Skip to content
-
Subscribe to our newsletter & never miss our best posts. Subscribe Now!
  • https://www.facebook.com/
  • https://twitter.com/
  • https://t.me/
  • https://www.instagram.com/
  • https://youtube.com/
Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

Habarimpya

Habari Mpya Kilasiku

  • Home
  • Sample Page
  • Home
  • Sample Page
Subscribe
Close

Search

Habari

Jamhuri yafunga ushahidi kesi ya Lissu

By admin
August 17, 2026 2 Min Read
0

Dar es Salaam. Jamhuri imefunga ushahidi wake katika kesi ya uhaini  inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu, 

Jamhuri imefunga ushahidi huo leo Jumatatu Agosti 17, 2026 baada ya kuwaita mashahidi 17 kati ya 30 waliokuwa wameorodheshwa.

Katika kesi hiyo Lissu anakabiliwa na shtaka moja la uhaini kinyume na kifungu cha 39(2) (d) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, linalotokana na maneno aliyoyatamka kuhusiana na kusudio la kuzuia kufanyika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.



Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, amefikishwa katika Mahakama Kuu, Masjala Ndogo Dar es Salaam leo Jumatatu, Agosti 17, 2026, kwa ajili ya kuendelea na usikilizwaji wa kesi ya uhaini inayomkabili, ambapo upande wa mashtaka unatarajiwa… pic.twitter.com/l1Y1h4IWGG

— Mwananchi Newspapers (@MwananchiNews) August 17, 2026

Anadaiwa kuwa Aprili 3, 2025, jijini Dar es Salaam, akiwa raia wa Tanzania, kwa nia ya uchochezi alishawishi umma kuzuia kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, kwa kutamka na kuandika maneno ya kumshinikiza kiongozi mkuu wa Serikali ya Tanzania, kuwa:-

“Wakisema msimamo huu unaashiria uasi, ni kweli…, kwa sababu tunasema tutazuia uchaguzi, tutahamasisha uasi, hivyo ndivyo namna ya kupata mabadiliko… kwa hiyo tunaenda kikinukisha…, sana sana huu uchaguzi tutaenda kuuvuruga kwelikweli… tunaenda kukinukisha vibaya sana…”

Kesi hiyo inasikilizwa na Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam na jopo la majaji watatu linaloongozwa na Jaji Dunstan Ndunguru, Jaji James Karayemaha na Ferdinand Kiwonde, ilipangwa kuendelea leo kwa ushahidi wa upande wa Jamhuri.

Hata hivyo baada ya kesi kuitwa Jamhuri kupitia mwendesha mashtaka Wakili wa Serikali  Mkuu Ajuaye Nzegeli ameieleza Mahakama kuwa baada ya kupitia ushahidi uliokwishawasilishwa na kuangalia ushahidi wa mashahidi waliosalia wameona ushahidi waliokwishawasilishwa unatosheleza.

“Hivyo tunapenda kuitaarifu Mahakama hii tukufu kuwa upande wa Jamhuri unafunga ushahidi wake kwa mashahidi 17”, amesema Wakili Nzegeli.

Viongozi wa Chadema, akiwemo Rugemeleza Nshala, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Boniface Jacob, ‘Boni Yai’, pamoja na wafuasi wa chama hicho, wamejitokeza katika Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, leo Jumatatu Agosti 17, 2026 kwa ajili ya kuendelea kwa usikilizwaji wa kesi… pic.twitter.com/jdXHxW30TK

— Mwananchi Newspapers (@MwananchiNews) August 17, 2026

Baada ya Jamhuri kufunga ushahidi wake sasa kesi imeingia katika hatua ya pili ambapo pande zote zinawasilisha hoja kuishawishi mahakama kama mshtakiwa kwa ushahidi huo ana kesi ya kujibu au la.

Kwa sasa ameanza mshtakiwa Lissu kuwasilisha hoja zake kuishawishi Mahakama kuwa upande wa mashtaka umeshindwa kuonesha kuwa kuna kesi ya kumfanya ajitetee, kabla ya upande wa mashtaka kujibu hoja hizo kuionesha Mahakama kuwa imeweza kujenga kesi kiasi cha kumlazimu mshtakiwa kujitetea kabla ya kutoa hukumu.

Author

admin

Follow Me
Other Articles
Previous

Lissu alivyoishawishi Mahakama hana kesi ya kujibu, aomba fidia

Next

Wajenzi wanavyokiuka vibali vya ujenzi, hatari kwa watumiaji

No Comment! Be the first one.

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recent Posts

  • Ziara ya Rais Tshisekedi kufungua ukurasa mpya wa biashara, amani
  • SEKTA YA MADINI YAVUTIA UWEKEZAJI WA TRILIONI 9 NDANI YA MIAKA MINNE*
  • VETA YAANDAA MTAALA WA MAFUNZO YA MUDA MFUPI WA FANI YA RECYCLING
  • VETA IMETAKIWA KUENDELEA KUWASHIRIKISHA WATAALAMU WALIOBOBEA FANI MBALIMBALI
  • BAHI IMETENGA MILLION 100 KUTOKA MAPATO YAKE YA NDANI KUSAIDIA VIJANA WA WILAYA KUPATA ELIMU VETA

Recent Comments

  1. A WordPress Commenter on Hello world!

Archives

  • August 2026

Categories

  • Habari
Copyright 2026 — Habarimpya. All rights reserved. Blogsy WordPress Theme