Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Subscribe
Close

Search

Habari

NAIBU WAZIRI NDERIANANGE AWATIA MOYO WENYE ULEMAVU IRINGA ATAKA WACHANHAMKIE FURSA YA MIKOPO

By admin
August 17, 2026 4 Min Read
0

  

NA MATUKIO DAIMA

MEDIA

IRINGA.Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na anayeshughulika na watu wenye  Ulemavu, Ummy Nderianange amewataka watu wenye ulemavu kutumia mikopo inayotolewa na Serikali kama fursa ya kujikwamua kiuchumi na kubadili maisha yao, badala ya kuichukulia kama msaada au hisani.

Naibu Waziri ameyasema hayo leo, Agosti 17, 2026, katika Ofisi za Mkoa wa Iringa, wakati wa ziara yake ya kutoa elimu kwa watu wenye ulemavu kuhusu fursa mbalimbali zinazopatikana kwa ajili ya kuwawezesha kiuchumi na kijamii.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuweka mazingira wezeshi kwa watu wenye ulemavu kupata mikopo na fursa nyingine za kiuchumi, huku akibainisha kuwa kiasi kikubwa cha fedha tayari kimetolewa kwa wanufaika nchini. 

Amesema awali watu wenye ulemavu nchini walikuwa wameweza kukopa kiasi cha takribani shilingi bilioni 5, lakini takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kuwa kiwango hicho kimeongezeka na kufikia shilingi bilioni 23, jambo alilolitaja kuwa ni ongezeko kubwa linaloonesha mwamko wa watu wenye ulemavu katika kutumia fursa za uwezeshaji.

Amesema ongezeko hilo ni ishara kuwa watu wenye ulemavu wameanza kutambua na kutumia fursa zinazotolewa kwa ajili ya kuanzisha na kuendeleza shughuli za kiuchumi, hivyo kuwataka kuendelea kujitokeza na kutumia fursa hizo kwa maendeleo yao na familia zao.

“Mafanikio ya baadhi ya watu wenye ulemavu waliopata mikopo yanapaswa kutumika kama mfano na kuwahamasisha wengine kuchangamkia fursa hizo”

Aidha Waziri Ummy  ameitaka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kujitathmini katika utoaji wa mikopo kwa watu wenye ulemavu, akibainisha kuwa kiwango kilichotolewa katika manispaa hiyo bado ni kidogo ikilinganishwa na mahitaji yaliyopo. 

“Serikali za mitaa zinapaswa kuhakikisha fursa za mikopo zinawafikia walengwa, huku wakitenga pia maeneo maalumu ambayo watu wenye ulemavu wanaweza kufanya shughuli za uzalishaji na biashara”

Naibu Waziri huyo amepongeza ushirikiano uliopo kati ya Serikali na viongozi wa vyama vya watu wenye ulemavu mkoani Iringa, akisema ushirikiano huo unarahisisha utatuzi wa changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu,amesema viongozi wa Serikali na wawakilishi wa watu wenye ulemavu wanapaswa kuwa karibu zaidi ili kuhakikisha changamoto na mahitaji ya kundi hilo yanafikishwa kwa mamlaka husika kwa wakati.

Ameeleza kuwa Serikali pia inaendelea kuhamasisha uwepo wa maeneo maalumu yenye huduma mbalimbali kwa watu wenye ulemavu, ambapo wanaweza kupata huduma kwa pamoja na kuendesha shughuli za kiuchumi. 

Amesema maeneo hayo yanaweza kuwa na shughuli za biashara, ubunifu na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali, hivyo kuwawezesha watu wenye ulemavu kupata kipato na kujitegemea badala ya kutegemea msaada.

Kwa upande wake, Mmoja wa walemavu wa ngozi (Albino) Sambala amewaomba viongozi wa mkoa, wilaya na halmashauri kuendelea kutenga sehemu ya bajeti kwa ajili ya kuwawezesha watu wenye ulemavu, pamoja na kutafuta maeneo kwa ajili ya shughuli zao za uzalishaji. 

Amesema hatua hizo zinaendana na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuhakikisha Watanzania wanaishi kwa tabasamu, huku akisisitiza kuwa mafanikio ya watu wenye ulemavu yatakuwa sehemu muhimu ya kutimiza dhamira hiyo.

Akisoma taarifa ya manispa  katika ziara ya Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu wa Watu Wenye Ulemavu, shughuli hizo zimewezesha baadhi ya wanufaika kuongeza mitaji ya biashara, kuboresha maisha yao na wengine kuweza kuajiri watu katika shughuli zao, Halmashauri imeeleza kuwa moja ya changamoto kubwa iliyopo ni baadhi ya wanufaika kushindwa kurejesha mikopo kwa wakati.

Akizungumzia changamoto hiyo, viongozi wa watu wenye ulemavu wamesema bado kuna haja ya kuongeza elimu kuhusu mikopo hiyo, hususan kwa kuwa baadhi ya wanufaika wamekuwa wakiichukulia kama msaada au hisani kutoka Serikalini. 

“Elimu hiyo inapaswa kutolewa kabla ya vikundi kupokea fedha, ili wanufaika waelewe masharti ya mikopo, matumizi sahihi ya fedha na wajibu wao wa kurejesha,wamependekeza kuwepo kwa utaratibu endelevu wa kutoa elimu kwa wanufaika wa mikopo, badala ya kufanya hivyo siku chache kabla ya fedha kutolew,elimu ya mara kwa mara itasaidia kuwawezesha watu wenye ulemavu kuelewa fursa zilizopo, kuendesha shughuli zao kwa ufanisi na kuongeza uwezekano wa kurejesha mikopo kwa wakati”alisema 

TAZAMA VIDEO BOFYA LINK HII

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Wabunifu zaidi ya 300 kushiriki maonyesho Tanga

Next

BIDHAA ZA CHAKULA ZISIZOKIDHI MATAKWA YA VIWANGO ZATEKETEZWA .

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • BIDHAA ZA CHAKULA ZISIZOKIDHI MATAKWA YA VIWANGO ZATEKETEZWA .
  • NAIBU WAZIRI NDERIANANGE AWATIA MOYO WENYE ULEMAVU IRINGA ATAKA WACHANHAMKIE FURSA YA MIKOPO
  • Wabunifu zaidi ya 300 kushiriki maonyesho Tanga
  • Bunge lasogezwa mbele kupisha sherehe za Maulid
  • Agizo la Chalamila Stendi ya Magufuli lapingwa

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
  • Magazeti
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme