Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Close

Search

  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Subscribe
Habari

Tanzania, DR Congo kuimarisha ushirikiano, kuondoa vikwazo

By admin
August 18, 2026 4 Min Read
Comments Off on Tanzania, DR Congo kuimarisha ushirikiano, kuondoa vikwazo

Unguja. Rais Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), Felix Tshisekedi na kukubaliana kuimarisha ushirikiano katika maeneo makuu saba.

Maeneo hayo yamejikita katika, miundombinu, biashara, usafirishaji, kilimo, madini, reli na uvuvi, kuimarisha sekta binafsi na kuondoa vikwazo mipakani.

Akizungumza na waandishi wa habari Ikulu ndogo Zanzibar leo Agosti 18, 2026 Rais Samia amesema ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na DRC unatoa nafasi muhimu ya kuimarisha maeneo mengine ya kimkakati.

“Kwa muda mrefu tumekuwa tukishirikiana katika nyanja mbalimbali ikiwemo biashara, uchukuzi na miundombinu. Takwimu mpaka mwaka jana zinaonyesha kwamba nchi yetu hufanya biashara ya Sh794 bilioni, na DRC,” amesema.

Rais Samia amesema, bandari ya Dar es Salaam imeendelea kuwa lango muhimu la biashara kwa nchi ya DRC, wakati nchi hizo mbili zimeendelea kushirikiana kupitia ushoroba wa kati ambao ni mtandao jumuishi wa usafirishaji unaounganisha DRC na masoko ya kimataifa kupitia bandari ya Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Félix Antoine Tshisekedi Tshilombo akisaini Kitabu cha Wageni baada ya kuwasili Ikulu Ndogo ya Zanzibar, Agosti 18, 2026.

“Ni kwa msingi huo, leo katika mazungumzo yetu na Mheshimiwa Rais Tshisekedi tumeupa umuhimu mkubwa mradi wa miundombinu jumuishi ya uchukuzi (Multimodal Transportation Project),” amesema Rai Samia.

Amefafanua kuwa mradi huo una umuhimu mkubwa katika kuunganisha bandari, reli, barabara, na usafiri wa majini, na hivyo kupunguza gharama na muda wa usafirishaji wa mizigo kupitia Ziwa Tanganyika.

Amesema ushirikiano huo pia utaongeza ufanisi wa ushuru wa kati na kuchochea biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na DRC, pamoja na nchi nyingine jirani.

Samia amesema kwa sasa jitihada za kuendeleza miundombinu ya reli na vituo vya mizigo zinaendelea vyema ikiwemo mwendelezo wa SGR kuelekea maeneo ya magharibi, ambayo baadaye itaunganisha na nchi za Burundi na DRC.

Amesema wanaendelea pia na uboreshaji wa bandari kwenye Ziwa Tanganyika, ikiwemo Kigoma, Tarema, Moba, na Kalemi.

“Mtakumbuka hivi karibuni nikiwa Kigoma nilizindua meli kwa ajili ya kutoa huduma kwenye Ziwa Tanganyika, meli nne na bado tuna jenga nyingine nne ili kurahisisha usafirishaji wa mizigo pia.”

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mhe. Félix Antoine Tshisekedi Tshilombo akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ikulu Ndogo ya Zanzibar,  Agosti, 2026.

Amesema asilimia takribani 60 ya mizigo inayopita bandari ya Dar es Salaam ni kutoka DRC, kwa hiyo ni lazima wawe na vyombo vingi vya kusafirisha kwenye maji vitakavyoweza kubeba na kupunguza mzigo Dar es Salaam.

Ametumia fursa hiyo kuipongeza serikali ya DRC kwa kuanza ujenzi wa barabara ya Kalemi-Manono, ambayo itakapokamilika itaunganisha zaidi mataifa hayo na kuchochea shughuli za kiuchumi kwenye nchi mbili na ukanda mzima wa Afrika Mashariki na Kati.

Sambamba na hayo, kwenye mazungumzo yao pia wawili hao wamesisitiza umuhimu wa kuimarisha biashara kwa kuondoa vikwazo visivyo vya lazima, kuboresha huduma za mipakani, na kuwezesha sekta binafsi kushiriki kikamilifu kadri fursa zinazojitokeza.

“Na tunashukuru Mheshimiwa Rais wa DRC ameeleza jinsi wanavyoishirikisha sekta binafsi katika ujenzi wa reli kule kwao, lakini na barabara pia, na hata huduma za bandari kama tunavyofanya sisi hapa ili kuharakisha utekelezaji wa miundombinu hiyo,” amesema

Katika hatua nyingine, Rais Samia amesema,”Nimemweleza    Rais wa DRC kwamba, Tanzania inazalisha kwa wingi bidhaa za kilimo, uvuvi, na mifugo, hivyo nawakaribisha kufanya biashara katika maeneo hayo pia.”

Amesema Tanzania na DRC zina utajiri wa rasilimali za madini, na hivyo wamekubaliana kushirikiana katika maeneo hayo, kubadilishana uzoefu na ujuzi, jinsi ya uchimbaji, uongezaji thamani na hata masoko ya madini.

Pia amesema wamewaalika waungane katika kituo cha madini kilichopo nchini kwa ajili ya nchi za Afrika Mashariki na Kati.

“Waungane nasi tubadilishane ujuzi, lakini pia utafiti katika kituo kile.”

Amesema pia katika mazungumzo yao pia  wamegusia masuala ya amani na usalama, ambayo ni nguzo muhimu katika mustakabali wa maendeleo ya mataifa hayo.

Kwa upande wake, Rais Tshisekedi amesema wamechunguza maeneo kadhaa ambayo tayari wanashirikiana, lakini ambayo wanapaswa kuyaimarisha, na katika maeneo mengine ambayo bado hayajachunguzwa.

“Ndiyo maana kumefanyika uamuzi wa kuifufua tume ya pamoja, tume mchanganyiko, niseme, ili kazi ifanyike kwa kina zaidi, kwa mpangilio na kwa ufanisi,” amesema.

Rais huyo wa DRC amesema ndio maana wamesisitiza zaidi masuala ya amani, usalama na utulivu.

“Pia tumetazama masuala ya kibiashara, masuala ya kubadilishana, kupitia ujenzi wa miundombinu, na kuweka mifumo inayowezesha mabadilishano hayo ya kibiashara. Na naweza kuwaambia kwamba naondoka hapa nikiwa na furaha kubwa na nina matumaini makubwa kuhusu mustakabali mzuri wa ushirikiano kati ya nchi zetu mbili,” amesema Rais Tshisekedi.

Amesema, “Huu ndiyo hasa aina ya ushirikiano unaopaswa kuwa kati ya nchi za Kiafrika. “Tuna ardhi, Afrika, bara ambalo limejaa fursa nyingi za maliasili, lakini pia lina nguvu nyingine ambayo mimi naiona kama muhimu zaidi ambayo ni rasilimali watu.”

Amesema takriban asilimia 60 ya idadi ya watu wa Afrika imeundwa na vijana ambao ni dhamana ya mustakabali thabiti. “Kwa sababu vijana wanapaswa kuelekeza tu na kuingia kazini. Kazi hiyo tutaiweka sawa tu pale tutakapotimiza kinachotia moyo yaani kufaulu kubadilisha maliasili zetu wenyewe hapa barani,” amesema.

 “Tumechoka sasa kuwa ardhi ya uchimbaji tu, ambapo tunaona madini yetu yanatoka ardhini yakiwa mabichi na kwenda kubadilishwa thamani mahali pengine, kupata thamani iliyoongezwa mahali pengine, wakati barani tunaweza kufanya hayo,” amesema

Rais Tshisekedi amemshukuru Rais Samia kumpa rambirambi kuhusu ugonjwa wa Ebola ambapo pia huo ni uthibitisho wa uimara huo wa Afrika.

“Ningependa kueleza ndugu zetu Watanzania kuhusu Ebola,tupo kwenye mlipuko wa 17 na kwa hiyo tumepitia milipuko yote 16, hivyo  msiruhusu kabisa jambo hili likutisheni,”

Amesema  wana uzoefu unaotambuliwa duniani kote katika kudhibiti na kukabiliana na ugonjwa huo.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Watano wafariki dunia akiwamo mtoto mchanga, wanane wajeruhiwa Lushoto

Next

Wafugaji walalamikia operesheni za usiku, Serikali yajibu

Recent Posts

  • Serikali yatoa siku nane kwa wazalishaji saruji kushusha bei
  • Mchengerwa ataja vipaumbele sita kupunguza vifo vya mama, mtoto
  • Babu adai kupigwa ngwara na mwalimu Bahi
  • Kibwagizo cha wimbo wa ‘kilio cha mtu mzima’ kilivyotumika kesi ya ardhi
  • Mwili wa mtoto wa miaka saba wakutwa shimoni Tabora

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
  • Michezo
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme