Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Rais Samia ahimiza amani, utulivu Tamasha la Kizimkazi

By admin
August 17, 2026 3 Min Read
0

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amewahimiza Watanzania, hususan vijana, kulinda amani, usalama na utulivu, akisema maendeleo ya Taifa hayawezi kustawi katika mazingira ya vurugu.

Amesema amani, usalama na utulivu ni nguzo muhimu zinazowezesha uwekezaji, utalii, biashara, ajira na utoaji wa huduma za jamii, ambazo haziwezi kustawi katika mazingira ya vurugu na uvunjifu wa amani.

“Niwaombe Watanzania wenzangu, hususan vijana, msikubali kuharibu amani ya nchi yenu, amani ndiyo kila kitu katika maisha yenu, niwaombe sana mumkatae kwa nguvu zote yeyote asiyeitakia mema Tanzania yetu, tulinde nchi yetu pamoja na Muungano wetu kwa mustakabali wa kizazi kijacho,” amesema Rais Samia.



Rais Samia Suluhu Hassan amewakaribisha wawekezaji kutumia fursa zilizopo Kizimkazi, akisema miundombinu na miradi inayojengwa imeendelea kuvutia wafanyabiashara na uwekezaji.

Amesema mazingira mazuri ya uwekezaji yamewekwa, hivyo wote wanaoona fursa ndani ya wilaya hiyo… pic.twitter.com/eKjmtpPMPn

— Mwananchi Newspapers (@MwananchiNews) August 14, 2026

Rais Samia amesema hayo leo Ijumaa, Agosti 14, 2026, alipohitimisha Tamasha la Kizimkazi katika Uwanja wa Mwehe, Makunduchi, Zanzibar.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, akiwamo Makamu wa Rais, Dk Emmanuel Nchimbi, Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Ali Mwinyi, pamoja na viongozi wa vyama vya siasa na taasisi za umma.

Akizungumzia tamasha hilo, Rais Samia amesema limeleta chachu ya maendeleo katika wilaya za Kusini mwa Zanzibar kwa kuchochea biashara na kuongeza fursa za kiuchumi zinazoboresha maisha ya wananchi.

“Ndugu zangu, shangwe siku zote ni nzuri. Zinatuleta pamoja, zinaimarisha mshikamano na umoja, zinatusaidia kutangaza utamaduni wetu na kuvutia wageni. Kazi yetu kama viongozi ni kuhakikisha fursa zinazoibuliwa kupitia shangwe hizi zinawagusa wananchi wetu na tunaziunga mkono,” amesema.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Makamu wa Rais, Dk Emmanuel Nchimbi katika Kilele cha Tamasha la Kizimkazi lililofanyika leo Agosti 14, 2026, Makunduchi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Amesisitiza kuwa, Tamasha la Kizimkazi linapaswa kuwa lango la fursa za kiuchumi na chanzo cha ustawi wa wananchi na Taifa kwa jumla.

Amesema Wilaya ya Kusini imepata mabadiliko makubwa ikilinganishwa na mwaka 2016, kutokana na kuongezeka kwa fursa za biashara na uwekezaji.

Ameongeza kuwa ujenzi wa miundombinu na utekelezaji wa miradi mbalimbali umeendelea kuvutia wananchi na wawekezaji kuwekeza katika eneo hilo.

“Rais wa Zanzibar ameweka mazingira mazuri ya uwekezaji. Karibuni muwekeze. Tunaendelea kujenga uwanja wa michezo ambao utasaidia kufungua fursa mbalimbali wakati wa michuano ya AFCON itakayofanyika Juni 2027,” amesema.

Ameongeza kuwa uwanja huo utatoa fursa kwa wawekezaji kuwekeza katika huduma zitakazohitajika na wachezaji pamoja na wageni watakaoshiriki mashindano hayo.

Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Ali Mwinyi amemshukuru Rais Samia kwa kuanzisha Tamasha la Kizimkazi, akisema limekuwa na mchango mkubwa katika kutangaza utalii wa Zanzibar.

“Nawapongeza wananchi wote kwa mwamko mkubwa wa kushiriki tamasha hili na kutumia fursa zilizoambatana nalo, hakika mwaka huu tamasha limefana sana. Limekuwa jukwaa muhimu la kuhamasisha shughuli za maendeleo,” amesema na kuongeza:

Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza na msanii wa Uganda, Jose Chameleone wakati wa tamasha la Kizimkazi linalofanyika leo Agosti 14, 2026 viwanja vya Mwehe Makunduchi, Mkoa wa Kusini Unguja.

“Tumeshuhudia uzinduzi wa miradi mbalimbali ikiwamo ya maji, barabara, elimu, nyumba za makazi na viwanja vya michezo,” amesema.

Rais Mwinyi amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itahakikisha miradi yote iliyozinduliwa na itakayotekelezwa baadaye inatunzwa na kuendelezwa ipasavyo.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Hoja ya uhamiaji kutikisa mkutano wa wakuu wa SADC

Next

Jose Chameleone alivyoibua shangwe akitumbuiza kilele tamasha la Kizimkazi

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • Makosa matatu yasababisha daladala 203 kufungiwa VTS
  • Wadau kujadili maendeleo ya kidijitali, data ikipewa kipaumbele
  • *MKAKATI WA TAIFA WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA WAANZA KUTEKELEZWA MKINGA*
  • Wimbi la magonjwa ya upumuaji linavyoathiri watoto
  • PATRICK VIEIRA ATEULIWA KUWA KOCHA MKUU WA SENEGAL

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme