Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Wanafunzi 1,700 Bagaza wafaidika msaada wa mahindi, sukari – HabariLeo

By admin
August 26, 2026 2 Min Read
Comments Off on Wanafunzi 1,700 Bagaza wafaidika msaada wa mahindi, sukari – HabariLeo

GEITA: TAASISI ya Mapung’o Foundation imetoa msaada wa magunia 30 ya mahindi na kilo 250 za sukari kwa Shule ya Msingi Bagaza iliyopo Kata ya Butobela wilayani Geita.

Msaada huo unalenga kusaidia upatikanaji wa uji shuleni hapo kwa wanafunzi zaidi ya 1,700 na kuwatengenezea mazingira bora ya kujifunzia ili kuunga mkono juhudi za serikali za kuinua kiwango cha elimu na ufaulu.

Mratibu wa Mapung’o Foundation, Marco Victor amekabidhi msaada huo kwa niaba ya taasisi na kueleza kuwa taasisi hiyo imejizatiti kusaidia mahitaji ya wanafunzi kwa manufaa ya jamii.

Ofisa Elimu wa Kata ya Butobela, John Otieno amekiri kuwa msaada huo utasaidia kuinua kiwango cha elimu na kuleta ahueni ya michango ya chakula kwa wazazi.

Otieno amewaomba wadau wengine kuiga mfano wa Mapung’o Foundation kwa kujitolea kuchangia vyakula mashuleni, akieleza kuwa hatua hiyo inaimarisha afya na maendeleo ya elimu kwa watoto.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Bagaza, Damasi Madata, amesema shule hiyo hutumia debe tatu za mahindi kwa siku kwa ajili ya uji hivo magunia 30 ya mahindi pamoja na kilo 250 za sukari vitasaidia kwa kiasi kikubwa kuendesha programu ya lishe shuleni.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

WAFANYABIASHARA WA LIBRARY ZA VIDEO IRINGA WATISHIA KUTOFANYA KAZI NA UMOJA MOVIES

Next

TRA United yaanza maandalizi kuivaa Dodoma Jiji FC – HabariLeo

Recent Posts

  • BONANZA LA BUNGE KULENGA AFYA NA MSHIKAMANO WA WATUMISHI
  • JAMII YAHIMIZWA KUTUMIA VYAKULA VYA MIMEA ASILI KUIMARISHA KINGA ZA MWILI
  • Doumbia Bado Anajitafuta! Ashindwa Kutamba Dhidi ya Coastal
  • WANANCHI URU KUSINI WACHANGIA ZAIDI YA MILIONI 200 KUKARABATI SHULE
  • UN YAITAKA TANZANIA KUSITISHA UHAMISHAJI WA WAMASAI NGORONGORO NA LOLIONDO

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme