Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Subscribe
Close

Search

Habari

UPANUZI UWANJA WA NDEGE SINGIDA WAANZA KWA FIDIA

By admin
August 17, 2026 2 Min Read
0

‎

‎Elisante John, Singida,

‎‎Hatua ya Serikali kupanua Uwanja wa Ndege wa Singida imeibua ombi kutoka kwa wananchi, kuondolewa kwenye maeneo yao, wakiomba thamani ya ardhi inayotumika katika fidia, ipandishwe kutoka Sh. 8,000 hadi Sh.10,000, kwa mita ya mraba.

‎‎Mthamini wa Ardhi Mkoa wa Singida, Zablon Mwalyasi, amesema upanuzi huo unahusisha kuongeza ekari 316.6 kutoka maeneo ya wananchi yaliyo pembezoni mwa uwanja. Amesema lengo ni kuboresha huduma za usafiri wa anga, kwa kuwa uwanja uliopo hautoshelezi mahitaji ya sasa.

‎Mwalyasi amesema kila mwananchi atakayepitiwa na zoezi hilo atalipwa fidia kwa kuzingatia thamani halisi ya ardhi na mali zilizopo. Amesema mali hizo ni pamoja na majengo, miti na maendeleo mengine yanayotambuliwa kisheria.

‎‎Ameongeza kuwa wananchi watastahili pia posho mbalimbali, ikiwamo ya usumbufu, makazi, upangaji na gharama za kuhamisha mali. Amewataka wananchi kuwa wazi wakati wa uthamini na kuwaruhusu wataalamu kukagua mali zote ili kuhakikisha thamani halisi inapatikana.

‎Baadhi ya wananchi, akiwamo Charles Rwegoshora, Shabani Nyuda, Karani Kisuke, Hassan Irunde na Diwani wa Kata ya Mandewa, Yusufu Makera, wameomba thamani hiyo ipandishwe kutoka Sh. 8,000 hadi Sh10,000, kwa mita ya mraba. Mwalyasi amesema atalifikisha ombi hilo kwa mamlaka husika kwa ajili ya uamuzi.

‎‎Kwa upande wake, mwakilishi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Singida, Bornege Tatwebwa, amesema upanuzi wa uwanja huo utaongeza fursa za usafiri wa anga na kuchochea maendeleo ya kiuchumi. Pia amewapongeza wananchi kwa ushirikiano wanaouonesha katika kuunga mkono zoezi hilo.

‎

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

NAIBU WAZIRI NISHATI AHAMASISHA UMMA KUPATA TAARIFA SAHIHI KUHUSU SEKTA DOGO YA UMEME

Next

SERIKALI YAZIDI KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA KWA WANANCHI MTWARA

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • Wabunifu zaidi ya 300 kushiriki maonyesho Tanga
  • Bunge lasogezwa mbele kupisha sherehe za Maulid
  • Agizo la Chalamila Stendi ya Magufuli lapingwa
  • TRA Songwe kuanzisha klabu za kodi shule za sekondari
  • GLOBAL EDUCATION LINK YAPELEKA WANAFUNZI 198 CHINA NA 189 INDIA

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme