Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Madeleka aeleza namna alivyokamatwa Mahakama Kuu

By admin
August 18, 2026 2 Min Read
Comments Off on Madeleka aeleza namna alivyokamatwa Mahakama Kuu

Dar es Salaam. Siku moja baada ya Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kumwachia kwa dhamana, Wakili Peter Madeleka ameeleza namna alivyokamatwa katika viunga vya Mahakama Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi eneo la Mikocheni.

Madeleka alikamatwa Agosti 14, 2026 na kushikiliwa kwa siku tatu katika Kituo Kikuu cha Polisi, Dar es Salaam kwa tuhuma za kudharau amri za Mahakama Kuu zilizotolewa Julai 17 na Agosti 13, 2026.

Akizungumza leo Jumanne, Agosti 18, katika ofisi za Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Madeleka amesema alikamatwa akiwa anatimiza majukumu yake ya kikazi mahakamani.



“Walinikamata baada ya kujitambulisha kuwa ni askari wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na walinitaka niambatane nao. Nilipowaambia kuwa nipo mahakamani kuna kesi inaendelea; na kuwaomba niambatane nao hadi kwa jaji kutoa taarifa, walikataa,” amesema wakili Madeleka.

Amesema alipelekwa katika ofisi ya Naibu Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu na kuambiwa tuhuma zinazomkabili ni kudharau Mahakama.

Madeleka amesema baada ya kuelezwa tuhuma hizo, alipewa fursa ya kuwasiliana na familia na mawakili wake, ambao walihakikisha anapata dhamana.

Amesema alikaa mahabusu kwa saa kadhaa kabla ya kuhamishiwa kituo kingine usiku akiwa chini ya ulinzi, na Agosti 15 kurejeshwa Kituo Kikuu cha Polisi.

Wakili Peter Madeleka akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Agosti 18, 2026 katika ofisi za Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) aliyekaa kushoto ni Wakili Maduhu William. Picha na Sute Kamwelwe.

Kuhusu amri inayodaiwa kuidharau, Madeleka amesema hana taarifa kuhusu amri hiyo wala hakumbuki kama Mahakama ilitoa amri yoyote Agosti 13, 2026.

Amesema kifungu cha 114 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu (Sura ya 16) kinaeleza hatua zinazopaswa kuchukuliwa kwa mtu anayekiuka amri ya Mahakama.

Hata hivyo, Wakili Madeleka amewashukuru polisi kwa kufanya uchunguzi kuhusu tuhuma hizo, akisema unaweza kusaidia kufikisha suala hilo mahakamani ili sheria ipate nafasi ya kutafsiriwa.

“Namuomba Mkurugenzi wa Mashtaka anipeleke mahakamani ili kukuza sheria yetu,” amesema Wakili Madeleka.

Amesema hajawahi kumdharau jaji au hakimu wala kufikishwa katika kamati ya maadili na kutiwa hatiani kwa kosa hilo.

Hivyo, amesema haoni kama amewadharau majaji, akisema anatambua maadili ya taaluma yake na mamlaka ya mhimili wa Mahakama.

“Kesi hii ni nzuri sana ambayo wananchi wanapaswa kuifuatilia kwa ukaribu, kwanza katika macho ya sheria, je, kesi ya kudharau Mahakama inapelelezwaje na polisi?” amehoji.

Akizungumzia hilo, Wakili William Maduhu amesema walihangaika usiku na mchana kwa siku tatu kuhakikisha Madeleka anaachiwa, huku akisema iwapo kuna kesi dhidi yake, wanaamini itapelekwa mahakamani.

Jumatatu Agosti 17, Wakili wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Paul Kisabo alisema Madeleka alipewa dhamana na kutakiwa kuripoti kituoni kwa siku alizopangiwa na polisi.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Makosa matatu yasababisha daladala 203 kufungiwa VTS

Next

Watano wafariki dunia akiwamo mtoto mchanga, wanane wajeruhiwa Lushoto

Recent Posts

  • WRRB, MIKOA NA HALMASHAURI KUIMARISHA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA
  • Tatoa yatishia kupaki malori | Mwananchi
  • TBS YALENGA VIFAA BORA NA MATUMIZI SALAMA YA UMEME KUPITIA MEPS
  • Hichilema ashinda tena urais Zambia, Mundubile aibua shaka
  • Bado kiza kimetanda mtoto wa siku moja aliyeibwa Dareda

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme