16 mbaroni kwa tuhuma za kuchoma moto shamba, matrekta ya mwekezaji
Babati. Wakazi 16 wa Kijiji cha Kiru, wilayani Babati, Mkoa wa Manyara, wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuvamia eneo la mwekezaji wa Dudumera Estate na kuchoma moto shamba pamoja na matrekta matatu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Ahmed Makarani, amethibitisha kushikiliwa kwa watu hao na kusema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Babati leo Jumatatu, Agosti 17, 2026, Makarani amesema tukio hilo lilitokea Agosti 15, 2026, katika Kijiji cha Kiru.
“Tunaendelea kuwashikilia watu 16 kwa tuhuma hizo na uchunguzi ukikamilika, hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa,” amesema kamanda huyo.
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya usalama ya Wilaya ya Babati mkoani Manyara, wakikagua maeneo ya kampuni ya Dudumera Estate yaliyochomwa moto na baadhi ya wakazi wa kijiji cha Kiru wilayani Babati mkoani Manyara. Picha na Joseph Lyimo
Amesema watuhumiwa hao wanadaiwa kushiriki kuchoma mali mbalimbali, zikiwamo shamba na matrekta matatu.
Kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Babati, ikiongozwa na katibu tawala wa wilaya hiyo, Thobias Abwaro, leo imefika eneo la tukio na kujionea madhara yaliyosababishwa na moto huo.
Hata hivyo, Abwaro amelipongeza Jeshi la Polisi kwa hatua ya kuwakamata watu hao huku akisema Serikali inaendelea kuchukua hatua nyingine zaidi kuhusu tukio hilo.
“Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Agosti 15, 2026, baada ya kundi la watu kudaiwa kuvamia eneo la mwekezaji huyo na kuchoma moto shamba lenye ukubwa wa takribani hekta 15,” amesema na kuongeza kuwa shamba hilo lilikuwa likilimwa miwa na mtama.
Kwa mujibu wa Abwaro, chanzo kinachodaiwa kusababisha tukio hilo ni mgogoro wa ardhi uliodumu kwa muda mrefu kati ya wananchi wa eneo hilo na mwekezaji, licha ya jitihada za viongozi wa Serikali za kutafuta suluhisho kufanyika.
Mwekezaji wa Dudumera Estate, Radhika Jeta, amesema tukio hilo limemsababishia hasara kubwa kutokana na uharibifu wa mali na kuvurugika kwa shughuli za uzalishaji shambani.
Amesema matrekta matatu yameteketea pamoja na mashamba yaliyokuwa yamepandwa miwa na mtama.
“Nimesikitishwa na tukio hilo la uchomaji moto, kwani mara nyingi tumekuwa tukishirikiana na wananchi na viongozi wa eneo hili. Mimi huwa nashiriki kutoa michango mbalimbali ya maendeleo,” amesema Jeta.
Akizungumzia tukio hilo, mlinzi wa eneo hilo, Hussein Twabatari, amesema usiku wa tukio alishtushwa na kundi la watu waliobeba silaha za jadi lililovamia eneo hilo.
Amesema alihofia usalama wake kutokana na namna uvamizi huo ulivyofanyika.
Wakati huohuo, tukio hilo limeathiri pia huduma ya umeme katika baadhi ya maeneo ya Tarafa ya Mbugwe.
Ofisa Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Manyara, Samuel Mandari, amesema watu wasiojulikana walichoma nguzo ya umeme na kusababisha baadhi ya maeneo kukosa huduma hiyo.
“Watu wasiojulikana wamechoma nguzo ya Tanesco na tukio hilo limesababisha hasara kwa shirika, na wakazi wa maeneo ya Magugu na jirani wamekosa huduma ya umeme,” amesema Mandari.Akizungumza na waandishi wa habari mjini Babati leo Jumatatu Agosti 17, 2026, Makarani amesema tukio hilo lilitokea Agosti 15, 2026 katika Kijiji cha Kiru.
Shamba la miwa la kampuni ya Dudumera Estate lililochomwa moto na baadhi ya wakazi wa kijiji cha Kiru wilayani Babati mkoani Manyara. Picha na Joseph Lyimo
“Tunaendeleo kuwashikilia watu 16 kwa tuhuma hizo na uchunguzi ukikamilika hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa,” amesema kamanda huyo.
Amesema watuhumiwa hao wanadaiwa kushiriki kuchoma mali mbalimbali, zikiwamo shamba na matrekta matatu.
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Babati, ikiongozwa na Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Thobias Abwaro, leo imefika eneo la tukio na kujionea madhara yaliyosababishwa na moto huo.
Hata hivyo, Abwaro amelipongeza Jeshi la Polisi kwa hatua ya kuwakamata watu hao huku akisema Serikali inaendelea kuchukua hatua nyingine zaidi kuhusu tukio hilo.
“Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Agosti 15, 2026 baada ya kundi la watu kudaiwa kuvamia eneo la mwekezaji huyo na kuchoma moto shamba lenye ukubwa wa takribani hekta 15,” amesema na kuongeza kuwa shamba hilo lilikuwa likilimwa miwa na mtama.
Kwa mujibu wa Abwaro, chanzo kinachodaiwa kusababisha tukio hilo ni mgogoro wa ardhi uliodumu kwa muda mrefu kati ya wananchi wa eneo hilo na mwekezaji, licha ya jitihada za viongozi wa Serikali za kutafuta suluhisho kufanyika.
Mwekezaji wa Dudumera Estate, Radhika Jeta amesema tukio hilo limemsababishia hasara kubwa kutokana na uharibifu wa mali na kuvurugika kwa shughuli za uzalishaji shambani.
Matrekta ya kampuni ya Dudumera Estate yaliyochomwa na baadhi ya wakazi wa kijiji cha Kiru wilayani Babati mkoani Manyara. Picha na Joseph Lyimo
Amesema matrekta matatu yameteketea pamoja na mashamba yaliyokuwa yamepandwa miwa na mtama.
“Nimesikitishwa na tukio hilo la uchomaji moto kwani mara nyingi tumekuwa tukishirikiana na wananchi na viongozi wa eneo hili, mimi huwa nashiriki kutoa michango mbalimbali ya maendeleo,” amesema Jeta.
Alizungumzia tukio hilo, mlinzi wa eneo hilo, Hussein Twabatari amesema usiku wa tukio alishtushwa na kundi la watu waliobeba silaha za jadi lililovamia eneo hilo.
Amesema alihofia usalama wake kutokana na namna uvamizi huo ulivyofanyika.
Wakati huohuo, tukio hilo limeathiri pia huduma ya umeme katika baadhi ya maeneo ya Tarafa ya Mbugwe.
Ofisa Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Manyara, Samuel Mandari amesema watu wasiojulikana walichoma nguzo ya umeme na kusababisha baadhi ya maeneo kukosa huduma hiyo.
“Watu wasiojulikana wamechoma nguzo ya Tanesco na tukio hilo limesababisha hasara kwa shirika na wakazi wa maeneo ya Magugu na jirani wamekosa huduma ya umeme,” amesema Mandari.

