Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Madiwani Tarime watakiwa kutanguliza maslahi ya wananchi

By admin
August 27, 2026 2 Min Read
Comments Off on Madiwani Tarime watakiwa kutanguliza maslahi ya wananchi

MARA: MKUU wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Gowele, amewataka madiwani na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kuhakikisha wanakuwa viongozi bora kwa kutanguliza maslahi ya wananchi na kutatua changamoto zinazowakabili katika maeneo yao.

Akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani cha kupitia taarifa ya kufunga hesabu za halmashauri kwa mwaka wa fedha 2025/2026 kilichofanyika Agosti 26, 2026, Meja Gowele, alisema viongozi wanapaswa kutumia nafasi zao kuleta maendeleo badala ya kuwa sehemu ya matatizo katika jamii.

Alisema mafanikio ya halmashauri yanategemea ushirikiano kati ya viongozi, watumishi na wananchi, huku akisisitiza umuhimu wa kuendeleza utamaduni wa kuheshimiana na kusikilizana.

Madiwani kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wakisikiliza taarifa ya kufunga hesabu za halmashauri kwa mwaka 2025/2026

“Tuwe na utamaduni wa kuheshimiana na kusikilizana. Kiongozi asikilize wananchi wake na wananchi wasikilize viongozi wao. Hii ndiyo njia ya kujenga maendeleo endelevu,” alisema Meja Gowele.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Wilaya alieleza kuwa hali ya ulinzi na usalama katika wilaya hiyo imeendelea kuimarika, lakini akawataka maafisa husika pamoja na madiwani kuendelea kushirikiana kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kudumishwa.

“Suala la ulinzi na usalama limeimarika, hivyo natamani hali hii iendelee kwa kuelimisha wananchi, kuzungumza nao na kuzuia mambo yanayoweza kuvuruga amani katika maeneo yetu,” alisema.

Vyombo vya ulinzi na uslama

Aidha, aliwataka madiwani kusimamia kwa karibu miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa katika kata zao na kuepuka vitendo vinavyoweza kuhujumu matumizi sahihi ya fedha za umma.

“Tunapokwenda katika miradi na kukukuta madiwani mmetia mkono katika ubadhirifu, tutachukua hatua bila kuangalia nafasi ya mtu. Jiepusheni na vitendo hivyo,” alionya.

Meja Gowele pia alihimiza halmashauri kuendelea kubuni na kuimarisha vyanzo vya mapato ili kuongeza uwezo wa kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kikao hicho, Matera Newland Chacha, aliwapongeza madiwani kwa kazi wanayoifanya na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya.

“Tutahakikisha tunaibua vyanzo vipya vya mapato, tunasikiliza kero za wananchi na kushiriki kikamilifu katika kutatua migogoro ili kuimarisha imani ya wananchi kwa viongozi wao,” alisema Chacha.

Pia alisisitiza umuhimu wa usimamizi madhubuti wa fedha za umma katika mwaka wa fedha 2026/2027 ili kuhakikisha mapato yatakayokusanywa yanatumika kwa miradi iliyokusudiwa na kuwanufaisha wananchi wa Tarime.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

WAZIRI MKUU DKT NCHEMBA AKIJIBU MASWALI LEO BUNGENI

Next

Mbappe Apiga Hat Trick Madrid Ikiibuka na Ushindi Mnono Dhidi ya Sociedad

Recent Posts

  • Shigongo Ahoji Serikali Kuhusu Barabara za Mitaa Nyehunge – Video
  • Dkt. Mwigulu Ampongeza Ndejembi, Aeleza Mikakati ya Serikali Kuhusu Mawasiliano na Usafiri – Vudeo
  • Tanzania yaandaa ziara ujumbe wa ADDI – HabariLeo
  • S/SGT Mongo Apewa Tuzo, Milioni 1 na Madereva wa Malori – Video
  • Mwakioja atekeleza ahadi, akabidhi pampu ya maji Lanzoni – HabariLeo

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme