya awali ya Euro milioni 2, huku thamani ya uhamisho huo ikitarajiwa kufikia hadi Euro milioni 4 iwapo bonasi zilizowekwa kwenye makubaliano zitatimia.

Kipa huyo anaingia Barcelona akiwa na uzoefu mkubwa wa kimataifa, baada ya kutumia misimu miwili akiwa na Fenerbahçe, ambapo alicheza mechi 74 na kuweka clean sheet 24.

Mbali na uzoefu wake katika ngazi ya klabu, Livaković amekuwa sehemu muhimu ya timu ya taifa ya Croatia, akiichezea nchi hiyo katika Kombe la Dunia mara tatu pamoja na michuano miwili ya UEFA Euro.

Usajili wake unafanyika wakati Barcelona ikiendelea kufanya maboresho katika nafasi ya golini, kufuatia Marc-André ter Stegen kuondoka kwa mkopo kwenda Ajax.

Kuwasili kwa Livaković kunatarajiwa kuongeza ushindani katika nafasi ya kipa, huku Barcelona ikitarajia kutumia uzoefu wake katika mashindano ya ndani na ya kimataifa.

Kwa upande wa Livaković, uhamisho huo unampa nafasi ya kuanza ukurasa mpya katika soka la juu la Ulaya akiwa sehemu ya moja ya klabu kubwa zaidi duniani.

Stori na Haika Urio | GPL-TUDACO

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar Akutana na Araqchi Tehran

Recent Posts

  • Barcelona Yamsajili Livaković kwa Mkataba wa Miaka Minne
  • Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar Akutana na Araqchi Tehran
  • Rais Samia Ateua na Kuhamisha Wakuu Wa Mikoa, Makatibu Tawala
  • RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI NA UHAMISHO WA WAKUU WA MIKOA
  • Mavunde Ampongeza Ndejembi “Ni Kiongozi Kijana, Mwadilifu na Mzalendo” – Video

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme