Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Wafugaji walalamikia operesheni za usiku, Serikali yajibu

By admin
August 18, 2026 2 Min Read
Comments Off on Wafugaji walalamikia operesheni za usiku, Serikali yajibu

Dar es Salaam. Baadhi ya wakulima na wafugaji wa Wilaya ya Liwale, Mkoa wa Lindi, wamelalamikia kile walichodai kuwa ni uvamizi wa makazi yao nyakati za usiku na mamlaka za ulinzi na usalama, wakisema mifugo yao imekuwa ikichukuliwa na kudaiwa fedha ili irejeshwe.

Malalamiko hayo yametolewa leo Jumanne, Agosti 18, 2026 na wawakilishi wa wakulima na wafugaji hao walipokutana na wanahabari katika ofisi kuu za Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, Serikali ya Mkoa wa Lindi imesema wakulima na wafugaji wanapaswa kuzingatia sheria kwa kufanya shughuli zao katika maeneo yaliyotengwa, ikisisitiza kuwa wasioweza kufuata utaratibu huo watahitajika kutafuta maeneo mengine.



Akizungumzia malalamiko hayo, Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Lindi ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa huo, Zainab Telack amesema Serikali imetenga maeneo maalumu kwa shughuli za kilimo na ufugaji.

“Nimekuwa nikishughulikia suala hili kwa karibu sana. Hata jana nilikuwa na kikao na viongozi wa wakulima na wafugaji na tumekubaliana mambo mengi. Tumeteua maeneo ya wafugaji na wakulima, lakini hawataki kuhamia,” amesema.

Amesema katika maeneo hayo, wakulima na wafugaji wanatakiwa kulipia kiasi kilichowekwa na kujenga miundombinu kwa ajili ya shughuli zao.

“Tumetenga vitalu vingi kwa wafugaji na wakulima, lakini mpaka sasa waliohamia hawazidi 50. Nitoe wito, anayeona hawezi kufuata sheria aondoke Lindi,” amesema.

Telack amesema eneo lililotengwa kwa wafugaji litumike kwa ufugaji na lile la kilimo litumike kwa kilimo, huku akisema Serikali itaendelea kufanya operesheni za ukaguzi.

Amesema pia wananchi wenye malalamiko wanapaswa kufikisha kero zao katika ofisi yake ili zipatiwe ufumbuzi.

Mmoja wa wawakilishi wa wafugaji kutoka Kijiji cha Milui, Kata ya Milui, Juma Msafiri, amesema wafugaji wamekuwa wakikabiliwa na vitendo wanavyodai ni vya manyanyaso, ikiwamo kuvamiwa nyakati za usiku.

“Sisi wafugaji tunaiomba Serikali na wadau wote watusikilize. Wafugaji tunadhulumiwa, tunavamiwa na askari na vijana wanaolipwa kutozwa fedha mara kwa mara, hasa usiku wa manane,” amesema.

James Maley, anayefanya shughuli za ufugaji na kilimo, amesema hali hiyo imekuwa tishio kwa usalama wa wananchi, akidai baadhi ya watu huenda kwa wafugaji usiku na kuwataka walipe fedha ili mifugo yao isichukuliwe.

Amedai baadhi ya vijana hutumwa kutafuta maeneo yenye mifugo na baadaye huambatana na polisi kuwakamata wafugaji.

Kaimu Katibu Mkuu wa Chaumma, Benson Kigaila amesema chama hicho kilibaini malalamiko kama hayo katika ziara yake mkoani Lindi, ikiwamo Liwale, Luangwa na Kilwa.

Amesema chama hicho kimeiandikia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuiomba iingilie kati suala hilo.

Kigaila amesema baadhi ya wafugaji wamepewa maeneo ambayo wanatakiwa kulipia Sh5.8 milioni na kujenga miundombinu, ikiwamo mabwawa ya maji na maeneo ya malisho.

Amesema gharama hizo zimekuwa mzigo kwa baadhi ya wafugaji, hali inayowafanya washindwe kuhamia maeneo yaliyotengwa na kuendelea kukumbwa na changamoto.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Tanzania, DR Congo kuimarisha ushirikiano, kuondoa vikwazo

Next

Dola ya Marekani yadhoofika, wawekezaji wakisubiri uamuzi wa Fed

Recent Posts

  • TBS YALENGA VIFAA BORA NA MATUMIZI SALAMA YA UMEME KUPITIA MEPS
  • Hichilema ashinda tena urais Zambia, Mundubile aibua shaka
  • Bado kiza kimetanda mtoto wa siku moja aliyeibwa Dareda
  • Dola ya Marekani yadhoofika, wawekezaji wakisubiri uamuzi wa Fed
  • Wafugaji walalamikia operesheni za usiku, Serikali yajibu

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme