Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Wasira awataka wana-CCM kuhakiki taarifa za mitandaoni

By admin
August 19, 2026 2 Min Read
Comments Off on Wasira awataka wana-CCM kuhakiki taarifa za mitandaoni

Dar es Salaam. Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira, amewataka wanachama wa chama hicho kukutana mara kwa mara katika vikao rasmi ili kujadili masuala mbalimbali na kuepuka kupotoshwa na taarifa zisizo za kweli zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

Wasira ametoa kauli hiyo leo, Agosti 19, 2026, wilayani Ikungi, mkoani Singida, wakati akianza ziara rasmi ya kikazi ya kukagua uhai wa chama hicho.

Amesema vikao vya wanachama ni muhimu kwa kuwa vinatoa fursa ya kupata taarifa sahihi, kubadilishana mawazo na kuambiana ukweli kuhusu masuala yanayohusu chama na nchi.


“Wanachama wetu nchi nzima, kwa mujibu wa Katiba mna vikao vya wanachama. Mkutane muambizane. Siku hizi kwenye mitandao kuna uongo mwingi sana. Usipoangalia unaweza hata wewe kushirikishwa kusema uongo,” amesema.

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira, akisalimiana na makada wa chama hicho wilayani Ikungi, mkoani Singida, wakati wa ziara rasmi ya kikazi ya kukagua uhai wa chama hicho.

Wasira amesema umuhimu wa wanachama kutokubali taarifa zinazotolewa mitandaoni bila kuzihakiki, badala yake wazijadili katika vikao na kutafuta ufafanuzi kutoka kwa watu wenye ujuzi kuhusu suala husika.

“Kwa hiyo ni vizuri kukutana mkasema hili jambo limesemwa sana, maana yake ni nini? Mkamwita mtu anayejua akawasaidia kufafanua,” amesema.

Amesema vikao hivyo pia vinapaswa kutumika kujadili masuala mbalimbali yanayoendelea nchini ili kuwajengea wanachama uelewa na kuwawezesha kukitetea chama kwa hoja sahihi.

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira, akisalimiana na makada wa chama hicho wilayani Ikungi, mkoani Singida, wakati wa ziara rasmi ya kikazi ya kukagua uhai wa chama hicho.

Katika hatua nyingine, Wasira amesema CCM itaendelea kulinda uhuru na umoja wa Tanzania, akieleza kuwa mambo hayo ni sehemu ya misingi ambayo chama hicho kimepewa jukumu la kuilinda.

 “Hii ndiyo CCM. Kazi ya kwanza tulipewa ni uhuru na tunalinda. Ya pili ni umoja na tunahakikisha unabaki. Yeyote anayetaka kuubomoa anabomoa msingi ambao hawezi. Anaweza kutikisa matawi lakini mizizi itabaki chini,” amesema.

Wasira pia amekosoa kauli za baadhi ya watu wanaodai kuwa CCM haijafanya chochote tangu Tanzania ipate uhuru, akisema madai hayo hayana uhalisia.

“Wanasema hatujafanya chochote tangu uhuru. Lakini uhuru wa kusema ndio huo walionao. Mdomo una kazi mbili: kusema na kula. Mtu akisema hakuna chochote tangu uhuru, muache tu. Huyo ana matatizo anahitaji msaada,” amesema.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

DIT MWANZA YAONESHA NGUVU YA TEKNOLOJIA NA UZALISHAJI WA BIDHAA TANGA

Next

ACT yalaani Gazeti la MwanaHALISI kusitishiwa leseni

Recent Posts

  • Polisi yawashikilia 18 kwa madai ya kuchoma magari
  • ACT yalaani Gazeti la MwanaHALISI kusitishiwa leseni
  • Wasira awataka wana-CCM kuhakiki taarifa za mitandaoni
  • DIT MWANZA YAONESHA NGUVU YA TEKNOLOJIA NA UZALISHAJI WA BIDHAA TANGA
  • Mgambo wazunguka soko la mitumba, wafanyabiashara ‘wafungiwa’ biashara

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme