Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
  • Home
  • Privacy Policy
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Ray Kigosi Atoa Siri ya Familia, Chuchu Hansy Atarajia Mtoto wa Pili – Video

By admin
August 21, 2026 1 Min Read
Comments Off on Ray Kigosi Atoa Siri ya Familia, Chuchu Hansy Atarajia Mtoto wa Pili – Video

Global Publishers
August 21, 2026
420 views
0 Comments

Mwigizaji mkongwe wa filamu Bongo, Vincent Kigosi, maarufu kama Ray, amefichua kuwa mzazi mwenzake, Chuchu Hansy, anatarajia kupata mtoto wao wa pili.

Ray ametoa taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram, akieleza furaha na shukrani alizonazo moyoni kutokana na ujio wa mtoto huyo, huku akimshukuru Mungu kwa baraka hiyo katika familia yao.

Katika ujumbe wake, Ray ameandika:
“MY LOVELY MZUNGU, maneno hayatoshi kueleza furaha na shukrani nilizonazo moyoni. Unakaribia kunipa zawadi ya thamani kuliko zote, mtoto wetu wa pili.

Namshukuru Mungu kwa ajili yako na kwa baraka hii kubwa katika familia yetu.

Asante kwa upendo wako na kwa kunipa furaha isiyo na kipimo. Nakupenda sana MY LOVELY MZUNGU. Mungu ailinde familia yetu na abariki familia yetu daima.

Nakuahidi kuthamini familia yetu, kukupenda sana na kusimama na wewe katika kila hatua ya maisha yetu.”

Ray pia ametumia ujumbe huo kuwashukuru watu mbalimbali waliohusika katika maandalizi ya picha zao, huku akiwataja wauzaji wa mavazi pamoja na mpiga picha.

Ujio wa mtoto huyo unakuwa hatua nyingine katika maisha ya familia ya Ray na Chuchu Hansy, huku mashabiki wao wakituma pongezi na kuwatakia safari njema kuelekea kumpokea mtoto wao wa pili.

Ray ni miongoni mwa waigizaji waliodumu kwa muda mrefu katika tasnia ya filamu Tanzania na amejijengea jina kubwa kupitia kazi zake mbalimbali katika Bongo Movies.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Lissu Aanza Kujitetea Kesi ya Uhaini, Ushahidi Waahirishwa hadi Jumatatu

Next

Luizer ampongeza Asha Baraka – HabariLeo

Recent Posts

  • Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar Akutana na Araqchi Tehran
  • Rais Samia Ateua na Kuhamisha Wakuu Wa Mikoa, Makatibu Tawala
  • RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI NA UHAMISHO WA WAKUU WA MIKOA
  • Mavunde Ampongeza Ndejembi “Ni Kiongozi Kijana, Mwadilifu na Mzalendo” – Video
  • MWABUKUSI: KUFUKUZWA CCM KWA NCHIMBI HAKUMVUI MOJA KWA MOJA UMAKAMU WA RAIS

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Burudani
  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
  • Siasa
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme