Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

KANISA LA EBENEZER MBALIZI LAGEUKA FARAJA KWA WAZEE WASIOJIWEZA

By admin
August 18, 2026 2 Min Read
Comments Off on KANISA LA EBENEZER MBALIZI LAGEUKA FARAJA KWA WAZEE WASIOJIWEZA

Na Josea Sinkala, Mbeya.

Kanisa la Ebenezer Assemblies of God Africa (EAGA) lenye makao yake makuu mjini Mbalizi wilayani Mbeya, limewagusa wahitaji ambao ni wazee wasiojoweza ndani na nje ya Kanisa hilo kwa kuwasaidia mahitaji ya vyakula.

Mahitaji yaliyotolewa kwa familia tano za wazee hao ni mahindi, maharage, sabuni na fedha kwa ajili ya kujikimu jambo ambalo limeonekana bayana kuwa la mfano kwa Kanisa na jamii kwa ujumla kutokana na kugusa maisha ya wananchi kwa ujumla ikizingatiwa msaada kama huo kwa jamii sio mara ya kwanza kufanywa na Kanisa hilo.

Akizungumza kwenye kilele cha ibada iliyofanyika jumapili iliyopita (Agosti 16, 2026) kanisani Ebenezer, Askofu mkuu wa Kanisa la Ebenezer Assemblies of God Africa Mchungaji Peter Jackson Hasunga anayechunga Kanisa hilo la Mbalizi alisema ameamua kwa kushirikiana na wazee wa Kanisa na waumini kwa ujumla kuwa na sadaka kwa ajili ya kusaidia wasiojiweza kama MUNGU alivyoagiza kuwajali wahitaji na wasiojiweza kwenye shida zao.

Askofu Hasunga aliwataka watu wengine kwenye Kanisa na jamii hasa wenye uwezo kiuchumi kujitoa kusaidia wasiojiweza na yatima ili kushiriki nao katika adha na magumu wanayokumbana nayo.

Wanufaika wa msaada huo walitumia ibada hiyo kumshukuru MUNGU kwa Mchungaji wao kiongozi Peter Hasunga na viongozi wengine kanisani hapo kwa kuwa na moyo wanaosema ni wa kujali na upendo kwa wananchi kwa ujumla.

Awali akihubiri kwenye ibada hiyo, Askofu mkuu wa Kanisa la EAGA aliwataka waumini hao kumwishia MUNGU na kuwa na maisha ya utakatifu na uaminifu ili kutoandamwa na laana za Shetani ikiwemo kuhakikisha wanakuwa waaminifu kwenye sadaka ya fungu la kumi.

Kanisa la YESU kwa ujumla linapaswa kuwa mfano mwema kuanzia ndani ya Kanisa kwa kuwa na kudumisha maisha ya utakatifu na upendo na baadaye hata nje ya Kanisa yaani katika jamii kuhakikisha Kanisa hilo linakuwa majibu na faraja kwa wananchi kama ambavyo Kanisa la Ebenezer Assemblies of God Africa EAGA Mbalizi limefanya kwa kutoa mahitaji kwa familia za wazee wasiojiweza.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Sababu wanaume kuvutiwa na wanawake wenye maumbo makubwa

Next

Wazazi sita ‘wabanwa’ kwa watoto kutokwenda shule

Recent Posts

  • Wafugaji walalamikia operesheni za usiku, Serikali yajibu
  • Tanzania, DR Congo kuimarisha ushirikiano, kuondoa vikwazo
  • Watano wafariki dunia akiwamo mtoto mchanga, wanane wajeruhiwa Lushoto
  • Madeleka aeleza namna alivyokamatwa Mahakama Kuu
  • Makosa matatu yasababisha daladala 203 kufungiwa VTS

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme