Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Michezo

AFCON 2027,TANZANIA KUTANGAZA UTAMADUNI WAKE KUPITIA

By admin
August 27, 2026 2 Min Read
Comments Off on AFCON 2027,TANZANIA KUTANGAZA UTAMADUNI WAKE KUPITIA

  

Na Lilian Kasenene, Morogoro

Matukio DaimaApp

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima, amewataka Watanzania kutumia fursa ya Tanzania kuwa mwenyeji wa mashindano ya AFCON 2027 kutangaza tamaduni za makabila mbalimbali nchini.

Malima alisema hayo wakati akifungua Tamasha la Nne la Kitaifa la Utamaduni linalofanyika mjini Morogoro, ambapo jumla ya washiriki 150,000 kutoka mikoa mbalimbali wanaonyesha na kutangaza tamaduni zao.

Alisema katika mashindano ya AFCON, miongoni mwa maeneo yanayotakiwa kutangazwa ni vivutio adimu vya utalii, sambamba na kufanya vizuri katika mashindano hayo.

Malima alisema mashindano hayo yatahusisha Tanzania, Kenya na Uganda, huku Tanzania ikiwa mwenyeji wa baadhi ya michezo itakayofanyika Arusha, Dar es Salaam na Zanzibar.

Aidha, amewataka Watanzania kuendelea kuheshimu na kuthamini utamaduni wao, akisisitiza kuwa utamaduni ni sehemu muhimu ya heshima na utambulisho wa taifa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, alisema Tamasha la Kitaifa la Utamaduni lilianza mkoani Dar es Salaam, kisha kufanyika Songwe na Ruvuma, kabla ya mwaka huu kufanyika Morogoro.

Akizungumzia maandalizi ya AFCON 2027, Msigwa aliwataka Watanzania kupuuza taarifa zisizo za kweli zinazoenezwa na baadhi ya watu kuhusu Tanzania kuondolewa kwenye uenyeji wa mashindano hayo.

Alisema taarifa hizo si za kweli na kwamba maandalizi ya mashindano hayo yanaendelea kwa ushirikiano wa Tanzania, Kenya na Uganda.

Baada ya ufunguzi wa tamasha hilo, kulifanyika Mdahalo wa Kitaifa kuhusu Maadili uliolenga kuhamasisha na kuchochea maadili mema kwa Watanzania.

Mdahalo huo ulifanyika katika eneo la Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), ambapo watoa mada walisisitiza umuhimu wa Watanzania kuwa kioo bora cha jamii kwa kuonyesha mfano mwema.

Wamesema maadili ni msingi wa utu, umoja na mshikamano wa kitaifa, hivyo Watanzania wanapaswa kuwa mfano bora kwa watoto na jamii kwa ujumla, kuipenda Tanzania kwa vitendo, kuheshimu utu na kujenga taifa lenye amani na mshikamano.

Maadili mema yameelezwa kuwa ni sehemu muhimu ya utambulisho wa Watanzania.

Mwisho.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

VIGOGO WATANO WA CCM WALIIOONDOKA KATIKA NYADHIFA ZAO CHINI YA RAIS SAMIA

Next

MBALI YA DKT NCHIMBI ,WANACHAMA HAWA PIA WALIWAHI KUFUKUZWA CCM

Recent Posts

  • Shigongo Ahoji Serikali Kuhusu Barabara za Mitaa Nyehunge – Video
  • Dkt. Mwigulu Ampongeza Ndejembi, Aeleza Mikakati ya Serikali Kuhusu Mawasiliano na Usafiri – Vudeo
  • Tanzania yaandaa ziara ujumbe wa ADDI – HabariLeo
  • S/SGT Mongo Apewa Tuzo, Milioni 1 na Madereva wa Malori – Video
  • Mwakioja atekeleza ahadi, akabidhi pampu ya maji Lanzoni – HabariLeo

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme