Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Jose Chameleone alivyoibua shangwe akitumbuiza kilele tamasha la Kizimkazi

By admin
August 17, 2026 1 Min Read
0

Unguja. Msaanii wa kimataifa kutoka Uganda, Jose Chameleone ameibua shangwe wakati akitumbuiza katika kilele cha tamasha la Kizimkazi.

Katika tamasha hilo linalofanyika leo Agosti 14, 2026 viwanja vya Mwehe Makunduchi, Mkoa wa Kusini Unguja, msanii huyo amepata fursa kutumbuiza nyimbo zake mbili, Jamila na Mama Mia.

Katika kibao chake cha Jamila, alishuka kutoka katika jukwaa la burudani na kusogelea meza kuu walipokaa viongozi wakuu wa kitaifa kutoka ndani na nje ya Tanzania.


Baada ya kufika katika jukwaa hilo, Rais Samia Suluhu Hassan alishuka kutoka kwenye kiti chake alipokuwa amekaa na kuongea na msanii huyo kisha kucheza naye wimbo huo wa mbona umeniacha.

Baada ya hapo aliondoka huku akiibua shwangwe kubwa kwa wananchi na viongozi waliofurika katika viwanja hivyo kwa ajili ya kusherehekea sherehe hizo.

Katika tamasha hilo pia wasanii wengine wa ndani na nje ya Tanzania wamepata fursa ya kutumbuiza.

Miongoni mwa wasanii hao ni Mrisho Mpoto, Sholo Mwamba, kikundi cha ngoma kutoka Dodoma cha Mahenza na ngoma ya asili ya Kizimkazi ya Shomoo.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Rais Samia ahimiza amani, utulivu Tamasha la Kizimkazi

Next

Asimulia alivyojifungua katikati ya tetemeko la ardhi

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • Wafugaji walalamikia operesheni za usiku, Serikali yajibu
  • Tanzania, DR Congo kuimarisha ushirikiano, kuondoa vikwazo
  • Watano wafariki dunia akiwamo mtoto mchanga, wanane wajeruhiwa Lushoto
  • Madeleka aeleza namna alivyokamatwa Mahakama Kuu
  • Makosa matatu yasababisha daladala 203 kufungiwa VTS

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme